Bwana Yesu asifiwe…
Siku moja nilipokuwa nimetulia Roho akasema nami kwa habari
ya ulinzi wa kiroho kwa mwamini. Akaniuliza Je ni kweli ulinzi wa watu
wangu upo katika kitu kiwayo chote hata kama kimeombewa na mtumishi?
Kwamba kitu hicho ndio kifanyike ulinzi kwa mwamini?
Kwa kweli sikuwa na jibu kipindi hicho,maana naliwaza nikawazua,nikafikiri kwamba inawezekana kulindwa na chochote kile kwa yule anaeamini.
Kwa kweli sikuwa na jibu kipindi hicho,maana naliwaza nikawazua,nikafikiri kwamba inawezekana kulindwa na chochote kile kwa yule anaeamini.
Ndiposa Roho akanichukua mpaka katika maneno aliyoyasema
Bwana Yesu,ambayo maneno hayo ndio asemayo leo. Akanipeleka mpaka katika
kitabu cha Yohana,ile sura ya 17:12.
Imeandikwa;
Imeandikwa;
” Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako
ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule
mwana wa upotevu, ili andiko litimie. ” Yoh.17:12
Maneno hayo ni maneno ya Bwana Yesu mwenyewe,yalikuwa ni maombi ya Bwana.
Swali hili ( Je mtu huweza kulindwa kwa kitambaa,au
mafuta,au maji yaliyoombewa na mchungaji ) ni moja ya maswali muhimu na
makini sana katika imani yako.
Si wengi wenye kujiuliza swali kama hilo,wengi huwa tunapokea au kufanya chochote kile tunachokiamini kuwa ni kinga yetu.
Si wengi wenye kujiuliza swali kama hilo,wengi huwa tunapokea au kufanya chochote kile tunachokiamini kuwa ni kinga yetu.
Wengine hawapendi kulisikia jambo hili likihubiriwa sababu
wanaona kana kwamba wao wanaohubiri wasije wakaharibu imani yao. Leo
nami imenilazimu kuyaeleza haya mambo wazi wazi pasipo kumuonea mtu
haya! kama vile alivyonionesha Roho wa Bwana.
Katika andiko lile lile alilolifunua Roho wa Bwana,ndilo nami naanzia papo hapo.
Bwana Yesu anatuambia wazi wazi kabisa ya kuwa ulinzi wa mtu upo katika jina lake tu. Biblia inasema Bwana Yesu alupokuwapo aliwalinda kwa JINA LAKE pekee,wala hazungumzii ulinzi wa kitu chochote kile.
Bwana Yesu anatuambia wazi wazi kabisa ya kuwa ulinzi wa mtu upo katika jina lake tu. Biblia inasema Bwana Yesu alupokuwapo aliwalinda kwa JINA LAKE pekee,wala hazungumzii ulinzi wa kitu chochote kile.


Unapolitamka jina la Yesu Kristo kwa habari ya ulinzi,na damu yake uhusika.
Jibu la swali la hapo juu ni hili.
Mtu hawezi kulindwa kwa kitambaa,wala maji wala chumvi,wala mafuta,wala
hawezi kulindwa na kitu chochote kile hata kama kimeombewa na
mchungaji. Ulinzi wa mwamini haupo katika kitu bali upo katika jina la
Yesu Kristo tu.

