BWANA YESU
atukuzwe ndugu yangu.
Karibu
tujifunze neno la MUNGU la uzima wa roho zetu.
Isaya 1:28 ‘’
Lakini kuharibika kwao wakosao nao wenye dhambi kutatokea wakati mmoja, nao
wamwachao BWANA watateketezwa. ‘’
=Wakosaji
watateketezwa siku ya mwisho kama hawatatubu wangali hai leo.
Wakosaji ni
wale wanaomkataa YESU na kukataa kuishi kwa kulifuata Neno la MUNGU, Hawataki
utakatifu, hata kama wanakwenda kanisani lakini kama ni wakosaji kwa MUNGU hao
wanatakiwa watubu maana wasipotubu kuna jehanamu mbeleni.
=Wenye
dhambi watateketezwa kama wasipotubu wangali hai.
Wenye dhambi
karibia wote wanajifahamu na wanajua kabisa kwamba dhambi hizo zitawafikisha
jehanamu ya milele lakini wameshupaza shingo zao, hawataki kutubu.
=Wamwachao
BWANA watateketezwa kama hawatatubu wakati wakiwa hai duniani.
Wamwachao
BWANA ni wengi sana.
-Kuna ambao
wanamwacha BWANA YESU baada ya kupokea kile walichohitaji kutoka kwake.
Kuna watu
wamepona magonjwa ya ajabu baada ya maombezi, watu hao waliapa mbele ya kanisa
na mbele za MUNGU kwamba wao hawawezi kumuacha BWANA YESU maana amewatendea
makuu sana. Ni kweli ni makuu lakini huwezi amini kuna baadhi ya watu wa jinsi
hiyo hata mwezi hauishi wanaacha wokovu na kurudi duniani. Kuna watu
walipotendewa muujiza na MUNGU waliahidi huku wakitoa machozi mengi kwamba wao
na YESU milele lakini hata miezi miwili haipiti wanarudi tena duniani. Hawamkomeshi
mchungaji wala yeyote bali ni kwa uangamivu wao wenyewe. Wakienda jehanamu
MUNGU hana hasara na kama wakirudi na kutubu kisha wakaenda mbinguni ni kwa
faida yao wenyewe na sio MUNGU. Lakini je! Unamwacha MUNGU ili iweje?
Kumbu 32:15 ‘’
Lakini Yeshuruni alinenepa, akapiga teke; Umenenepa, umekuwa mnene, umewanda;
Ndipo akamwacha MUNGU aliyemfanya, Akamdharau Mwamba wa wokovu wake. ‘’
-Waisraeli
walimwacha BWANA baada ya BWANA kuwapa
amani na furaha, walikuwa tu wanasikia kwamba kuna mataifa ni wakimbizi.
Hata leo
akina Yeshuruni wapo wengi sana.
Kuna mtu
alikuwa mtumishi mzuri wa MUNGU lakini baada tu ya kubarikiwa kwa gari kwa sasa
safari zake sio za kanisani tena kama zamani bali kila siku yuko safarini
kwenda kwenye starehe.
Ndugu yangu,
hata kama BWANA atakubariki utajiri usije ukamwacha.
-Hata kama
umebarikiwa kwa kufunga ndoa takatifu lakini isiwe hiyo ndiyo chanzo cha
kumwacha Mwamba wa wokovu wako.
Kuna watu walikuwa
hawana kazi kwa miaka mingi, waliomba sana , walilia sana lakini hawakupata
maana adui alikuwa anawakamata kwa sababu walikuwa upande wake, watu hao wakaokoka
na kuingia katika ufalme wa Mwana wa pendo la MUNGU, BWANA YESU akawabariki
kazi. Lakini wamekuwa waaminifu mwezi wa kwanza tu lakini baada ya hapo hata
mchungaji akiwapigia simu hawapokei au wanapokea na kusema wako busy kazini
kumbe hata hawako kazini. Ndugu kama unafanya hivyo hiyo ni kwa uangamivu wako
mwenyewe.
Kuna watu
baada ya MUNGU kuwabariki hata Kiswahili wamebadili. Zamani walikuwa
wanyenyekevu sana kwa MUNGU lakini sasa watumishi wakiwatafuta kwenye simu majibu yao ni haya ‘’ I will call you later
au wait a minute kisha hiyo minute
inageuka mwezi mmoja na nusu, au anajibu
I am busy today kumbe wala hakuna busy wala nini’’, Watu hawa wakati wanaombewa
walikuwa wapole sana na hata hawajawahi kuchanganya lugha lakini baada ya Baraka
kufika hawamhitaji tena Mwamba wa Wokovu wao. Ndugu unayefanya hayo tambua
kwamba ni kwa uangamivu wako mwenyewe.
Kuna
watumishi wamewahi kufunga siku 5 au zaidi ili kuwaombea tu watu Fulani wapate
kazi nzuri lakini baada ya MUNGU kuwapa Baraka ya kazi watu hao wamegeuka na
kuanza hata kuwasema vibaya hao hao ambao walilia mbele za MUNGU kwa ajili yao
kwa ajili ya kazi. Ndugu unayefanya hayo tambua kwamba hiyo ni kwa uangamivu
wako mwenyewe.
-Kuna watu
huokoka ili wafanikiwe kisha wakishafanikiwa wanamwacha BWANA YESU aliyewaokoa.
