Karibu
tujifunze Neno hai la MUNGU Mwenyezi.
Hatimaye
siku ya mwisho itafika.
Siku hiyo
wababe wote wa dunia watakuwa wapole kama kondoo.
Wanaokataa
Wokovu wa BWANA YESU leo siku hiyo watakuwa wapole sana.
Isaya 1:31 ‘’
Na mtu hodari atakuwa kama makumbi, na kazi yake kama cheche ya moto; nao
watawaka pamoja, wala hapana atakayewazima. ‘’
-Watu hodari
siku hiyo watakuwa wapole.
-Wale hodari
kwa kufanya dhambi watawaka moto wala hapana wa kuwazima.
-Wanaomkataa
YESU leo siku hiyo watamjua yeye ni nani.
-Siku hiyo
BWANA pekee ndiye atakayetukuzwa..
Isaya
2:11-12 ‘’ Macho ya mwanadamu yaliyoinuka yatashushwa chini, na kiburi cha mwanadamu
kitainamishwa, naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo. Kwa maana
kutakuwa siku ya BWANA wa majeshi juu ya
watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo
yatashushwa chini. ‘’.
-Wanaojivuna
leo kwa sababu ya umaarufu wao wa dhambi, siku hiyo watakuwa wapole sana.
-Wanaotesa
wanadamu wenzao leo, siku hiyo watawaka moto milele.
-Watenda
dhambi wasiotubu leo, siku hiyo watalia na kusaga meno hadi meno yataisha nab
ado hata asilimia 1% ya kulia watakuwa hawajaimaliza.
Maonyo hayo
ni makali lakini muda wa kugeuka na kutubu ni leo kabla ya kifo kufika.
Muda wa
Kuokoka na kuanza kuliishi neno la MUNGU ni leo wala sio kesho.Usikubali
kumkataa YESU.
Ni muda wa
kuacha dhambi maana ukiendelea na dhambi
maisha yako yote basi tambua kwamba kuna ziwa la moto mbeleni. Ni ziwa
la moto ambalo watakaoingia humo watazama na kuteseka milele. Hakutakuwa tena
na kifo wakati huo, kifo kitazuiliwa na yatakuwa mateso makali sana maana
ndivyo Biblia isemavyo. BWANA YESU ni muhimu kwako leo kuliko yote uyawazayo
wala uyatendayo. Mpokee na jina lako litaandikwa kwenye kitabu cha uzima.
Ukishindwa
kumtii KRISTO basi hakika unamtii shetani.
Kumbuka
shetani hatakuwa na wa kumcheka siku hiyo maana hata yeye na nabii wa uongo
wake watatupwa kwenye ziwa la moto tena hata kabla ya wanadamu kuhukumiwa.
Siku hiyo
inakuja, ndugu yangu, ni bora Kuokoka leo.
Viburi nya
duniani havitamsaidia mtu yeyote.
Siku hiyo
atatukuzwa BWANA pekee.
Isaya
2:17-20 ‘’ Na majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu
kitashushwa; naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo. Nazo sanamu
zitatoweka kabisa. Na watu wataingia ndani ya pango za majabali, na ndani ya
mashimo ya nchi, mbele za utisho wa BWANA na utukufu wa enzi yake, atakapoondoka ili
aitetemeshe mno dunia. Siku hiyo kila mtu atazitupilia mbali sanamu zake za
fedha, na sanamu zake za dhahabu, walizojifanyia ili kuziabudu, kwa fuko na
popo; ‘’
-Siku hiyo
hakutakuwa na mtu maarufu na Yule ambaye hakuwa maarufu duniani.
Siku hiyo
hakutakuwa na raisi wala mbunge, hakutakuwa na diwani wala meneja, hakutakuwa
na machinga wala mamantilie, wote watakuwa sawa wakihukumiwa kila mmoja
sawasawa na dhambi Na matendo yake.
Hakuna
umaarufu wa sasa wa mtu utakaomsaidia
siku hiyo.
Ndugu yangu,
Leo yako ndio inayoamua kesho yako itakavyokuwa. Mwamini YESU leo na mpokee ili
kesho yako iwe mbinguni na sio motoni.
Mpokee YESU
KRISTO leo, ishi maisha matakatifu,
jitenge na dhambi na jitenge na kila machukizo.
Wanaomdharau
YESU leo siku hiyo watapiga magoti mbele yake bila mafanikio.
Wanaomdharau
BWANA YESU leo siku hiyo watamkiri sana ila watakuwa wamechelewa.
Wafilipi
2:9-11 ‘’ Kwa hiyo tena MUNGU alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile
lipitalo kila jina; ili
kwa jina la YESU kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na
vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa
utukufu wa MUNGU BABA. ‘’
-Kumkataa
YESU ni kuukataa uzima wa milele.
Ndugu yangu
uliyesoma ujumbe, nakuomba kama hujampokea BWANA YESU basi mpokee leo maana
hujachelewa. Kama umeshaokoka tayari basi shikilia sana ungamo lako.
MUNGU wa
mbinguni aleta neema yake kuu ya Wokovu Kwa kila ndugu atakayesoma ujumbe huu.
Waefeso
1:17-23 ‘’ MUNGU wa BWANA wetu YESU KRISTO, BABA wa utukufu, awape ninyi roho
ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye; macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue
tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake
katika watakatifu jinsi ulivyo; na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani
yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake; aliotenda
katika KRISTO alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika
ulimwengu wa roho; juu
sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina
litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akavitia vitu
vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya
kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika
vyote. ‘’
-BWANA YESU
ana mamlaka kuu san asana.
Siku ya
Mwisho BWANA YESU atakuja kuhukumu wanadamu wote.
Ukimkimbia leo
na Wokovu wake basi siku hiyo utakuwa na hasara.
Ndugu
Mkimbilie BWANA YESU leo. Yeye BWANA YESU anasema
Ufunuo
22:12-13 ‘’ Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu
kama kazi yake ilivyo. Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa
mwisho. ‘’
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku
nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio
kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na
utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi
kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko
KRISTO BWANA. MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Comments