MAOMBI YA KUICHAMBUA NA KUIANGUSHA SERIKALI YA UTAWALA WA KISHETANI KUANZIA NGAZI YA JUU HADI YA CHINI.:ASKOFU MKUU JOSEPHAT GWAJIMA

Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima, Ufufu na Uzima.

Shetani ambaye ndiye ibilisi amewakilishwa kwa majina tofauti kwenye Biblia na ibilisi ni neno la kiarabu limeandikwa kwenye Biblia mara 29, neno shetani nalo limeandikwa mara 51, huyuhuyu shetani mahala pengine ameandikwa mwovu na mkuu wa ulimwengu na ndiye anayefanya ulimwengu huu uonekane jinsi unavyooneka leo. Neno lucifes maana yake ni mtoa nuru, mtu anapotaka nuru ya siasa anamtafuta yeye, au umaarufu anamtafuta yeye, ulimwengu wa rohoni haupo mbali sana. 

SHUHUDA 9 ZINAZOONYESHA KWAMBA SHETANI ANAKAA DUNIANI. 

1. Ufunuo12: 12 Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu. Shetani yupo duniani kwamaana alitupwa kutoka mbinguni 

2. Ufunuo9: 1 Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu. 2 Akalifungua shimo la kuzimu; moshi ukapanda kutoka mle shimoni kama moshi wa tanuru kubwa; jua na anga vikatiwa giza kwa sababu ya ule moshi wa shimoni. Shimo la kuzimu lipo hapa duniani, nyota iliyoanguka ni malaika aliyeshuka kutoka mbinguni 11 Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu, jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kiyunani analo jina lake Apolioni. Shimo lilifunguliwa na malaika wa kuzimu alitoka humo ndani.

 3. Ayubu1: 7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo. Shetani aliwahi kuonekana duniani hapa hapa akizungukazunguka na yupo hata leo anazunguka na unatakiwa ujue shetani ana uwezo wa kuzunguka na kutembea duniani. Ayubu2:2

  4. Kumbukumbu la torati 34: 1 Musa akapanda kutoka uwanda wa Moabu mpaka mlima Nebo, hata kilele cha Pisga kukabili Yeriko. Bwana akamwonyesha nchi yote ya Gileadi hata Dani; 2 na Naftali yote, na nchi ya Efraimu na Manase, na nchi yote ya Yuda, mpaka bahari ya magharibi; 3 na Negebu, na uwanja wa bonde la Yeriko, mji wa mitende, hata mpaka Soari. 4 Bwana akamwambia, Hii ndiyo nchi niliyowaapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, nikisema, Nitawapa wazao wako. Basi nimekuonyesha kwa macho yako, lakini hutavuka huko. 5 Basi Musa, mtumishi wa Bwana, akafa huko, katika nchi ya Moabu, kwa neno la Bwana. 6 Akamzika bondeni, katika nchi ya Moabu, kukabili Beth-peori; lakini hapana mtu ajuaye kaburi lake hata leo. Kwenye agano jipya unashangaa yuda alisoma wapi kuhusu Mungu alipomzika Musa. shetani Aligombania mwili kwenye mazishi na yale matukio ambayo mtu anagombania mwili wa marehemu ujue kuna shetani mahali pale. Yuda1:9 

5. Zakaria3: 1 Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye. 2 Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni? Aliingia kwenye ibada wakati askofu mkuu Joshua anaongoza ibada 

6. 1Mambo ya nyakati21: 1 Tena shetani akasimama juu ya Israeli, akamshawishi Daudi kuwahesabu Israeli. Shetani aliongea na daudi hapa duniani, kwenye ulimwengu ulioendelea wanasema shetani ni mawazo lakini si hivyo yupo

 7. 1Yohana5: 19 Twajua ya kuwa sisi tu wa Mungu; na dunia yote pia hukaa katika yule mwovu. Dunia yote inakaa katika yule mwovu sio Tanzania yote ni dunia yote, unaweza kukutana na mtu anataka kukuchumbia kumbe ni shetani, mtu anataka kufanya na wewe bihashara kumbe ni shetani kabisa ndio maana anasema anazunguka zunguka huku na huko.

