Karibu tule
chakula cha uzima.
Wateule wa
YESU kwa jina jingine huitwa Wanafunzi wa YESU(Matendo 11:26, …. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima
wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi
waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia.).
Wanafunzi wa
YESU lazima wawe wamejifunza kwa YESU kupitia Neno lake Biblia, Tena wakidumu
katika neno lake na kulishika na kulitii (Yohana 8:31-32, Basi YESU akawaambia wale Wayahudi
waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli
kweli; tena
mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.).
Wanafunzi wa
YESU ni wale walioivaa nira yake(Mathayo 11:29-30, Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa
mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa
maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.).
Hizo ni sifa
za wanafunzi wa YESU lakini zipo tabia pia za wanafunzi wa YESU na yapo maisha
pia ambayo wanatakiwa kuishi wanafunzi wa YESU.
-Tabia njema
ni jambo la muhimu sana kwa kila mwanafunzi wa YESU.
-Mwana wa
MUNGU ni Yule tu anayemheshimu MUNGU.-Tabia mbaya inaweza kuwa kikwazo cha watu wengine kuokolewa. Ziko nyingi ila Leo nazungumzia maisha ya wanafunzi wa YESU.
MAISHA YA WANAFUNZI WA KWELI WA YESU KRISTO.
1.Huushinda
ulimwengu (1 Yohana 5:4, Kwa
maana kila kitu kilichozaliwa na MUNGU huushinda ulimwengu; na huku ndiko
kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu. ).
Kuushinda ulimwengu ni kushinda dhambi,
kushinda mambo ya kidunia yaliyo machukizo kwa MUNGU na kuwashinda mawakala wa
shetani wote.
2.
Hujitenga
na anasa za dunia(1 Yohana 2:15-17, Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika
dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda BABA hakumo ndani yake. Maana kila
kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha
uzima, havitokani na BABA, bali vyatokana na dunia. Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake,
bali yeye afanyaye mapenzi ya MUNGU adumu hata milele. )
3.
Hawaendi katika njia ya wasio haki na wala
hawakai barazani pa wenye mizaha( Zaburi 1:1-3 , Heri mtu yule asiyekwenda
Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala
hakuketi barazani pa wenye mizaha. Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na
sheria yake huitafakari mchana na usiku. Naye atakuwa kama mti uliopandwa
Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani
lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.). Shauri la wasio haki ni
kwenye mambo au vikao vya watu wanaopanga mabaya, ni kwenye ajenda za kupinga
Wokovu. Njia ya wakosaji ni kwenye mambo yote ya dhambi, baraza la wenye mizaha
ni kwa wanaokejeli injili na ukombozi wa Mwanadamu kupitia YESU KRISTO.
4.
Ni
waombaji(Waefeso 6:18, kwa sala zote na
maombi mkisali kila wakati katika ROHO, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu
katika kuwaombea watakatifu wote;).
Maombi ni maisha, maombi ni mkono mrefu
zaidi wa kupokea kutoka kwa MUNGU.
Maombi huwaweka huru watu, maombi ni maisha
ya waenda mbinguni
5.
Humtumikia
MUNGU(Yoshua 24:14-15, Basi sasa mcheni BWANA, mkamtumikie kwa unyofu wa moyo
na kwa kweli; na kuiweka mbali miungu ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya
Mto, na huko Misri; mkamtumikie yeye BWANA. Nanyi kama mkiona ni vibaya
kumtumikia BWANA, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile
ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale
Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia
BWANA.). Ni heri kumtumikia BWANA MUNGU. Wanafunzi wa kweli wa YESU KRISTO humtumika
MUNGU tu. Hujiepusha na miungu na sanamu zote, hujepusha na usoma nyota,
unajimu, mizimu na kila machukizo.
6.
Huongozwa
na ROHO MTAKATIFU(Warumi 8:14, Kwa kuwa
wote wanaoongozwa na ROHO wa MUNGU, hao ndio wana wa MUNGU.). Wanafunzi wa YESU
huongozwa na ROHO MTAKATIFU.
ROHO hutukumbusha, hutufariji, hutufundisha,
hutuonya, hutuelekeza na hutufunulia tusiyoyajua na hata mafumbo ya MUNGU. ROHO MTAKATIFU ni muhimu kuliko vyote kwa
mteule wa MUNGU.
7.
Huishi
maisha matakatifu(Wakolosai 1:21-22, Na ninyi, mliokuwa hapo kwanza
mmefarikishwa, tena adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya,
amewapatanisha sasa; katika mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake, ili awalete
ninyi mbele zake, WATAKATIFU, wasio na mawaa wala lawama;)
Manafunzi
anaambiwa hivi ‘’katika mambo yote
ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika
mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu, na maneno yenye uzima
yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa
hana neno baya la kunena juu yetu.- Tito 2:7-8’’
Ndugu yangu,
hakikisha unakuwa mwanafunzi wa kweli wa YESU kwa kumtii MUNGU.
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Comments