![]() |
Na Mtumishi Alex Simion Makuli |
Katika maisha yetu hapa duniani tunaishi lakini kwa upande mwingine tukumbuke kwamba lipo tumaini jipya ndani ya KRISTO YESU, YESU KRISTO anahitaji sana mioyo yetu kuliko kitu kingine chocho, hataki hata mmoja wetu apotee bali kila mmoja afikilie toba. Niongee na wewe ambaye siku zote umeisikia sauti ya Bwana ikikusihi "KUOKOKA" halafu ukaufanya moyo wako kuwa Mugumu, bado Nafasi ipo, na YESU bado anakupenda hataki uangamie ktk Jehanamu, bado lipo tumaini jipya, Kumbuka kuokoka ni leo wala sio kesho, "Na utakapoisikia sauti ya BWANA leo usifanye moyo wako kuwa Mugumu". BIBLIA inasema "Ufunuo 3:20" TAZAMA NASIMAMA MLANGONI, NABISHA, MTU AKISIKIA SAUTI YANGU, NA KUFUNGUA MLANGO NITAINGIA KWAKE, NAMI NITAKUWA PAMOJA NAYE, NA YEYE PAMOJA NAMI. YESU KRISTO yupo mlangoni kwako leo mkubari ili aingie kwako, Na kama hujampokea YESU kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako ndio wakati sasa wa kumpokea

Mtu mmoja anapomwamini YESU kunakuwa na furaha mbinguni kwa ajiri ya mtu huyo ambaye amempa YESU maisha yake. "LUKA 15:7 NAWAMBIA HIVYO HIVYO KUTAKUWA NA FURAHA MBINGUNI KWA AJILI YA MWENYE DHAMBI MMOJA ATUBUYE, KULIKO KWA AJILI YA WENYE DHAMBI TISINI NA KENDA AMBAO HAWA HAJA YA KUTUBU". Kwa hiyo unaweza kuona ni kwa jinsi gani roho ya mtu ilivyo ya thamani mbele za MUNGU.
FAIDA ZA KUMPOKEA/KUMWAMINI YESU
(1)Unahamishwa kutoka ktk ufalme wa giza na kuingizwa ktk MUNGU[KOL 1:13].
(2)Unasamehewa dhambi[LUKA 7:48-49, KOL 1:14].
(3)Unafanyika mtoto wa MUNGU[YOH 1:12].
(4)Unapata haki[WARUMI 5:9]. (5)Unapata nguvu ya MUNGU[1KOR 1:18].
(6)Unakuwa kiumbe kipya[2KOR 5:17].
MUNGU wetu anatupenda sana hataki hata mmoja wetu apotee bali kila mmoja afikirie toba. Mpokee YESU leo upate uzima wa milele.


Barikiwa sana!.
By Alex Simion Makuli
Comments