 8. 2wakorintho4: 3 Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; 4 ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu. Anaitwa mungu wa dunia hii utaona anadhibiti uchumi, siasa, ulinzi na anawafanya watu wawe waishi kwenye dhambi kwasababu ya maisha ya shida, anawapa watu umaarufu kwa kuwaharibu kwanza na kuwapatia umaarufu. Kazi yake ni kupofusha fikra unakuwa kipofu na huoni kabisa kwamba Yesu anaokoa, huoni kama mbele kuna maisha mazuri ukiwa ndani ya wokovu amepofusha fikra za watu. 

SEHEMU YA PILI UHAKIKA KWAMBA SHETANI ANA SERIKALI YAKE

 Shetani anaitwa mfalme na watu wengi hawajui kwa nini anaitwa mfalme; neno mfalme zamani lilikuwa linatumika kama mkuu wa nchi na ulimwengu wa kale wakuu wa kale wote walikuwa wanaitwa wafalme na shetani anatembelea kwenye mtiririko huo wa kifalme Yohana 12: 31 Sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo; sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje. 32 Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu. Anaserikali yake ndio maana anaitwa mkuu, mfano mkuu wa nchi ya Tanzania ni Jakaya kikwete ana wasaidizi wake mawaziri, wabunge na wengine wako chini yake, mkuu wa nchi ya marekani ni Barack Obama naye ana baraza lake mawaziri na wasaidizi walio chini yake, Ukiangalia shetani huyu baadaye huyu atatoka kuwa mkuu na kuitwa mpinga kristo na nabii wa uongo. Jina lingine anaitwa Lucifer kama mwanzilishi wa nuru ya dunia na unaona watu wanao mwendea kupata siasa, uchawi, hekima ya dunia wanaenda kupata nuru kwa shetani, na ndio maana Yesu alisema ‘mimi ndiye nuru ya ulimwengu’ inamaana kuwa Lucifer ni nuru feki ni mwongo amepofushafikra za watu na kuwafanya wamtumikie na kumwendea ili wapate mali na utajiri. Yohana 16: 11 kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa. Utaona majina yake ana majina mengi kama baba wa uongo shetani si mwanaume wala mwanamke hana jinsia na “Mungu naye hana jinsia japo tuna mwita Baba” na neno baba maana yake ni mwanzilishi au asili na mwanaume anaitwa Baba kwasababu ni mwanzilishi wa familia yaani asili. Na shetani anaitwa baba wa uongo maana yake ni mwanzilishi wa uongo au asili wa uongo. Yohana 8: 44 Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo. Yeye ni mwongo na baba wa huo uongo, shetani ni mkuu na mwanzilishi wa uongo na ana watoto chini yake kama vile Mungu anavyo zaa nayeye ana zaa pia shetani ndio asili ya magonjwa, mikosi, matatizo, dhambi, uovu, uonevu, uchafu na uharibifu wote unaoendelea duniani. 1Yohana 3: 9 Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu. 10 Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake. 

TUNATAKA TUFANYE MAPINDUZI DHIDI YA UTAWALA WA KISHETANI KWA JINA LA YESU.

 Serikali ya shetani imejengwa kijeshi zaidi kuanzia Lucifer mwenyewe ni mjeshi mpaka kale ka mwisho ni kajeshi, Ukiangalia ametoka mbinguni kwa vita, alipigana na wanajeshi wenzake malaika walioasi na hawa ni waasi wa kijeshi wametoka mbinguni walipigana mbinguni na mwisho wao waliondoka wakiwa wamekaa kivita zaidi. Efeso6: 12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. “serikali ya kishetani imekaa kijeshi zaidi” na ndio maana unaona majeshi ya pepo wabaya. Unatakiwa ujue tunapambana na falme baada ya shetani, mamlaka na kama unataka kumshinda shetani lazima uwe kijeshi zaidi kwasababu utawala wake umekaa kijeshi. Unaposema falme maana yake shetani na chini yake kuna falme zinazotenda kazi. Luka8: 28 Alipomwona Yesu alipiga kelele, akaanguka mbele yake, akasema kwa sauti kuu, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakusihi usinitese. 29 Kwa kuwa amemwamuru yule pepo mchafu amtoke mtu yule. Maana amepagawa naye mara nyingi, hata alilindwa kifungoni na kufungwa minyororo na pingu; akavikata vile vifungo, akakimbizwa jangwani kwa nguvu za yule pepo. 30 Yesu akamwuliza, Jina lako nani? Akasema, Jina langu ni Jeshi; kwa sababu pepo wengi wamemwingia. Yesu alimuuliza jina lake nani na mashetani yaliyokuwa ndani ya mtu yule yakamwambia unatakiwa ulize ni jeshi gani hili ndio maana yaka mwambia Jina langu ni jeshi. 