Roho alinifunulia haya ili niwaambie ndugu zangu wenye
kutembea na vitambaa vya upako kama kinga yao,na wale wenye kutegemea
maji,au mafuta kama kinga kwao,kwamba vitu hivyo havina ulinzi wowote
ule.
Vitu vya namna hiyo ni kama uganga wa kawaida kabisa. Maana
ipo tofauti gani kwa yule mwenye kutembea na kitambaa kama kinga yake
na yule mwenye kutembea na irizi kama kinga yake?
Utofauti wa hawa wawili upo wapi?
Utofauti wa hawa wawili upo wapi?
Tuangalie neno la Bwana linasemaje
” Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza;…” Yoh. 17:12
” Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza;…” Yoh. 17:12
Yesu anazungumzia ulinzi kwa jina lake,wala hazungumzii
ulinzi kwa mafuta,maji,kitambaa bali kwa jina lake. Na anazidi kusema
kuwa jina lake lina kazi ya kutunza. Hii ikiwa ina maana kuwa,jina la
Yesu lina ulinzi tosha na linautunzaji kwa wale wenye kumuamini.
Naomba unielewe kwamba;
Roho mtakatifu Yeye ni Mungu wa utaratibu na njia zake hazichunguziki. Roho mtakatifu anaweza kumuelekeza mtumishi wake,atumie mafuta katika ibada fulani kwa ajili ya kufungua nira za yule aliyefungwa ( Isaya 10:27 ) . Kwa habari ya jambo kama hilo sio mbaya,maana ni Roho mwenyewe yupo kazini saa ile ile katika ibada.
Roho mtakatifu Yeye ni Mungu wa utaratibu na njia zake hazichunguziki. Roho mtakatifu anaweza kumuelekeza mtumishi wake,atumie mafuta katika ibada fulani kwa ajili ya kufungua nira za yule aliyefungwa ( Isaya 10:27 ) . Kwa habari ya jambo kama hilo sio mbaya,maana ni Roho mwenyewe yupo kazini saa ile ile katika ibada.
Lakini ubaya unakuja pale mtumishi anapotumia mafuta kwa
kuyaombea au kitambaa kisha na kuwapa waamini waende navyo kama kinga
yao,watembee navyo muda wote kama ulinzi wao.Hilo ndio tatizo kubwa sana,!!
Pameandikwa wapi,kwamba watu walindwe na vitambaa,au maji,au mafuta au chumvi,au mchanga ?
Pameandikwa wapi,kwamba watu walindwe na vitambaa,au maji,au mafuta au chumvi,au mchanga ?
Mpendwa imefika wakati wa kugeuka kutoka katika
kuvitumainia vitu viaribikavyo na kuanza kulitumainia jina la Yesu
Kristo. Jina hili ndilo tulilopewa wanadamu litupasalo kuokolewa kwalo (
Matendo 4:12 ).Hatuna haja tena ya kutegemea kitu kingine ikiwa
tumepewa jina la Yesu.
Wakati mmoja nalipokuwa naelekea Israeli, watu wengi
wakristo waliniagiza vitu mbali mbali nije navyo. Wengine walinituma
nije na mchanga wa Isareli,wengine walinitaka nibebe matope ya
Israeli,wengne walihitaji mafuta ya upako. N.K,basi tu kila mmoja
alikuwa na lake kulingana na kile anachokiamini.Lakini cha kushangaza
hakuna hata mmoja wao aliyeniagiza nije na Yesu wa Nazareti,yaani nije
na upako.
Ndipo sasa nikaangalia imani yao,nikagundua kwamba imani ya
wakristo wengi siku ya leo imeegemea katika vitu na sio katika uweza wa
jina la Yesu Kristo,hii ni shida kubwa katika kanisa la leo.
Unajua ni shetani ndio ameingia hata kwa baadhi ya wachungaji na kwa waamini kwa kubadilisha imani yao kwamba wasiliamini jina la Yesu Kristo na kugeukia vitu vilivyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu kwa kuvifanya ndio miungu yao.
Unajua ni shetani ndio ameingia hata kwa baadhi ya wachungaji na kwa waamini kwa kubadilisha imani yao kwamba wasiliamini jina la Yesu Kristo na kugeukia vitu vilivyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu kwa kuvifanya ndio miungu yao.
Mpendwa,kataa kuvitumainia vitu hivyo kwa ulinzi bali
litumainie jina la Bwana pamoja na damu yake kwa ulinzi tosha wa maisha
yako. Hakuna awezaye kulinda maisha yako isipokuwa Yesu Kristo tu. Kwa
jina lake sisi tunakuwa na uzima,kwa jina lake tunaishi na kwa jina lake
tunakwenda kwa ushindi tele.
Ushauri wangu wa bure kwako;
Ikiwa mtu amekuamanisha kuvitumainia vitu vingine,umuulize
amepata wapi imani ya namna hiyo? Maana hatukuagizwa kutembea na ulinzi
wa namna nyingine iwayo yote isipokuwa jina la Yesu tu na damu yake.
Kwa huduma ya maombi na maombezi nipigie;
0655-11 11 49.
Mch. Gasper Madumla
Beroya bible fellowship church-Kimara
UBARIKIWE.

Comments