AMENITOKEA ANA SURA NYINGINE


Na  Mcunhaji Adriano Makazi Ufufuo na uzima  Morogoro.

Utangulizi:  Somo letu linaitwa Amenitokea Ana Sura Nyingine”. Yesu ana sura nyingi sana, na hutokea watu kwa sura tofauti. Ndiyo maana Yesu alivyokutokea mwaka jana,  siyo kama atakavyokutokea mwaka huu. Au jinsi Yesu alivyokutokoea mwezi jana sivyo ambavyo alivyokutokea mwezi huu.

UFUNUO 1:9-20….[Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi. 9 Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya Yesu Kristo, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu. 10 Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu, 11 ikisema, Haya uyaonayo uyaandike katika chuo, ukayapeleke kwa hayo makanisa saba: Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia. 12 Nikageuka niione ile sauti iliyosema nami. Na nilipogeuka, niliona vinara vya taa saba vya dhahabu; 13 na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini. 14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji; na macho yake kama mwali wa moto; 15 na miguu yake kama shaba iliyosuguliwa sana, kana kwamba imesafishwa katika tanuru; na sauti yake kama sauti ya maji mengi. 16 Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume; na upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa chake; na uso wake kama jua liking'aa kwa nguvu zake. 17 Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, 18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu. 19 Basi, uyaandike mambo hayo uliyoyaona, nayo yaliyopo, na yale yatakayokuwa baada ya hayo. 20 Siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume, na ya vile vinara saba vya dhahabu. Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba; na vile vinara saba ni makanisa saba.]… Yesu katika wale wanafunzi 12, alikuwa na wanafunzi watatu aliokuwa anawapenda sana: Yakobo, Petro na Yohana. Kila mwanafunzi mmoja anazo sifa zake  za utambuzi: Yohana akiwa na hekima za kufundisha wengine kuhusu UPENDO, ikidhihirishwa na zile nyaraka alizoandika. Yakobo alikuwa ni mwalimu wa TUMAINI,  na hata kwa mtu aliyekata tamaa, ilikuwa ni rahisi kufarijika. Petro alikuwa mzuri sana katika kufundisha mambo  ya IMANI.
Yesu aliwahi  kusema kuwa mmoja wa wanafunzi wake hatokufa kabisa, naye ni YOHANA,ambaye walimtesa sana, wakamtupa katika mafuta ya moto, lakini hata hivyo hakufa. Ndiposa walipomtupa  katika kisiwa vha Patmo,  ambapo alikaa upweke na wanyama wakali  wakiwemo dubu.


Yesu alimtokea Yohana akiwa na sura na umbo tofauti kabisa. Wanafunzi watatu wa Yesu aliowawapenda zaidi walikuwa na kawaida ya kuegama katika kifua chake. Hata hivyo,  Yohana alijishangaa mara hii kuona Yule Yule aliyekuwa anaegama kifuani mwake mbona leo  inakuwa ngumu hata kumtambua?
MARKO 16:12-13…[Baada ya hayo akawatokea watu wawili miongoni mwao, ana sura nyingine; nao walikuwa wakishika njia kwenda shamba. 13 Na hao wakaenda zao wakawapa habari wale wengine; wala hao hawakuwasadiki.  ]…. Hapa tunajifunza kuwa, wale wanaoenda shamba, shule, kazini, hospitalini,n.k Bwana huwa anaweza kuwatokea na ktana na hitaji lao kwa kuwa Yesu hana ubaguzi.
LUKA 24:13 …[ Na tazama, siku ile ile watu wawili miongoni mwao walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili. 14 Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia. 15 Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao. 16 Macho yao yakafumbwa wasimtambue. 17 Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao. 18 Akajibu mmoja wao, jina lake Kleopa, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi? 19 Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote; 20 tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha. 21 Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo; 22 tena, wanawake kadha wa kadha wa kwetu walitushitusha, waliokwenda kaburini asubuhi na mapema, 23 wasiuone mwili wake; wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosema kwamba yu hai. 24 Na wengine waliokuwa pamoja nasi walikwenda kaburini wakaona vivyo hivyo kama wale wanawake walivyosema, ila yeye hawakumwona.  25 Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii! 26 Je! Haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake? 27 Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe. 28 Wakakikaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, naye alifanya kama anataka kuendelea mbele. 29 Wakamshawishi wakisema, Kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukaa nao. 30 Ikawa alipokuwa ameketi nao chakulani, alitwaa mkate, akaubariki, akaumega, akawapa. 31 Yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua; kisha akatoweka mbele yao. 32 Wakaambiana, Je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko? 33 Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao, 34 wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, naye amemtokea Simoni. 35 Nao waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyotambulikana nao katika kuumega mkate.]… Ukeshakuwa unasemezana na wengine habari za Yesu,  Yesu  huja na kuambatana nanyi. Yesu huungana nasi tunapozungumzia habari zake. Tunapolifunua neno la Mungu leo, Yesu naye afunuliwe kwetu. Baada ya Yesu kuumega mkate, wale watu walifunguliwa macho yao.