SERIKALI YA SHETANI IMEGAWANYIKA KWENYE SEHEMU KUBWA MBILI.

 1. Serikali ya shetani inayofanya kazi rohoni Hawa wanamwingia mtu ndani ya mwili wake na kumletea magonjwa, mikosi, balaa, na matatizo mengi kwenye maisha yake. 

2. Serikali ya kishetani kwenye ulimwengu wa mwili Hawa ni mashetani wanaovaa miili ya kibinadamu na wanaonekana kama wanadamu lakini roho zao ni mashetani asilimia mia moja na shetani hawezi kuzaa, lakini anajifanya mwanamke anakuwa na mahusihano na mwanaume na anazihifadhi hizo mbegu na anajigeuza tena anakuwa mwanaume na anakwenda kumtafuta mwanamke na anamwekea hizo mbegu na baadaye anazaliwa mototo wa kijini. Wengine wanafanyiwa hivyo kwenye ndoto na wanazaa watoto kabisa na ndio maana watoto wengi wanaozaliwa baba zaao wanakuwa sio wale halisi na tatizo hili sio uaminifu pekeyake bali hata na mashetani yahusika kufanya hivyo, ni serikali ya kishetani kwenye ulimwengu wa mwili ndiyo inatenda hayo ili kuujenga ufalme wa kishetani. Mathayo3: 7 Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? Yesu aliwaona hawa wazawa wanadamu kwamba ni majoka na sio binadamu kama wanavyo onekana kwa macho ya binadamu. Mathayo12: 34 Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake. Yesu anawashangaa kwanini wanaongea mazuri wakati asili yao ni mabaya ni mapepo, mashetani! Luka3: 7 Basi, aliwaambia makutano ya wale waliomwendea ili awabatize, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? 1Wakorinto15: 24 Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu. 25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake. 26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti. 27 Kwa kuwa, Alivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake. Lakini atakaposema, Vyote vimetiishwa, ni dhahiri ya kuwa yeye aliyemtiishia vitu vyote hayumo. 28 Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote. Yesu amepokea utawala kutoka kwa Baba yake mbinguni na amekuja hapa duniani na anataka abatilishe utawala wote wa giza na tawala zote za giza na ndipo Yesu atachukua kanisa. 

Utawala wa shetani una makao makuu sehemu tatu

 1. Ardhi 
2. Bahari 
3. Anga 

Kumbuka serikali ya kishetani imekaa kijeshi zaidi. Ndio maana ufunuuo 12 inasema ole wa nchi na bahari. Efeso2: 1 Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu; 2 ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi; Ni mkuu wa anga pia na ukiona hata kwenye majeshi duniani kuna jeshi la kwenye maji, nchi kavu wanatembea na kukimbiza, na kuna jeshi la anga. Mungu alipomuumba Adamu alimpa utawala wote wa angani ardhili na baharini. Mwanzo1: 26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. Unapokuwa unaomba unatakiwa ujue makao yake makuu ni yapi kwamba ni angani, ardhini, na baharini. Unaamua katika jina la Yesu ninafunga anga na jeshi lake la anga, mashujaa wake wa anga mizinga yake ya anga kwa jina la Yesu baadaye unafunga baharini na wakuu wake wote na majeshi yake yote na majini yake yote alafu unafunga na kwenye nchi na wachawi wake na waganga wake wote kwa jina la Yesu unapofunga makao makuu ya shetani katika nchi unawafunga na mashetani waliovaa miili na kufanya kazi pamoja na wanyama wote na ndege wote. Tunapomfunga shetani haimaanini tunammaliza bali tunamzuia asiweze kujibu mashambulizi na baadaye tunachukua vyote alivyovichukua na akija kuamka havipo na hawezi kuvichukua vyote. 

