![]() |
| Na Mtumishi Alex Simion Makuli |
Katika maisha yetu hapa duniani tunaishi lakini kwa upande mwingine tukumbuke kwamba lipo tumaini jipya ndani ya KRISTO YESU, YESU KRISTO anahitaji sana mioyo yetu kuliko kitu kingine chocho, hataki hata mmoja wetu apotee bali kila mmoja afikilie toba. Niongee na wewe ambaye siku zote umeisikia sauti ya Bwana ikikusihi "KUOKOKA" halafu ukaufanya moyo wako kuwa Mugumu, bado Nafasi ipo, na YESU bado anakupenda hataki uangamie ktk Jehanamu, bado lipo tumaini jipya, Kumbuka kuokoka ni leo wala sio kesho, "Na utakapoisikia sauti ya BWANA leo usifanye moyo wako kuwa Mugumu". BIBLIA inasema "Ufunuo 3:20" TAZAMA NASIMAMA MLANGONI, NABISHA, MTU AKISIKIA SAUTI YANGU, NA KUFUNGUA MLANGO NITAINGIA KWAKE, NAMI NITAKUWA PAMOJA NAYE, NA YEYE PAMOJA NAMI. YESU KRISTO yupo mlangoni kwako leo mkubari ili aingie kwako, Na kama hujampokea YESU kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako ndio wakati sasa wa kumpokea
Hakuna furaha kubwa kama kumwamini YESU KRISTO ktk maisha yako,
ikimwamini YESU anakuwa kiumbe kipya(2KOR 5:17), hajalishi umetenda uovu
kiasi gani lakini YESU akiingia ndani yako anabadilisha historia ya
maisha yako na kukupa uzima. Ukimwamini YESU na kumpokea moyoni mwako
hapo ndipo unapata nafasi ya kufanyika mtoto wa MUNGU(Yoh 1:12).
Nashangaa sana nyakati hizi tulizonazo watu
wanakataa "WOKOVU" eti kwa sababu wanazo dini zao ua madhehebu yao,
YESU ni wa mhimu sana kuliko dhehebu lako. Lakin ja ajabu watu wako
gizani pamoja na dini zao, Ukija kwa YESU unakuwa nuruni, BIBLIA inasema
"YOH 12:46 MIMI NIMEKUJA ILI NIWE NURU YA ULIMWENGU, ILI KILA MTU
ANIAMINIYE MIMI ASIKAE GIZANI". Unaweza kuwa na dhehebu lako zuri lakin
ukawa gizani, lakin ukija kwa YESU unakuwa nuruni na kupata uzima wa
mileleMtu mmoja anapomwamini YESU kunakuwa na furaha mbinguni kwa ajiri ya mtu huyo ambaye amempa YESU maisha yake. "LUKA 15:7 NAWAMBIA HIVYO HIVYO KUTAKUWA NA FURAHA MBINGUNI KWA AJILI YA MWENYE DHAMBI MMOJA ATUBUYE, KULIKO KWA AJILI YA WENYE DHAMBI TISINI NA KENDA AMBAO HAWA HAJA YA KUTUBU". Kwa hiyo unaweza kuona ni kwa jinsi gani roho ya mtu ilivyo ya thamani mbele za MUNGU.
FAIDA ZA KUMPOKEA/KUMWAMINI YESU
(1)Unahamishwa kutoka ktk ufalme wa giza na kuingizwa ktk MUNGU[KOL 1:13].
(2)Unasamehewa dhambi[LUKA 7:48-49, KOL 1:14].
(3)Unafanyika mtoto wa MUNGU[YOH 1:12].
(4)Unapata haki[WARUMI 5:9]. (5)Unapata nguvu ya MUNGU[1KOR 1:18].
(6)Unakuwa kiumbe kipya[2KOR 5:17].
MUNGU wetu anatupenda sana hataki hata mmoja wetu apotee bali kila mmoja afikirie toba. Mpokee YESU leo upate uzima wa milele.
Hakuna kitu kibaya kama kumkataa YESU, Maana ukimkataa YESU umeikataa
mbingu/umekataa uzima wa milele. BIBLIA inasema "1YOH 5:11-12 NA HUU
NDIO USHUHUDA, YA KWAMBA MUNGU ALITUPA UZIMA WA MILELE, NA UZIMA HUO UMO
KATIKA MWANAE, YEYE ALIYENAYE MWANA ANAO HUO UZIMA, ASIYENAYE MWANA WA
MUNGU HANA HUO UZIMA". Kama kweli unataka kuingia ktk uzima wa milele
aliko KRISTO YESU lazima umwamini YESU
na umruhusu aingia ndani yako. Lakini kama ukimkataa YESU kuna hukumu,
YOH 3:18 Biblia inasema "AMWAMINIYE YEYE HAHUKUMIWI, ASIYEMWAMINI
AMEKWISHA KUHUKUMIWA KWA SABABU HAKULIAMINI JINA LA MWANA PEKEE WA
MUNGU, NA HII NDIYO HUKUMU YA KUWA NURU IMEKUJA ULIMWENGUNI NA WATU
WAKAPENDA GIZA KULIKO NURU KWA MAANA MATENDO YAO YALIKUWA MAOVU". Kwa
hiyo ukisikia sauti ya YESU halafu ukaikataa Biblia inasema "UMEKWISHA
HUKUMIWA" Sio "UTAHUKUMIWA",
Unapomruhusu YESU ili aingie ndani ya moyo wako hapo ndipo jina lako
huandikwa ktk kitabu cha uzima. Na wale wote ambao majina yao
yameandikwa ktk kitabu cha uzima cha Mwanakoodoo ndio wenye haki ya
kurithi uzima wa milele wakiwa na KRISTO YESU. UFUNUO 21:27 Biblia
inasema "NA NDANI YAKE HAKITAINGIA KAMWE CHOCHOTE KILICHO KINYONGE, WALA
YEYE AFANYAYE MACHUKIZO NA UONGO, BALI WALE WALIONDIKWA KATIKA
KITABU CHA UZIMA CHA MWANA-KONDOO". Kwa upande mwingine inawezekana
kweli tumempokea YESU, lakini tunapaswa KUTUBU pamoja na KUISHI MAISHA
MATAKATIFU ili siku ile ya mwisho tusije tukawa watu wa kukataliwa.
"1YOH 1:8-9 TUKISEMA KWAMBA HATUNA DHAMBI TWAJIDANGANYA WENYEWE WALA
KWELI HAIMO MWETU. TUKIZIUNGAMA DHAMBI ZETU, YEYE NI MWAMINIFU WA HAKI
HATA ATUONDOLEE DHAMBI ZETU NA KUTUSAFISHB NA UDHALIMU WOTE". MUNGU
atusaidie sana ili tuweze kufikia ile ahadi ya uzima wa milele. "YESU
ANAOKOA", Barikiwa sana!.
By Alex Simion Makuli

Comments