UDONGO ULIOHUISHWA

Na RP Adriano Makazi , Ufufuo na uzima Morogoro.

Utangulizi: Somo la leo linaitwa Udongo Uliohuishwa”. Kuhuishwa ni kufanywa hai tena. Ni kufufuliwa kwa kilichokufa. UDONGO uliohuishwa ni habari zinahusu ‘mwili’ kwa sababu miili yetu  imetokea katika ardhi, na ndiyo maana shetani ana uwezo wa kucheza na miili yetu kwa sababu anakuwa anacheza na ardhi.
WARUMI 4:17…[(kama ilivyoandikwa, Nimekuweka kuwa baba wa mataifa mengi); mbele zake yeye aliyemwamini, yaani Mungu, mwenye kuwahuisha wafu, ayatajaye yale yasiyokuwako kana kwamba yamekuwako.]… Mungu ndiye anayeshuisha.
WARUMI 8: …[ Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu.]…
1 KORINTHO 15:45…[Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha.]…
2 KORINTHO 3:6…[Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha.]…
EFESO 2:5…[hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.]…
FILIPI 4:10….[Nalifurahi sana katika Bwana, kwa kuwa sasa mwisho mmehuisha tena fikira zenu kwa ajili yangu, kama vile mlivyokuwa mkinifikiri hali yangu lakini hamkupata nafasi.]….
MWANZO 3:17…[Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako;]… Kama ardhi imelaaniwa kwa ajili  ya mtu aliyetoka katika hiyo ardhi.
MWANZO 3:19…[ kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.]….
1 KORITNHO 15:47….[Mtu wa kwanza atoka katika nchi, ni wa udongo. Mtu wa pili atoka mbinguni.]…..
MWANZO 2:7….[Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.]…
USHAHIDI WA KIBIBLIA KUWA ‘MTU  NI UDONGO’


MWANZO 2:7...[Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai]…
MWANZO 3:19….[kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.]…. Shetani  anajua asili ya ‘mwili’ na akitaka kukutesa,  anashika hayo mavumbi. Kwa hiyo ni rahisi sana mashetani kuharibu mwili wa mtu kwa kuwa ni udongo tu.


ISAYA 64:8…[Lakini sasa, Ee Bwana, wewe u baba yetu; sisi tu udongo, nawe u mfinyanzi wetu; sisi sote tu kazi ya mikono yako.]…


YEREMIA 18:6….[Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile kama mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema Bwana. Angalieni, kama udongo ulivyo katika mkono wa mfinyanzi, ndivyo mlivyo ninyi katika mkono wangu, Ee nyumba ya Israeli.]… Udongo ukiwa mikononi  mwa mfinayanzi,  anawezza kuufanya chochote. Ndiyo maana tabia za mtu zaweza kubadilika ghafla na kuwa kitu tofauti. Shertani wanaweza kufinyanga na hicho kitu kikaonekana lakini siyo cha halisi (magonjwa,  tabia za uzinzi n.k).
AYUBU 33:6…[Tazama, mimi ni mbele ya Mungu kama ulivyo wewe;  Mimi nami nilifinyangwa katika udongo.]…
ZABURI 10:18…[Ili kumhukumu yatima naye aliyeonewa, Binadamu aliye udongo asizidi kudhulumu.]…..
ZABURI 146:4….[Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, Siku hiyo mawazo yake yapotea.]….
ZABURI 90:3….[Wamrudisha mtu mavumbini, usemapo, Rudini, enyi wanadamu.]….
Hii ndiyo maana mtu anapokufa, watu husema ‘huu ni mwili wa fulani aliyefariki dunia’. Watu husema hivyo  kwa sababu mwili asili yake ni duniani. Mungu hakumuumba mwanadamu ili baadae afe, bali dhambi ilipoingia duniani, ardhi ililaaniwa kwa ajili ya Adamu.