Mashetani wakuu wanaotawala dunia ni watatu. 
 Lucifer mwenyewe, beelzebuli mkuu wa mapepo anaonekana kama mtoto wa lucifa mwenyewe, “Ashtoreth” walijenga nguzo juu ya Ashtoreth. Kitabu cha shams kaburi kinaelezea hawa mapepo jinsi wanavyo tawala siku. Jumapili ni siku ya jua na mamlaka nyingi zikitaka kufanya chochote cha kimamlaka hufanya siku ya jumapili ili jambo hilo lifanikiwe, mfano uchaguzi unafanywa siku ya jumapili, pia kuna mashetani yanayofanya kazi siku ya juma pili kuleta aibu maana yake mtu akikuloga anakuloga uwe na aibu anafanya siku ya jumapili, pia huitumia siku ya juma pili kupanga mahesabu ili mambo yao yaende sawa sawa, pia mashetani haya hupanga majeshi ya kishetani ili kushambulia siku zinazofuata kwenye maisha ya watu na kuleta matatizo, wachawi hukaa siku ya jumapili kupanga mipango yao, kuna mashetani yanayofanya vikao vyao vya uharibifu. Pia kuna mashetani yanafanya ahadi zao za kishetani mfano kushambulia kwa mtu kiroho au kimwili mipango yake hupangwa saa moja kamili asubuhi, Saa mbili asubuhi ni wakati mzuri wa mwanamke au mwanamke kudanganywa, Saa tatu; kama mtu una cheo na una mipango yako ya bihashara wanaweza kuja kukunyemelea na kukusikiliza, Saa nne: saa nzuri ya mauzo, saa mbaya sana kwa wale wanao tamkiwa maneno mabaya maana laana hutenda kazi vizuri, saa hii maana yake mtu akikutamkia utakufa basi utakufa kweli maana mashetani huyabeba maneno na kuyatendea kazi kikamilifu, ukifunga ndoa saa hii haita simama, usitajetaje jina la mtu vibaya maana maisha yake yote yatakuwa vile vile mfano ukimtamkia mtu ukichaa mkubwa basi mashetani yanachukua maneno hayo na kuyatendea kazi, Saa sita ni saa nzuri ya nzuri ya mauzo, na ni saa nzuri ya kumtapeli mtu mwenye akili, Saa saba kamili kwa wachawi kama wamemtisha mtu ukikutana naye anakuwa ni jasiri, Saa nane wakiongea na mtoto aliye tumboni, mtoto atasikia vizuri na hapa ndipo mtoto analogewa wanakuja wanamnongoneza mtoto ajinyonge, azunguke, atangulize mguu kichawi ili mimba iharibike. Saa tisa ni saa nzuri ya kufunga ndoa ya kishetani mfano umejilaza unaota mtu anakuvisha pete, Saa kumi ni siku kuu ya kishetani, Saa kumi na moja ni siku ya kumpa mtu mnyonge zawadi iliyonuiziwa mabaya au ugonjwa, kumi na mbili chochote kinachuhusu mti kikifanyika mda ule wao wachawi wanaamini ni sawa na mafanikio.

 Huyu shetani anayeimiliki jumapili akiamua awe mtu atakutokea kama kofia yenye dhahabu aliyepanda simba au amevaa koti jekundu, au akiamua kujitokezaa atajifanya jogoo mnene mwenye shingo ndefu na miguu yake mifupi, anaweza kujitokeza kama kijana mwenye mavazi ya kifalme, anaweza kuwa mrembo amevikwa kimalkia na hii hutokea kwenye ndoto, anaweza kutokea kwenye ndoto kama dume la simba ambaye kwato zake zinaonekana zinadamu, ndege mkubwa mwenye manyoya anarangi nzuri zinazopendeza na anaweza kutokea kama ukiwa ndotoni hivyo hutakiwi kuogopa unatakiwa ushambuliee kwa jina la Yesu. 

