![]() |
Na Mchungaji kiongozi Josephat Gwajima, ufufuo na uzima. |
Mungu anataka tushindane na ametugawia nguvu ya kupigana, Mungu huwa anakupa vinavyomilikiwa na watu ili upigane na kuvimiliki. Watu wengi katika kanisa leo wamesahu hilo, wanaamini kwamba Mungu akisema amekupa tayari umeshapata kumbe kuna vita ya kupigana.
Ndio sababu watu wengi walioahidiwa vitu na Mungu hawajaviona vikitokea
mpaka Leo, kwasababu waliokaa wakaridhika wakaacha kufanya vita. Mungu
anapokuahidi jambo inatakiwa ujue ufanyeje ili kupokea ahadi ya Bwana
katika maisha yako.
Imeandikwa: Ilikuwa hapo Farao alipokwisha kuwaacha watu hao waende zao, Mungu hakuwaongoza kwa njia ya nchi ya Wafilisti, ijapokuwa ilikuwa ni ya karibu; maana Mungu alisema, Wasije wakaghairi watu hawa hapo watakapokutana na vita, na kurudi Misri; (KUT. 13:17 SUV)
Mungu aliwaongoza njia isiyokua na vita kali, lakini njia inayooitwa haina vita ndio ile ile waliopigana na Waamaleki, pamoja na mataifa mengine. Ilifika kipindi ikabidi Mungu asimamishe jua ili Israel wapigane vita.
Mungu akataka hata watoto waliozaliwa katika nchi ya ahadi wajifunze kupigana vita, ndio sababu akawaacha mataifa matano katika nchi hiyo ili wapigane nao vita.
Imeandikwa: Basi haya ndiyo mataifa ambao BWANA aliwaacha, ili awajaribu Israeli kwa hao, yaani, awajaribu hao wote ambao hawakuvijua vita vyote vya Kanaani; (AMU. 3:1 SUV)
Hii ndio sababu wakati mwingine Mungu anaruhusu magumu au changamoto ili ujifunze kupigana vita. Ndio sababu Mungu anaitwa "Bwana wa vita"
Paulo alimwambia mwanae wa kiroho Timotheo kuwa amepigana vita.
Imeandikwa: Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; (2 TIM. 4:7 SUV)
Huwezi kumiliki pasipo kufanya vita.
Mungu na akupe Neema ya kufanya vita ili umiliki kila ulichoahidiwa na Bwana kwa jina la Yesu.
Imeandikwa: Ilikuwa hapo Farao alipokwisha kuwaacha watu hao waende zao, Mungu hakuwaongoza kwa njia ya nchi ya Wafilisti, ijapokuwa ilikuwa ni ya karibu; maana Mungu alisema, Wasije wakaghairi watu hawa hapo watakapokutana na vita, na kurudi Misri; (KUT. 13:17 SUV)
Mungu aliwaongoza njia isiyokua na vita kali, lakini njia inayooitwa haina vita ndio ile ile waliopigana na Waamaleki, pamoja na mataifa mengine. Ilifika kipindi ikabidi Mungu asimamishe jua ili Israel wapigane vita.
Mungu akataka hata watoto waliozaliwa katika nchi ya ahadi wajifunze kupigana vita, ndio sababu akawaacha mataifa matano katika nchi hiyo ili wapigane nao vita.
Imeandikwa: Basi haya ndiyo mataifa ambao BWANA aliwaacha, ili awajaribu Israeli kwa hao, yaani, awajaribu hao wote ambao hawakuvijua vita vyote vya Kanaani; (AMU. 3:1 SUV)
Hii ndio sababu wakati mwingine Mungu anaruhusu magumu au changamoto ili ujifunze kupigana vita. Ndio sababu Mungu anaitwa "Bwana wa vita"
Paulo alimwambia mwanae wa kiroho Timotheo kuwa amepigana vita.
Imeandikwa: Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; (2 TIM. 4:7 SUV)
Huwezi kumiliki pasipo kufanya vita.
Mungu na akupe Neema ya kufanya vita ili umiliki kila ulichoahidiwa na Bwana kwa jina la Yesu.
Comments