UKIRI
Leo naiondoa laana katika ardhi ambayo katika hiyo ardhi mimi nilitwaliwa, Kwa  Jina la Yesu. Amen
 


MWANZO 1:24…[Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo]…. Ardhi inaweza kutoa vitu. Ardhi inapokuwa imelaaniwa maana yake imezuiliwa isitoe hivyo vitu. Ndiyo maana hata wewe unapotaka kufanya mambo makuu, ikiwemo kuondoa mapepo, mwili unakuwa mgumu sana kukuruhusu. Hii ni kwa sababu unakuwa umezuiliwa, kwa sababu ya hiyo laana. Wakati mwingine unataka kufanya mambo, ikiwemo kusaidia wengine lakini unajikuta unashindwa kufanya hivyo. Ndiyo maana yamkini unaonekana haufai, au hauna sifa, ni kwa sababu ya laana katika udongo ambao katika huo ulitwalliwa. Leo  tunamfuata Mfalme wa Wafalme aliyeufanya udongo ili atubariki tena kwa Jina la Yesu.
Laana ikiwepo mahali hakuna kitakachoota. YEREMIA 17:5….[ 5 Bwana asema hivi,  Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana. 6 Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.]….Laana inafanya nchi isikaliwe na watu.
2 SAMWELI 1:13-21…[Naye Daudi akamwambia yule kijana aliyempa habari, Watoka wapi wewe? Akajibu, Mimi ni mwana wa mgeni, Mwamaleki. 14 Daudi akamwambia, Jinsi gani hukuogopa kuunyosha mkono wako umwangamize masihi a wa Bwana? 15 Ndipo Daudi akamwita mmoja wa vijana, akamwambia, Mwendee, ukamwangukie. Basi akampiga hata akafa. 16 Daudi akamwambia, Damu yako na iwe juu ya kichwa chako mwenyewe; maana umejishuhudia nafsi yako ukisema, Nimemwua masihi a wa Bwana. 17 Basi Daudi akamwomboleza Sauli, na Yonathani, mwanawe, maombolezo haya; 18(kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Yashari), akasema,  Wana wa Yuda na wafundishwe haya, 19 Walio fahari yako, Ee Israeli  Juu ya mahali pako palipoinuka wameuawa;  Jinsi mashujaa walivyoanguka! 20 Msiyahubiri mambo haya katika Gathi, Msiyatangaze katika njia za Ashkeloni;  Wasije wakashangilia binti za Wafilisti,  Binti za wasiotahiriwa wakasimanga. 21 Enyi milima ya Gilboa, visiwepo juu yenu Umande wala mvua, wala mashamba ya matoleo;  Maana ndipo ilipotupwa kwa aibu ngao ya shujaa, Ngao yake Sauli, pasipo kutiwa mafuta.]… Laana hii ya Daudi kwa mlima huu wa Gilboa, umefanya ene hilo kuwa jangwa hadi hivi leo.


UKIRI
Mashetani wote manaoshikilia mwili wangu kwa sababu ya laana iliyotamkwa katika nchi, leo nawasambaratisha kwa Jina la Yesu. Amen
 


MWANZO  4:11-12….[Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; 12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani]…. Kilicholaaniwa hakiwezi kukupa mambo mema. Na linguine ni kuwa,  laana kwenye ardhi inaweza kumfanya mtu kuwa mtoro,  na hata kama baada ya kufanya kazi katia ardhi, matatizo hujitokeza na mshahara ule upeperushwe na upepo. Wapo watu ambao huhama hama, na kutotulia eneo moja. Hata makanisani, wapo ambao hawakai mahali pamoja, leo kanisa hili na kesho kanisa lile. Matokeo yake, mahali pale ambapo Mungu amepachagua ili ukutane na Baraka zako unapakosa.
Majeshi ya Bwana ya Bonde la Maono Morogoro wakifuatilia maandiko ya somo la "Udongo Uliohuishwa" na kumshangilia Bwana hapo tarehe 18/1/2015.