Mimi ni rungu la Bwana nitavunja vunja mwanamke na mwanaume maana yake shetani akijigeuza mwanamke unamponda akijigeuza mwanaume unamponda pia, mfano nitavunja vunja gari la vita na aliyemo ndani yake maana yake kuna mashetani yanyojigeuza maumbo na hayana nguvu juu yetu kwa jina la Yesu. Kwa jina la Yesu naimiliki siku ya jumapili na masaa yake yote kwenye maisha yangu yote kwa jina la Yesu natawala masaa yote ya jumapili zote za maisha yangu kwa jina la Yesu, nakutangazia ewe shetani unayetawala jumapili naiteka kalenda yako ya utawala wa jumapili kwa jina la Yesu, mwaka huu kila pepo atakaye nitokea kwenye kisima cha maji, baharini, ziwani, mtoni nakushambulia kwa jina la Yesu. Ninaliteka anga nalifunga kwajina la Yesu, naiteka bahari naifunga kwa jina la Yesu na mashujaa wako, na wanajeshi wako na askari wako ninawafunga kwa jina la Yesu nakuteka nchi na mapepo yako na mashujaa wako kwa jina la Yesu ninateka mashetani ya angani, ardhini, na baharini ninayafunga kwa jina la Yesu, watawala wa nchi ninawaponda kwa jina la Yesu mnaotawala kwa miili ya kibinadamu ninawaponda kwa jina la Yesu kwa mamlaka ya jina la Yesu kristo, ninafnya vita katika ulimwengu wa rohoni na mashetani wote mnaofanya vita na maisha yangu siku ya juma pili ninawateketeza kwa jina Yesu, mashetani mnaosimamia utapeli, laana, mikosi ninawateka wote nawateketeza kwa jina la Yesu. Silaha kubwa yakum shinda shetanii ni kumfahamu vizuri na hapendi umfahamu vizuri lakini akijua hilo atakuacha mara moja kukufuatilia. 

Kabla ya waaraabu hawakuwepo na majini hayakuwepo shetani alikuwepo na kuna mashetani kama haya ambayo ni wasaidizi wake

 wa kwanza ni “rucifuge rofokale” huyu anamamlaka yote ya kudhibiti mali zote na utajiri na ndiye anadhibiti mali na hazina zote za hapa duniani na ndiye anaruhusu mtu awe na mali au asiwe nayo na anaishi ndani ya mtu na ndiye mkuu wa utawala unaweza kumgooglekwenye mtandao ukamwona. 

Wapili ni “Santachia” huyu anamamlaka juu ya wanawake na wasichana wote ambao hawajaokoka anauwezo wa kuwafanyia lolote au wale wanaorudi nyuma anaweza kuwafanyia wafanye lolote ama wawe machangudoa au wawe na viburi unaweza kumgoogle na ukamfahamu ili ujue unapambana na nini na upige hapo na kumsambaratisha kwa jina la Yesu. Ni mkuu wa utawala au amri jeshi mkuu wa ufalme wa kishetani. 

Wa tatu anaitwa “agaliarept” anamamlaka na uwezo wa kugundua siri zote za mabaraza na anaamuru kikosi cha majini maelfu kwa maelfu ni shetani orijino si jinni na kazi yake ni kugundua siri na ni idara ya upelelezi ya kishetani ndio kamanda wa jeshi la kishetani anauwezo wa kuona huyu ana nyota au atakuwa kiongozi, na watu wanamwendea huyo ili kujua raisi ajaye na mambo mengine. 