LENGO LA SOMO LA LEO

1.      Yesu ana uwezo wa kugeuka sura
2.      Yesu ana uwezo wa kukutokea akiwa na sura nyingine (maana yake, alivyokutokeea jana sivyo atakavyokutokea kesho)
 
YOHANA 1:9…[ 11 Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea. 12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;]…..Yesu anawazungumzia Wayahudi,  ambao hata baada ya kutokea wao hawakumpokea. Ni kwa sababu, Wayahudi walitarajia masiya atazaliwa kwenye familia ya kitajiri,  lakini badala yake akazaliwa katika hori la kulia ng’ombe, hali ya umaskini kabisa.

KUTOKA 6:2-3…[Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, Mimi ni YEHOVA; 3 nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao.]…. Ina maana kuwa, ni  wepesi zaidi kwa Musa kumfahamu Mungu kuliko baba zake. Kwamba baba zake Musa hawakuwahi kumjua Mungu kwa jina la Yehova. Ndiyo maana hata sasa, wapo wengi wasioelewa maana ya Ufufuo na Uzima. Maana yake, Mungu ni  Yule Yule mmoja lakini huvijia vizazi kwa namna tofauti.
UKIRI
Bwana Yesu,  Ninaomba unipe akili ya kujua waweza kunitokea kwamba waweza kunitokea katika sura nyingine, ninaomba unipe  imani, unipe ujasiri na nuru yako ya kujjifunza maneno ya uzima, kwa  Jina la Yesu. Amen
 

Shetani ambaye ni mungu wa dunia hiii, hupofusha fikra za watu ili wasiijue kweli. Imeandikwa katika 2KORINTHO 4:4….[Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; 4 ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.]…. Maana yake, nuru ya injili yenye kuondoa giza haiwezi kuwazukia waliopo chini ya shetani. Ikumbukwe kuwa mwanadamu  ana sehemu tatu: mwili, nafsi na roho. Tunajua je haya?
Imeandikwa katika 1 THESALONIKE 5:23…[ 23 Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.]…
Imeandikwa katika MWANZO 1:25….[Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.]….Maana yake mwili na roho huifanya nafsi.  Muunganiko huu wa mwili na roho ukitengana, nafsi nayo hutoweka.
NAFSI nayo imeundwa na viitu vitatu: NIA, HISIA na UTASHI. Nafsi ni sawa na masjala ambayo hufanya usajili,ni kama ghala ambalo  hutunza vitu. Mtu anapokosa kumbu kumbu zake, ni kuwa ndani  ya nafsi yake taarifa hizi zimepotea. Nia ni  idara ya fikra (2KORINTHO 4:4). Nia ya mtu ndipo anapofikiri mtu. Mungu hakuwahi kumuumba mwanadamu akiwa na mapungufu. Ndiyo  maana baada tu ya Mungu kumaliza uumbaji alisema kila kitu  alichoumba kilikuwa chema. Hakuna aliyeumbwa akiwa mbumbumbu. Mungu aliviumba vyote vikiwa vikamilifu. Ni vyema kukataa kuitwa majina kama vile  vile: ‘Mama wa nyumbani’, kwa sababu Mungu hajwahi kumuumba mwanamke awe wa kukaa nyumbani.
UKIRI
Kwa Jina la Yesu, Baba wangu wa mbinguni,ninaomba fikra zangu zilizokamatwa na kutiwa giza na mashetani  ziachiliwe,  nanyunyiza Damu ya Yesu,  kwa kila anayetumia nia yangu nakuamuru achia nia yangu kwa Damu ya Yesu.  
Baba yangu wa mbinguni najua ulimuumba mtu ukamwekea pumzi ya uhai, mtu akawa nafsi hai,  leo naidai nafsi yangu hai kwa Jina la Yesu. Eneo la mawazo leo naondoa vifungo vya mashetani kwa Jina la Yesu. Naiondoa laana iliyo katika fikra zangu kwa Jina la Yesu. Naondoa uzito kwenye nia yangu, na kwenye akili yangu, nafyatua kwa Jina la Yesu. Achia nia yangu kwa Jina la Yesu. Amen


SHETANI HUPOFUSHAJE FIKRA ZA MTU?
MATHAYO 28:11-15…[Nao wale walipokuwa wakienda, tazama, baadhi ya askari waliingia mjini, wakawapasha wakuu wa makuhani habari za mambo yote yaliyotendeka. 12 Wakakusanyika pamoja na wazee, wakafanya shauri, wakawapa askari fedha nyingi, 13 wakisema, Semeni, ya kwamba wanafunzi wake walikuja usiku, wakamwiba, sisi tulipokuwa tumelala. 14 Na neno hili likisikilikana kwa liwali, sisi tutasema naye, nanyi tutawaondolea wasiwasi. 15 Basi wakazitwaa zile fedha, wakafanya kama walivyofundishwa. Na neno hilo likaenea kati ya Wayahudi hata leo. ]… Askari walipewa fedha nyingi ili waseme uwongo. Hapa ni kuwa Wayahudi walipofushwa fikra zao hadi leo kuhusiana na ufufuo wa Yesu. Shetani hutumia aina hii ya mfumo kupindisha ukweli. Yapo pia mafundisho ya  kishetani  ambayo nyakati kadha kadhaa watu wakiyasikiliza basi hugeuka na kuwa sababu ya upofu wa fikra zao, kwa sababu imani huja kwa kusikia.

Comments