Msubiri  Bwana kwa sababu muujiza wako  upo. Kwa wanaotafuta ‘wachumba’, hapa Ufufuo na Uzima ni kisima cha Yakobo, ambapo wachumba hupatikana kwa Jina la Yesu.
UKIRI
Ewe laana kwenye ardhi uliyenisababishia nisiwe na makao duniani, leo nakuvunja kwa Jina la Yesu. Leo natoka mavumbini kwa Jina la Yesu. Enyi mavumbi mniachie kwa Jina la Yesu, kwa maana mimi ni udongo lakini uliohuishwa kwa Jina la Yesu. Naitegua mitego yote iliyotegwa mavumbini kwa Jina la Yesu. Amen.
 


Udongo uliolaaniwa,utaushangaa sana kuziona zile adhabu alizozitoa Mungu kwa Adamu,  Eva na kwa Nyoka. MWANZO 3:13-14…[Bwana Mungu akamwambia mwanamke, Nini hili ulilolifanya? Mwanamke akasema, Nyoka alinidanganya, nikala. 14 Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako;]…  Mungu anamwambia shetani kuwa mavumbi ni chakula cha shetani. Maana yake, mtu aliyetoka katika mavumbi ya ardhi ni chakula cha shetani. Je, kuna kupona? Yesu alipokuja duniani,  alivaa mwili kama tulivyo sisi,  na akashambuliwa katika mwili. Alipofufuka alikuwa na mwili,  lakini mtu wa kwanza aliyemtokea ni Mariamu, aliyemwabia ‘usiniguse’  kwa sababu aliyefufuka haguswi guswi ovyo. Maaniko yanasema, tulikufa pamoja na Kristo, tukafufuka pamoja naye….. kwa maana hiyo,  mwili wa mtu aliyeokoka  na kufufuka pamoja Kristo, hawezi kuguswaguswa na shetani, wala magonjwa yake. Wengine wataugua lakini siyo sisi tulio ndani ya Kristo, kwa maana sisi siyo tena chakula cha shetani.
UKIRI
Kwa Jina la Yesu, nilikufa pamoja na Kristo, nikaa kaburini siku zote tatu pamoja na Kristo, nikafufuka pamoja na Kristo siku ile ya tatu. Ndoa yangu imefufuka pamoja na Kristo. Kazi yangu imefufuka pamoja na Kristo. Mimi na Watoto wangu tumetoka mautini na kuingia uzimani kwa Jina la Yesu.   Amen.
 


HESABU 22:1-6…[ Kisha wana wa Israeli wakasafiri na kupanga katika nchi tambarare za Moabu ng'ambo ya pili ya Yordani karibu ya Yeriko. 2 Na Balaki mwana wa Sipori akaona mambo yote ambayo Israeli wamewatendea Waamori. 3 Moabu akawaogopa hao watu sana, kwa kuwa walikuwa wengi; Moabu akafadhaika kwa sababu ya wana wa Israeli. 4 Moabu akawaambia wazee wa Midiani, Sasa jeshi hili la watu litaramba vitu vyote vinavyotuzunguka,   kama vile ng'ombe arambavyo majani ya mashamba. Na Balaki, mwana wa Sipori, alikuwa mfalme wa Moabu zamani zile. 5 Basi Balaki akatuma wajumbe kwa Balaamu mwana wa Beori, hata Pethori, ulio kando ya Mto, mpaka nchi ya wana wa watu wake,  kwenda kumwita, akisema, Tazama, kuna watu waliotoka Misri; tazama, wanaufunika uso wa nchi, tena wanakaa kunikabili mimi. 6 Basi, njoo wewe, nakusihi unilaanie watu hawa; maana wana nguvu kunishinda mimi. Labda nitawaweza, tupate kuwapiga, niwafukuze watoke katika nchi yangu, kwa maana najua ya kuwa yeye umbarikiye hubarikiwa, na yeye umlaaniye hulaaniwa.]…. Laana inapokuwepo ni rahisi mno  kushindwa. Mfalme Balaki hakuwa mchawi, bali alimwendea mchawi (Balaam) ili tengeneze laana kwako. Mtu  aliyebarikiwa hawezi kulaaniwa. Mtu akeshalaaniwani rahisi kwa shetani kufanya  jambo lolote kwa mtu huyo.
KUTOKA 1:8-11…[Basi akainuka mfalme mpya kutawala Misri, asiyemjua Yusufu. 9 Akawaambia watu wake, Angalieni, watu wa wana wa Israeli ni wengi tena wana nguvu kuliko sisi. 10 Haya! Na tuwatendee kwa akili, wasije wakaongezeka; tena, ikitokea vita, wao nao wasije wakashikamana na adui zetu na kupigana nasi, na kutoka katika nchi hii.]….. Hata kama atakuja mfalme mpya asiyemjua Yusufu, bado Baraka zako zipo pale pale. Lakini kwa kadiri watakavyonitesa, ndivyo ambavyo nitakavyozidi kuongezeka kwa Jina la Yesu.
YOHANA 3:6…[Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho..]… Mwili huzaa mwili na roho huzaa roho.
YOHANA 6:63…[Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima.]…