Wa nne ni “fleurety” ana mamlaka na nguvu za kufanya kazi yeyote usiku na kusababisha mvua yam awe na mafuriko katika sehemu yeyote inayohitajika na majeshi ya kwenye maji huyu ni kamanda wa mafuriko. Shetani anapohitaji mahali Fulani pawe na tsunami anahusika huyu 

Wa tano “sargatanas” ana nguvu na mamlaka ya kumfanya mtu yeyote asionekane na huyu ndiye anayeshughulika kumfanya mtu achukuliwe msukule na ukimpiga huyu unawaona wachawi. Ni shetani anayewasafirisha watu waende sehemu yeyote ile wakiwa hawaonekani, pia hufungua koki au kufuli au kitasa cha aina yeyote ile duniani, huonyesha na kuweka wazi mambo yote yanayoendelea ndani ya nyumba za watu mfano maongezi n.k, hudhibit na kuamuru mashetani yasio pungua elfu tano 

sita ni “nebiros” huyu anauwezo wa kushurtisha mto yeyote amtakaye afanye uovu mfano hutaki kufanya uzinzi, kusema uongo lakini huyu anakuongoza ufanye hayo yote, pia anawapa watu ufahari japo mtu anaonekana ni wa maana lakini sio wa maana, ndiye mkuu wa utabiri wa mambo yanayotokea baadaye, kuzunguka huko na huko kila sehemu kwaajili ya kuangalia maasi, huyu ni inspekta generali wa kukamata, na hapa kuna roho ambazo zinaleta tuhuma. Hawa wote ni mashetani ambao wapo kabisa duniani wanatenda kazi kila siku na tukiwa tunafanya mapinduzi ya kidunia lazima hawa wote wapigwe na ufalme wa kishetani uondolewe ili ufalme wa mwanakondoo ujengwe duniani kote kwa jina la Yesu kristo. 

Hawa sita wana wasaidizi wao 17 ambao hufanya kazi kama mawaziri

 1. Clauneck kazi zake ni;- nguvu na mamlaka juu ya vitu vyote na utajiri, anauwezo wa kuvumbua hazina iliyofichwa kwa yeyote atakayeweka mkataba naye, ana uwezo wa kumzawadia mtu utajiri mkubwa sababu anapendwa na Lucifer sababu ya mikataba yake, anauwezo wa kukuletea pesa kutoka mbali 

2. Musisin; ana nguvu juu ya mabwana wa kuu wa kishetani kuwapa maelekezo juu ya mambo Fulani. 

3. Becharn ; ana nguvu juu ya upepo, tufani, radi, umeme, mvua, uchawi wa chura na vitu vingine vya namna hiyo kama misri mfalme farao alipofanya uchawi wa chura 

4. Frimstost; ana uwezo wa kumsaidia mwaanamke kumpa furaha yenye kuishia kwenye maangamizi ana mashetani mengi chini yake. 
5. Khil; huyu husababidha matetemeko ya ardhi. 
6. Mersilde; ana uwezo wa kukusafirisha mara moja sehemu yeyote utakayo 
7. Clistheret; ana uwezo wa kukugeuzia usiku kuwa mchana malaika wa nuru. 
8. Sirchad; ana uwezo wa kukuonyesha aina zote zile za wanyama katika umbo lolote lile walilo nalo. 
9. Sigal ana uwezo wa kukuonyesha dhahiri miujiza ya kichawi na ndiye mkuu wa mazingaumbwe yote. 
10. Hiepatch; ana uwezo wa kukuletea mtu aliye mbali papo kwa hapo, wachawi humtumia huyu. 
11. Humots; ana uwezo wa kusafirisha aina zote za vitabu kwa starehee yake. 
12. Fruciesseiere; ana uwezo wa kufanya miujiza mikubwa ya kuwafanya waliopotea wakapatikana. 
13. Grand; ana uwezo wa kusabaabisha aina zote za maradhi
 14. Surgat; ana uwezo wa kufungua aina zote za lock. 
15. Morail; ana uwezo wa kutengeneza dunia isiyo onekana ‘kufanya vitu vyote visionekane’ huyu ndiye kuzimu mwenyewe. 
16. Frutimiere; ana uwezo wa kukupa kila aina ya starehe utakayoilipia kifo.
 17. Huictiigar; ana uwezo wa kukusababisha kutembea ukiwa usingizini na wengine kuwakosesha usingizi kabisa. Shambulia hawa mawaziri wa kipepo wanaotawala kwenye maisha yetu kwa jina la Yesu kristo. 

Tutaendelea kesho kuzichambua na kuzisambaratisha tawala zote za shetani na majeshi yake na wakuu wake wote kwa jina la Yesu.

Comments