Askofu Josephat Gwajima. |
Pamoja na hilo, Kibatala aliomba mteja wake huyo kuambiwa kwa maandishi juu ya vitu vinavyotakiwa kuwasilishwa kwa Jeshi hilo.
Barua hiyo ambayo Kibatala ameielekeza kwa Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, pia nakala yake ameituma kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Ernest Mangu na kwa mteja wake huyo.
Barua hiyo ambayo Kibatala ameielekeza kwa Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, pia nakala yake ameituma kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Ernest Mangu na kwa mteja wake huyo.
“Kwa barua hii
tunaomba Jeshi la Polisi kwa niaba ya mteja wetu kumwandikia rasmi kwa
maandishi mteja wetu mkiainisha nyaraka mnazohitaji na vifungu vya
sheria vinavyotumika na Jeshi la Polisi kutaka nyaraka hizo.
“Tutashukuru
kupata hati hiyo, ambayo bado hatujaipa jina, kwani tunategemea jeshi
hilo litafahamu jina la kisheria la nyaraka husika inayotumika kutaka
mteja wetu alete nyaraka tajwa na mara tu mteja wetu akipata maandishi
tuliyoomba atatimiza wito au kuchukua hatua stahiki za kisheria,”
ilisomeka sehemu ya barua hiyo.
Juzi wakili
mwingine wa Gwajima, John Mallya, alilalamikia hatua ya polisi akisema
mahojiano yalichukua mambo binafsi badala ya kile alichoitiwa na
kutakiwa kuwasilisha vitu 10.
Wakili huyo
alitaja mambo yanayotakiwa kuwasilishwa polisi kuwa ni hati ya usajili
wa kanisa, namba ya usajili, majina ya Baraza la Wadhamini (Baraza la
Kiroho), idadi ya makanisa (matawi) anayohudumia, nyaraka za helikopta
ya kanisa na muundo wa uongozi wa kanisa
Vitu vingine ni
waraka wa maaskofu uliosomwa makanisa yote, nyaraka za nyumba na mali
za kanisa, nyaraka kuonyesha taarifa za hesabu kutoka kwa Msajili wa
Vyama vya Hiari na kuambatana na mtu anayepiga picha za video kanisani
hapo.
Hata hivyo,
katika barua ya wakili huyo wa Gwajima, Kibatala, ilieleza kwa mshangao
kwamba Askofu huyo, ambaye anatuhumiwa au anapelelezwa kuhusiana na
tuhuma za kutoa lugha ya matusi wakati wa mahojiano, hakutaarifiwa kama
tuhuma hizo ziko chini ya kifungu gani cha sheria.
Gwajima
alitakiwa kurejea katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam Aprili 16,
mwaka huu, akiwa na vitu hivyo 10, hatua ambayo imekuja kinyume na
matarajio ya wengi kuwa kiongozi huyo angekuwa anahojiwa tu kuhusu
matamshi yake ya kashfa dhidi ya Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Dar es Salaam,
Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.
Kutokana na
matamshi hayo yaliyosambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii kwa njia
ya video na sauti, Gwajima alitakiwa kuripoti polisi kuhojiwa Machi 27,
mwaka huu, ambapo kabla ya kukamilika kwa mahojiano aliishiwa nguvu na
kupelekwa hospitalini alikolazwa kwa siku nne, huku taarifa zikieleza
kuwa alishtushwa na kuhojiwa taarifa binafsi badala ya tuhuma alizoitiwa
polisi.
Baada ya kutoka
hospitalini, Gwajima aliendelea kutembea akiwa kwenye kiti chenye
magurudumu, alichotumia hadi Aprili 6, alipohubiri katika Ibada ya
Pasaka ambako alionekana kusimama kutokana na kudai kuombewa na
wachungaji wageni waliofika kanisani hapo kutoka Japan.
Kamishina Kova hakupatikana kuzungumzia kupokea barua hiyo kutokana na simu yake kuita bila majibu.
Source:Mwananchi
Comments