YAKOBO 2:26…[Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa.]….
Ibilisi anaweza kupanda kwenye udongochochote atakacho. MATHAYO  13:36-39…[Kisha Yesu akawaaga makutano, akaingia nyumbani; wanafunzi wake wakamwendea, wakasema, Tufafanulie mfano wa magugu ya kondeni. 37 Akajibu, akasema, Azipandaye zile mbegu njema ni Mwana wa Adamu; 38 lile konde ni ulimwengu; zile mbegu njema ni wana wa ufalme; na yale magugu ni wana wa yule mwovu; 39 yule adui aliyeyapanda ni Ibilisi; mavuno ni mwisho wa dunia; na wale wavunao ni malaika.]…Ndiyo maana Yesu alitupa mamlaka ya kung’oa kila pando asilopanda Baba wa mbinguni.
UKIRI
Enyi wachawi na waganga mlionipandia balaa, magonjwa mlionipandia, leo nayango’a yote kwa Jina la Yesu. Ewe mtawala wa dunia, Lusifa na mashetani wako,  nakushambulia kwa Jina la Yesu.Amen
 
Laana huruhusu mlango wa shetani (adui) kuingia na kukushambulia.
2 SAMWELI 21:1-6...[Kulikuwa na njaa siku za Daudi muda wa miaka mitatu, mwaka kwa mwaka; naye Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, Ni kwa ajili ya Sauli, na kwa nyumba yake yenye damu, kwa kuwa aliwaua hao Wagibeoni. 2 Ndipo mfalme akawaita Wagibeoni akawaambia; (basi Wagibeoni si wa wana wa Israeli, ila ni wa masalio ya Waamori; na wana wa Israeli walikuwa wamewaapia; lakini Sauli akatafuta kuwaua katika juhudi yake   kwa ajili ya wana wa Israeli na Yuda;) 3 basi Daudi akawaambia hao Wagibeoni, Niwatendee nini? Na kwa tendo gani nifanye upatanisho,  mpate kuubariki urithi wa Bwana? 4 Na hao Wagibeoni wakamwambia, Si jambo la fedha wala dhahabu lililo kati ya sisi na Sauli, au nyumba yake;   wala si juu yetu kumwua mtu ye yote katika Israeli. Akasema Mtakayoyanena, ndiyo nitakayowatendea ninyi. 5 Wakamwambia mfalme, Yule mtu aliyetupoteza, na kutufanyia shauri la kutuharibu, tusikae katika mipaka yo yote ya Israeli, 6 basi, na tutolewe watu saba katika wanawe, nasi tutawatundika mbele za Bwana katika Gibeoni, katika mlima wa Bwana. Mfalme akasema, Nitawatoa.]… Daudi aliingia kumilikibaada ya Sauli, na laana ya ukame ikatokea kipindi cha utawala wa Daudi. Ndiposa Bwana akampa Daudi ufafanuzi wa ile laana.  Inapokuwepo laana, mema yote huzuiliwa yasije, hata kama utajitahidi namna gani.  Si vyema  kuishi vibya na mtu mwingine, kwani huyo  mtu akiiingia mbele za Mungu na kuongea sirini mbele za Mungu kinyume na wewe kuidai haki yake, maneno yake hufanyika laana kwako. Yapo  mashetani yanayoingia kazini  kushikilia aina hii ya maneno. Daudi ingawa siye aliyewaua Wagibeoni, aliwaita wale watu na kuongea nao ili kuyamaliza.
UKIRI
Mungu naomba unisaidie, kama kuna mtu aliyelia machozi ka ajili yangu naomba unikumbushe, na unipe ujasiri wa kumfuata na kumalizana naye kwa Jina la Yesu. Amen
 


