BWANA YESU
atukuzwe ndugu yangu.
Karibu tena
tujifunze habari njema za MUNGU aliye hai.
Warumi 8:1-2
‘’ Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika KRISTO YESU. Kwa sababu sheria ya
ROHO wa uzima ule ulio katika KRISTO YESU imeniacha huru, mbali na sheria ya
dhambi na mauti. ‘’
Leo
tunazungumzia majina 7 ya heshima ya wateule wa MUNGU. Sio kwamba majina
haya tu saba ndio yapo kwa ajili ya waenda mbinguni bali kuna majina mengi tu.
Nimeandika majina saba kama tu yalivyoandikwa katika 1 Petro 2:9. Sio
kwamba wakristo wote ni wateule wa KRISTO bali wale tu waliokombolewa kwa damu
ya YESU na kuukulia wokovu kwa mafundisho katika makanisa sahihi ya kiroho.
1 Petro
2:9-10 ‘’ Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu
wa milki ya MUNGU, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani
mkaingie katika nuru yake ya ajabu; ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa
ni taifa la MUNGU; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema. ‘’
Kutokana na maandiko
hapo juu tunatambua kwamba Wateule wa MUNGU ni;
-Mzao mteule
-Makuhani wa
kifalme.
-Taifa
takatifu.
-Watu wa
milki ya MUNGU.
-Watangaza
fadhili za MUNGU.
-Tulioitwa
na MUNGU kutoka gizani na kwenda kwenye uzima wake.
-Tuko kwenye
nuru yake ya ajabu.
1. MZAO MTEULE.
Wateule wa
KRISTO wanaitwa mzao mteule kwa sababu wamezaliwa kiroho na MUNGU ‘’Yohana
1:13, waliozaliwa, si kwa damu,
wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa MUNGU.’’ Pia Biblia inaendelea kusema kwamba bila
kuzaliwa upya au kuzaliwa mara ya pili haiwezekani kuurithi ufalme wa MUNGU
Hivyo hawa kuitwa mzao mteule ni haki yao kabisa maana Yohana 3:5-6 Inasema ‘’
YESU akajibu, Amin, amin,
nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa ROHO, hawezi kuuingia ufalme wa
MUNGU. Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa ROHO ni roho.
‘’. MUNGU ametuita na kutukirimia vitu vyote
vipasavyo uzima na utauwa(1 Petro 1:3)
2. MAKUHANI WA KIFALME.
Wateule wa
MUNGU pia wanaitwa makuhani wa kifalme kwa sababu MUNGU mwenyewe anasema ‘’
nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu. Hayo ndiyo maneno
utakayowaambia wana wa Israeli. -Kutoka 19:6’’
Moja ya sifa
za kuhani wa JEHOVAH MUNGU wetu ni hizi;
-Uaminifu(1
Samweli 2:35)
-Wana sheria
ya MUNGU(Yeremia 18:18)
-Wamehifadhi
maarifa ya Kimungu(Malaki 2:7)
Hizo ni sifa
za makuhani na makuhani wa kifalme ambao ni wateule wa BWANA YESU wana sifa
hizo na zaidi, Pia ni makuhani wa
kifalme kwa sababu wamempokea MFALME wa wafalme yaani YESU KRISTO. Ufunuo 1:5-8
‘’ tena zitokazo kwa YESU KRISTO, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa
kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha
dhambi zetu katika damu yake, na kutufanya kuwa ufalme, na makuhani
kwa MUNGU, naye ni BABA yake; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele.
Amina. Tazama, yuaja na mawingu; na kila jicho litamwona, na hao waliomchoma;
na kabila zote za dunia wataomboleza kwa ajili yake. Naam. Amina. Mimi ni Alfa
na Omega, mwanzo na mwisho, asema BWANA MUNGU, aliyeko na aliyekuwako na
atakayekuja, Mwenyezi. ‘’
3. TAIFA TAKATIFU.
Wateule ni
taifa takatifu kwa sababu wanaishi maisha ya
utakatifu kama atakavyo MUNGU. Wakolosai
1:21-22 ‘’ Na ninyi, mliokuwa hapo
kwanza mmefarikishwa, tena adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya,
amewapatanisha sasa; katika mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake, ili awalete
ninyi mbele zake, watakatifu, wasio na mawaa wala lawama; ‘’
BWANA ni
mtakatifu na aliyeungwa roho moja na BWANA lazima tu naye awe mtakatifu, 1 Kor
6:17 ‘’ Lakini yeye aliyeungwa na BWANA ni roho moja naye. ‘’ Ni heshima kuu MUNGU Bamteupa sisi wateule
wake. Waefeso 2:20 -22 ‘’ Basi tangu
sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu,
watu wa nyumbani mwake MUNGU. Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii,
naye KRISTO YESU mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni. Katika yeye jengo lote linaungamanishwa
vema na kukua hata liwe hekalu takatifu katika BWANA. Katika yeye ninyi nanyi
mnajengwa pamoja kuwa maskani ya MUNGU katika ROHO. ‘’