Wagalatia
1:6-7 ‘’ Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema
ya KRISTO, na kugeukia injili ya namna nyingine. Wala si nyingine; lakini wapo
watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya KRISTO. ‘’
-Nastaajabu
unamwacha YESU upesi kiasi hiki.
Umeokoka
baada ya kukaa miaka zaidi ya 35 bila kuolewa maana ulikuwa na laana ya
kutokuolewa, lakini BWANA amekuondolea laana hiyo na umeolewa lakini kwanini
unamwacha BWANA upesi namna hii.
-Umeokoka
baada ya kutangaziwa na wachawi kwamba humalizi mwaka huu, BWANA amekuzingira
pande zote maana wewe sasa ni mtoto wake, lakini je kwanini unataka kumwacha
upesi namna hii?
BWANA YESU
hana hasara, ukimwacha wewe ni kwa kujiangamiza wewe mwenyewe.
Wakati wa
matatizo kila mtu anamtaka YESU amsaidie.
Wakati wa
matatizo kila mtu ni mnyenyekevu sana kwa MUNGU lakini akipokea Baraka yake
anakuwa tofauti, anaweza hata akawatukana watumishi wa MUNGU wale wale
waliomwombea.
Ndugu zangu
kuna madhara kama ukimwacha BWANA YESU aliyekuokoa na kukuponya na mabaya.
Mithali 4:6 ‘’
Usimwache, naye atakuhifadhi; Umpende, naye atakulinda. ‘’
-Ndugu,
usimwache BWANA hata siku moja.
-Kaa katika
wokovu wake siku zote naye atakulinda.
Kuna watu
wanamwacha BWANA hata kama wako makanisani maana dhambi zao ndizo zinawatenga
na MUNGU .
Kuna watumishi wamemwacha BWANA hata kama wako
makanisani, ukiacha agizo la MUNGU maana yake umemwacha MUNGU.
Mafalisayo
walikuwa wanafanya kazi ya MUNGU lakini walikuwa wamechagua tu ya kuyafuata
huku wameacha utakatifu na hawakuwa wanakemea dhambi tena
Luka 11:42 ‘’
Lakini, ole wenu, Mafarisayo, kwa kuwa mwatoa zaka za mnanaa na mchicha na kila
mboga, na huku mwaacha mambo ya adili, na upendo wa MUNGU; iliwapasa kuyafanya
hayo ya kwanza, bila kuyaacha hayo ya pili. ‘’
-YESU
hakuwakataza kutoa zaka alitaka watoe zaka ila sio kutoa zaka tu bali
walitakiwa kumtii MUNGU katika yote.
Hata leo
yawezekana kuna watumishi ambao hawajawahi kukemea dhambi, hawawezi kusisitiza
utakatifu kwa waumini lakini kila siku jambo la kusisitiza ni zaka tu, sio vibaya
kusisitiza zaka maana mteule lazima atoe zaka lakini MUNGU anataka yote kwa
pamoja. Usikemee tu uchawi wakati wazinzi
unawafahamu na haujawahi kuwakemea, BWANA hataki hivyo.
-Hao ambao
huwakemei wamemwacha BWANA hata kama wanahudhuria ibada. MUNGU anataka uwakemee
waovu ili wageuke na kuacha uovu wao. Mitume walikemea dhambi na imani yetu
imesimama katika misingi ya mitume na manabii, mbona hatufuati kile mitume
walichofanya? Ndugu mtumishi wa BWANA YESU nakuomba kemea kwa ujasiri. Wambie watu
waikatae dhambi, waikimbie dhambi, waiogope dhambi na wasifanye dhambi.
Kama
hawajaacha dhambi hao wememwacha BWANA hata kama wanakuja kanisani kila ibada
ikifika.
Yeremia 2:17
‘’ Je! Hukujipatia mambo haya mwenyewe, kwa kuwa umemwacha BWANA, MUNGU wako,
alipokuongoza njiani? ‘’
-Ndugu
unayemwacha BWANA YESU baada ya kubarikiwa unaweza wakati mwingine ukapata
mabaya hapa hapa duniani lakini pia mabaya zaidi ni kama utaondoka bila kurudi
kwa BWANA YESU maana hapo utapata mabaya zaidi yaani jehanamu.
Yeye MUNGU
huwa hamwachi mtu yeyote lakini sisi ndio tunaomwacha, matendo mabaya ndiyo
yanawatenga watu na MUNGU muumbaji wao.
Waebrania
13:5-9 ‘’ Msiwe na tabia ya kupenda
fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema,
Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa. Hata twathubutu kusema, BWANA
ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini? Wakumbukeni wale waliokuwa
wakiwaongoza, waliowaambia neno la MUNGU; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa
mwenendo wao, iigeni imani yao. YESU KRISTO ni yeye yule, jana
na leo na hata milele. Msichukuliwe na mafundisho ya namna nyingine nyingine,
na ya kigeni; maana ni vizuri moyo ufanywe imara kwa neema, wala si kwa
vyakula, ambavyo wao waliokwenda navyo hawakupata faida. ‘’
-Usimwache
BWANA YESU siku zote za maisha yako.
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku
nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio
kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na
utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi
kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko
KRISTO BWANA. MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Comments