MTUME PETER RASHID ABUBAKAR AWAFUNDISHA WATEULE HUKO BURUNDI JINSI YA KUANGAMIZA UCHAWI.

Mtumumishi wa MUNGU Peter Rashid Abubakar siku za karibuni alikuwa Bujumbura Burundi kihuduma.
Zifaatazo ni habari picha katika matukio tofauti kwenye zaidi ya siku 2 za watu kufunguliwa, pia alifundisha kuhusu jinsi ambavyo wateule wanaweza kuwashinda wachawi, hili ni somo katika moja ya ibaada hizo huko Bujumbura Burundi.
 
MUNGU alimtumia mtumishi wake kuwaombea na kuwafungua mamia ya watu kwa jila kuu la YESU KRISTO.
Mtume Peter Rashid Abubakar akiihubiri injili ya yesu. Hapa anaonekana akiwa na mtafisiri wake au mkalimani wake jijini Bujumbura.
 
Senior Pastor Peter Rashid Abubakar akiwa Burundi-Bujumbura alifundisha kanisani somo la  kuuangamiza uchawi wa MISHALE;TERAFI NA MAINI Alisoma Ezekiel 21:21. Maana mfalme wa Babeli alisimama penye njia panda, Penye kichwa cha njia hizo mbili, ili atumie uganga; alitikisa Mishale huko na huko, akaziuliza TERAFI akayatazama MAINI. For the king of Babylon stood at the parting of the way, at the head of the two ways, to use divination;he made his arrows bright,he consulted with images,he looked in the liver.
 
 
 Senior Pastor/Mtume Peter Rashid Abubakar alifanunua akisema: Wapo wafalme wengine wanahofu ya Mungu wengine wachawi kama huyu Mfalme wa Babeli alisema leo tunaangamiza uchawi aina 4: 1. Penye kichwa cha njia: watu wengi hawafahamu kama hata njia zina vichwa wengi wanajua njia ni njia tu kumbe ili mchawi akuroge hasimamima kwenye njia tu ili mradi njia hapana hutafuta kichwa cha njia na kisha anasimama kwenye kichwa hicho cha njia ndipo anaanza KUNUIZA UCHAWI WAKI TENA KWA KUWATAJA WALE ALIOKUSUDIA KUWAROGA 2.Alitikisa MISHALE huko na huko ikimaanisha pande nne za dunia ipo mishale ya kichawi ikirushwa inamfikia yule aliyekusudiwa ndio wale unawasikia wakilalamika mara nasikia vichomi visivyoisha mwilini mwangu hiyo ni mishale ya kichawi, mwingine anatembea na MSHALE na ulikusudiwa ifikapo siku fulani na tarehe fulani na mwaka fulani huo MSHALE utamuua ndio wale unaweza kusikia kuwa FULANI AMEKUFA!! watu wanaanza kushangaa huku wakisema Mmh! Mm nilikuwa naye tu na tuliagana kwa amani!! Amekufa!!!? Huo ni mshale wa kichawi 3.
 Aliziuliza TERAFI swali terafi ni nini? Terafi naweza nikafafanua ni VITABU VINAVYOFUNDISHA ELIMU YA UCHAWI kama vile unaweza kusikia KITABU CHA FARAKI;YAASINI;RUKYA;ALGHAZAR etc kiasi kwamba mchawi aliyesomea uchawi huo hawezi kufanya uchawi wake hadi aviulize hivyo VITABU ili vimpatie maelekezo mazuri asije akakosea ktk kazi zake! Sasa basi alipozotazama hizo TERAFI 4. Ndipo alipoyaona MAINI yapo safi yanafanya kazi vizuri ndipo kupitia uchawi huo akayaharibu maini yakawa hayafanyi kazi! Ndio maana watu wengi sasa hivi waweza kuwasikia wakisema jamani jamani mm maini yangu nimepimwa na Doctor wameniambia maini yote yameharibika au ini moja limeharibika!! Kumbe huo ni uchawi uliotumika. Senior Pastor Peter Rashid Abubakar aliombea watu wengi na kufunguliwa kwa kukausha wafalme au viongozi wakubwa wa serkali wanaotumia uchawi huo ktk jina la yesu, kisha alivunja vunja vichwa vyote vya njia mahali wanaposimama wachawi ktk jina la yesu pia VITABU vyote vya uchawi alivichoma vyote ktk ulimwengu wa roho kwa moto wa Mungu. 
Siku Mtume Peter Rashid alipowasili Burundi. Hapa akiwa Air port na mke wake Pamela.
Hakika wengi walifunguliwa.

Comments