4. WATU WA MILKI YA MUNGU.
Wateule ni
watu wa milki ya MUNGU kwa sababu Wanaliishi kusudi la MUNGU, Wameokoka Waefeso
2:8 ‘’ Kwa maana
mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu,
ni kipawa cha MUNGU.‘’ KRISTO ametuokoa na na yeye anamilki milele. Ufunuo
11:15 ‘’ Malaika wa saba akapiga baragumu, pakawa na sauti kuu katika mbingu,
zikisema, Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa BWANA wetu na wa KRISTO
wake, naye atamiliki hata milele na milele.
‘’
5. WATANGAZA FADHILI ZA MUNGU.
Wateule ni
muhimu sana kwa MUNGU maana wanatangaza fadhili za MUNGU hapa duniani Zaburi
103:17 ‘’ Bali fadhili
za BWANA zina wamchao Tangu milele hata milele, Na haki yake ina wana wa wana;
‘’ Watu wanamjua MUNGU wa kweli kupitia wateule wake. Zaburi 96:2-7 ‘’ Mwimbieni
BWANA, libarikini jina lake, Tangazeni wokovu wake siku kwa
siku. Wahubirini mataifa habari za utukufu wake, Na watu wote habari za
maajabu yake. Kwa kuwa BWANA ni mkuu mwenye kusifiwa sana. Na wa
kuhofiwa kuliko miungu yote. Maana miungu yote ya watu si kitu,
Lakini BWANA ndiye aliyezifanya mbingu. Heshima na adhama ziko mbele zake,
Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake. Mpeni BWANA, enyi jamaa za watu, Mpeni
BWANA utukufu na nguvu. ‘’. Tu wajumbe
kwa ajili ya KRISTO(2 Kor 5:20-21)
6. TULIOITWA NA MUNGU KUTOKA GIZANI NA KWENDA
KWENYE UZIMA WAKE.
MUNGU
mwenyewe ni nuru na anatutaka wateule wake tuwe nuruni siku zote 1 Yohana 1:5-7
‘’ Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kwake, na kuihubiri kwenu, ya kwamba MUNGU
ni nuru, wala giza lo lote hamna ndani yake. Tukisema ya kwamba
twashirikiana naye, tena tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatuifanyi
iliyo kweli; bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru,
twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake YESU, Mwana wake, yatusafisha dhambi
yote. ‘’ Pia Biblia inaendelea
kusema kwamba tumetoka gizani na sasa tuko nuruni kwenye uzima wa BWANA . 1
Yohana 3:13-14 ‘’ Ndugu zangu, msistaajabu, ulimwengu ukiwachukia. Sisi tunajua ya kuwa
tumepita toka mautini kuingia uzimani, kwa maana twawapenda ndugu. Yeye
asiyependa, akaa katika mauti. ‘’
7. TUKO KWENYE NURU YA AJABU.
Tuko kwenye
nuru ya BWANA YESU, Waefeso 5:8 ‘’ Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali
sasa mmekuwa nuru katika BWANA; enendeni kama watoto wa nuru, ‘’
YESU ni
nuru(Yohana 8:12) na ametufanya na sisi wateule wake kuwa Nuru ya ulimwengu.
Mathayo 5:14-16 ‘’ Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika
ukiwa juu ya mlima. Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu
ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani. Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele
ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze BABA yenu aliye mbinguni. ‘’
Naamini
umejifunza mambo mazuri sana kukuhusu wewe mteule mwenzangu wa KRISTO na pia
Yule ambaye bado hajampokea YESU kama BWANA na MWOKOZI wake siku ya kufanya
hivyo ndugu naomba uifanye iwe leo maana zamani hizi ni za maovu mengi. Mimi
mteule ‘’ Nimesulibiwa pamoja na KRISTO; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali
KRISTO yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika
imani ya Mwana wa MUNGU, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili
yangu. Wagalatia 2:20)
Kwa
sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku
nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio
kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na
utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi
kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko
KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
MUNGU Akubariki.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
MUNGU Akubariki.
Comments