Watoto 132 wazaliwa mkesha wa Krismasi, Wakiume 77 na wakike 55.

Kina mama wakiwa na watoto wao katika Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam jana baada ya kujifungua katika mkesha wa Krismas. Picha na Venance Nestory 


 Watoto 132 wamezaliwa usiku wa kuamkia Sikukuu ya Krismasi katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Morogoro.
Muuguzi mkuu wa zamu wa Hospitali ya Amana, jijini Dar es Salaam, Teresia Akida alisema kati ya watoto 52 walizaoliwa wakiume ni kiume ni 31 na wa kike 21.

Alisema mmoja wa wazazi wa watoto hao, Asha Abdallah alijifungua watoto watatu wa kiume ambao bado hawajatimiza miezi, hivyo wamehifadhiwa kwenye mashine za watoto njiti.

“Watoto wote wanaendelea vyema na hali afya zao ukiacha hao watatu ambao bado wapo katika uangalizi maalumu.

“Pia, kuna pacha wengine wawili wa kike na wa kiume ambao wamezaliwa na afya njema,” alisema.

Abdallah alisema anaendelea vizuri na afya yake isipokuwa watoto wanaendelea na matibabu.

“Licha ya kuwa na hali hii lakini wananyonya vizuri maziwa,” alisema.

Kwa upande wa Hospitali ya Temeke, watoto 19 walizaliwa, wakiwamo tisa wa kike tisa na 10 wa kiume.

Ofisa muuguzi wa hospitali hiyo, Grace Rusya alisema watoto hao wamezaliwa katika njia za kawaida na wakiwa na afya njema.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala, Sophianias Ngonyani alisema kati wa watoto 30 waliozaliwa, wa kiume 17 na wakike 13.

Katika hatua nyingine; watoto 20 walizaliwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

Muuguzi wa zamu wa hospitali hiyo, Mariam Mazengo alisema watoto sita wamezaliwa kwa njia ya upasuaji na wengine 14 kawaida.Mazengo alisema watoto wanane kati ya 20 ni wa kike.
Mkoani Tanga, watoto 11 walizaliwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo wakiwamo pacha wa kike na kiume waliozaliwa kwa njia ya upasuaji.

Muuguzi wa zamu wodi ya wazazi, Ashirina Mwanyoka alisema watoto wa kiume ni saba na wa kike wanne. Alisema watoto wote na mama zao wako salama kiafya.

Comments