Bwana Yesu asifiwe…
Ninakukaribisha
katika uchambuzi wa makanisa saba ikiwa leo ni siku ya tano ya
uchambuzi huu. Ukweli ni kwamba ninachambua kwa ufupi kwa kila
kanisa,maana nikisema nikuandikie yote,basi ni dhahili fundisho hili la
makanisa yale saba litakuwa ni fundisho lefu kuliko mafundisho yote
niliyopata kuandika. Lakini pia zipo jumbe nyingi sana katika kila moja
ya barua kwa kanisa kama ilivyoandikwa katika Ufunuo 2&3.
Siku ya leo tutamaliza ufafanuzi wote kwa kuyaangalia kwa kifupi juu ya makanisa matatu ya yaliyobakia,ambayo ni;
◇Kanisa la Laodikia.
◇Kanisa la Efeso.
◇Kanisa la Smirna.
[V] KANISA LA LAODIKIA.
~ Laodikia ilikuwa kama kilomita sabini kusini mashariki mwa Filadelfia.
~
Inasemekana mji uligunduliwa na mfalme Antiochus II Theos(261-246
BCE).Mfalme huyu akauita jina la mji huu Laodoce jina la mke wake.
~ Mji huu ulikuwa ni tajiri.
~ Mji huu ulikuwa maarufu kwa ustawi wake na ulikuwa na shule maarufu ya UTABIBU.
~ Mahali hapa palisifika na kuwa na manyoya mazuri,lakini pia kulikuwa na dawa ya macho maarufu ulimwenguni.
~ Kanisa hili halipo hai hivi sasa,na limebakia magofu tu.
“Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. ” Ufunuo 3:18
Bwana
Yesu anatuonesha utoshelevu wake,anamwambia Laodikia atafute utajiri wa
kweli ndani yake Bwana Yesu pia Laodikia wapate kuona sawa sawa,maana
walidhani wana dawa nzuri ya macho ingawa walikuwa bado ni vipofu-Yesu
pekee ndie dawa ya kufungua waliofungwa na kwa walioonewa na ibilisi.
( Ufunuo
3:20)Laodikia,amepewa nafasi ya kufungua mlango ili Bwana
aingie,Laodikia wa leo ni wewe,tazama-Bwana anabisha ukisikia na
kufungua yeye ataingia ndani ya moyo wako. Bwana Yesu anakutazamia
uokoke,aingie ndani yako uwe kiumbe kipya.
[VII] KANISA LA EFESO.
~Efeso ulikuwa ni mji mkubwa na tajiri sana katika ulimwengu wa zamani
~Kulikuwa na bandari juu ya Asia ndogo,hivyo Efeso ulikuwa ni makao ya biashara na usafiri.
~Hapa
ndipo palipokuwa na hekalu kubwa la Artemi pia Artemi alijulikana kama
Diana. Artemi alikuwa mungu wa uzazi,hivyo aliabudiwa sana.
~ Mji ukawa maarufu hata kwa biashara,(Matendo 19:23-24) & Matendo 19:34.
~ Leo,kanisa hili limebaki magofu,pia ndipo pana eneo kubwa sana kuliko maeneo ya makanisa yote sita. ~ Pana eneo la michozo la kizamani.
~ Leo,kanisa hili limebaki magofu,pia ndipo pana eneo kubwa sana kuliko maeneo ya makanisa yote sita. ~ Pana eneo la michozo la kizamani.
Bwana
Yesu analisifu kanisa hili kwamba katikati ya miungu na mchanganyiko wa
mafundisho ya uongo,lenyewe bado lilikuwa na subira kwa Bwana(Ufunuo
2:3)
~Subira ni
jambo la msingi sana katika maisha ya mkristo. Wengi siku ya leo
wamekosa subira maana hata kuomba kwao wanataraji kujibiwa papo hapo.
Mpendwa kuwa na subira kwa Bwana,Yeye MUNGU ni mwaminifu hawai wala
hachelewi.
[VII] KANISA LA SMIRNA.
~Hili
ndilo kanisa la pekee lililobaki hai mpaka leo. Makanisa sita
hayaendelei na ibada zao,lakini kanisa hili linaendelea na ibada zake.Hivyo ni kanisa moja la kipekee kabisa tofauti na yale saba.
~Smirna sasa ni Izmir,ulikuwa ni kilomita hamsini kaskazini mwa Efeso.
~Lakini pia Smirna ulijulikana kwa ibada za kipagani,ingawa barua ya kanisa hili imewaja na faraja.
Hivi sasa,watu waendao kujifunza habari za mkanisa,hupitia kufanya ibada mahali hapa.
~Kanisa hili lipo chini ya Warumi.
Jambo moja kubwa na la msingi ambalo Bwana Yesu anawaambia watu wa kanisa la Smirna ni; ◇ Wasiogope majaribu,bali wawe waaminifu hata kufa.
Jambo moja kubwa na la msingi ambalo Bwana Yesu anawaambia watu wa kanisa la Smirna ni; ◇ Wasiogope majaribu,bali wawe waaminifu hata kufa.
”
Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi
yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa 3na dhiki siku kumi. Uwe
mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima. “Ufunuo 2:10
Bwana
Yesu leo anasema na wewe maneno hayo hayo,kwamba majaribu hayana budi
kuja kwako,lakini usiogope kupitishwa majaribuni maana ndipo mahali
pekee pa kupanda ngazi kiroho . Lakini uwe MWAMINIFU HATA KUFA,yaani
pale inapobidi kufa kwa uaminifu basi ni bora kufa kuliko kumkosa Bwana
Yesu mwenye mbingu. Hapa,panatutaka hata kupoteza mali na pesa kwa ajili
ya uzuri wa Bwana MUNGU.
![]() |
Na Mtumishi Gasper Madumla |
@ Mtumishi Gasper Madumla.
MWISHO.
UBARIKIWE.
Comments