ILIKUWA FURAHA KUU KWA ABEL SHIRIWA NA NEEMA DAVID BAADA YA KUFUNGA NDOA TAKATIFU.

Mtumishi wa MUNGU Abel Suleiman Shiriwa akiwa na mkewe Neema David Sempol mara baada ya kufunga ndoa katika kanisa  TAG Mbagala kuu

Kama kuna matukio muhimu katika maisha basi tukio la ndoa ni moja ya matukio muhimu sana. Ni heshima kubwa sana kufikia hatua hii ya kufunga ndoa takatifu kanisani. Kila mtu hufurahi, wazazi hufurahi na kuheshimiwa, wahusika hufurahi maana MUNGU amejibu hitaji lao la ndoa. 

Hakika huwa ni furaha kuu. Siku za karibuni Mtumishi wa MUNGU Abel Shiriwa alifunga ndoa na dada Neema  David walifunga ndoa  takatifu katika kanisa la T A G Mbagala kuu jijini Dar es salaam. Ndoa hiyo ambayo ilihudhuriwa na watu wengi ilifungishwa na Mchungaji Charles Aloyce Wandwi. Sherehe ilifana  na hakika BWANA atukuzwe kwa hili. Zifuatazo ni baadhi ru ya picha katika baadhi ya matukio katika siku hiyo.




 

 
 

 

 

 

Comments