2 SAMWELI 3:28-29…[Hata baadaye Daudi aliposikia, akasema, Mimi na ufalme wangu hatuna hatia milele mbele za Bwana, kwa sababu ya damu ya Abneri, mwana wa Neri; 29 na imwangukie Yoabu kichwani pake, na nyumba yote ya babaye, tena hiyo nyumba ya Yoabu isikose kuwa na mtu mwenye kutoka damu, au aliye na ukoma, au mwenye kutegemea fimbo, au mwenye kuanguka kwa upanga au mwenye kuhitaji chakula.]…. Katika baadhi ya koo, unapoona watu wanatokwa damu ujue kuna laana inawafuatilia. Maana yake yupo mtu aliwahi kuwatamka laana ya aina hiyo kwa watu wa ukoo huo. Leo ni siku kwa watu wa aina hiyo kuzivunja laana hizo kwa Jina  la Yesu.
AYUBU 2:4-7…..[ 4 Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake. 5 Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako. 6 Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yeye yumo mkononi mwako; lakini tunza tu uhai wake. 7 Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana, akampiga Ayubu na majipu mabaya tangu wayo wa mguu hata utosi wa kichwa.]….  Shetani alikuwa anatafuta mlngo kuingia kwa Ayubu, na akeshapata mlango huweza kuharibu apendavyo.
GALATIA 3:13...[ Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti; 14 ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.]… Leo ni siku ya kujitoa katika aina zote za laana za koo zetu,  nchi yetu, ardhi zetu kwa kuwa Kristo alifanywa laana kwa ajili yetu ili tuzipate zile Baraka za Ibrahimu na ahadi ya Roho kwa njia ya  imani.
UKIRI
Baba wa Mbinguni, ninaomba msamaha Bwana, yamkni kuna jambo nimelifanya limeleta laana kwenye uzao wa tumbo langu, naungama uovu wangu nilioufanya mimi,  au walionitangulia, ndugu zangu, watawala wan chi yangu, nami leo Bwana napitia uhairibifu kwa laana hiyo, ya nchi au ukoo wangu, naomba msamaha kwako Bwana, kwa ajili ya laana iliyoachiliwa kuja kwangu, kwenye  kazi yangu,  kwenye nchi yangu, naitumia Damu ya Yesu, Damu ya Agano Jipya, leo initakase,  inene mema kwa ajili yangu. Naivunja laana kwenye ardhi. Naitumia  Damu ya Yesu mwenye haki, kuvunja laana, inenayo mema kuliko damu  ya Habili. Naiharibu laana, ya taifa, ya ukoo,  ya wachawi,  ya shetani kwa Damu ya Mwanakondoo. Amen
 


ZEKARIA 5:3-4….[Ndipo akaniambia, Hii ndiyo laana itokayo kwenda juu ya uso wa nchi yote; maana kwa hiyo kila aibaye atatolewa kama ilivyo upande mmoja, na kwa hiyo kila aapaye atatolewa kama ilivyo upande wa pili. 4 Nitaituma itokee, asema Bwana wa majeshi, nayo itaingia katika nyumba ya mwivi, na katika nyumba yake yeye aapaye kwa uongo kwa jina langu; nayo itakaa katikati ya nyumba yake, na kuiteketeza, pamoja na boriti zake na mawe yake.]…. Leo tunaituma laana iliyokuja kwetu irudiilkotoka  kwa Jina la Yesu

Comments