MICHORO YA UBAYA

Na Mchungaji Bryson Lema, Ufufuo na uzima Morogoro.
Utangulizi: Ipo michoro ya ubaya katika maisha.usipokuwa mwangalifu, unaweza  kuingia katika  aina hii ya michoro ya ubaya. ZABURI 38:12…[Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego; Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya; Na kufikiri hila mchana kutwa.]…. Daudi alitafakari na kuona jinsi ambavyo wapo watu wanaomwazia mabaya. Daudi mwana wa Yese, alikuwa akichunga kondoo wachache wa baba yake kwa kuwa ndiye aliyeonekana mtoto mdogo kuliko wote, na kwamba hawezi  kuchunga kundi kubwa la kondoo. Haa hivyo, ufalme ulimwangukia Daudi ingawa  baba yake (Yese) hakuwa anaonekana kama ndiye atakayefaa  kutawala. Ndiyo maana Yese hakumuita Daudi mbele ya Nabii Samweli,  kwa sababu alidharauliwa kuwa hakufaa,  ingawa ndiye ambayeMungu  alitaka apakwe mafuta kuwa mfalme.

Wanadamu wanaweza kukuona haufai lakini  ujue kuwa Mungu haangalii kama wandamu wanavyokuwazia. Halipo jambo linaloweza kukupata ambalo  halijatengenezwa. Uonapo kitu, ujue kina mwanzo wake. Kila kitu huanza kwa mchoro. Ukiona mti mahali ujue kuna siku mbegu ya  huo  mti ilidondoka ardhini,ikafa na baadae ikachomoza kuwa mche wa huo mti. Unapoiona pengine ndoa yako ina vurugu,  ujue kuwa huo mgogoro haukuibuka tu wenyewe,  bali  ipomsababu ya kutokea hicho kilichotokea. Ndiyo maana YOHANA 3:16…[Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.]… maana yake Mungu hataki hata mmoja  apotee.  Tena neno linasema Mungu antuwazia mema.sasa iweje maisha yangu hayapo jinsi neno hili halijatokea kwako? Siyo rahisi kwenda salama kama haujafanya juhudi za kuufuta huo  mchoro.

Daudi baada ya kumuua Goliathi, akinamama walianza kumsifia kwa nyimbo wakisema”Sauli ameua eflu,lakiniDaudi kumi elfu”. Jambo  hili liliamsha hasira kwa mfalme Sauli  akaanza kutengeneza michoro ya kumuangamiza Daudi.
ZABURI 56:5-6….[Mchana kutwa wanapotosha maneno yangu, Mawazo yao yote ni juu yangu kunitakia mabaya. 6 Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu, Kwa kuwa wameniotea nafsi yangu.]…. Daudi alikaa na watu na kuona jinsi wale anaoishi nao wanavyojificha na kumjadili kisirisiri.
Hata leo hii  wapo watu ambao bila kujua bado wanapita kwenye zile njia za michoro yenye kuleta uharibifu kwenye maisha yao. Wapo waliokaa vikao kwa kuumia tu  wanapoiona ndoa yako imetulia. Tena mbaya zaidi, pale unapowatangazia kuwa mshahara wako umeongezeka, ni kosa lingine kubwa kwao. Adui wanapoichora hii michoro, huweka na mipaka ya hiyo  michoro.  Huweza kuitengeneza kwa maana kuwa,watoto wako watasoma vizuri hadi sekondari, lakini wakifika chuo kikuu pale tu  wanapomaliza wanachanganyikiwa. Maadui hawa ndio ambao hawataki mtu aishi yale maisha ambayo  Mungu aliyakusudia.
 Usichokijua ni kwamba hata  fedha yako mwenyewe inaweza kuchorewa michoro. Ndiyo maana wengine pale wapatapo fedha, magonjwa hujitokeza au misiba ya kila mara. Adui  huitengeneza michoro hii ili kwamba fedha inapoingia ipate matumizi  yasiyokusudiwa. Wengine kila mishahara inapoingia mwisho wa mwezi, husiha baada ya muda mfupi,na matokeo yake unaingia katika mikopo kwenye  maduka ya wafanya biashara. Wengine hununua bidhaa ambazo  hawazihitaji, ili  angalau tu fedha yako isikae salama kwako. Leo ni  siku ya kuifuta hiyo michoro ya maadui za maisha yetu kwa  Jina la Yesu. Ninacho kifutio ambacho  ni damu ya Yesu,iuliyomwagika  miaka zaidi ya 2015 iliyopita.
MUNGU ANASEMA JE KWA WACHORA MICHORO?

Imeandikwa katika ZABURI 41:5-7…[Adui zangu wananitaja kwa maneno mabaya, Atakufa lini, jina lake likapotea? 6 Na mmoja wao akija kunitazama asema uongo, Moyo wake hujikusanyia maovu, Naye atokapo nje huyanena. 7 Wote wanaonichukia wananinong'ona, Wananiwazia mabaya.]… Mungu wangu hamzuii mtu kuniwazia mabaya.nikijuacho mimi  ni  kuwa maisha yangu yapomikononi  mwa Bwana Yesu. Leo naamuru kuwa, Kila anitakiaye mabaya, aibu ikakae nyumbani kwake kuanzia leokatika Jina la Yesu.  Kama ulifikiri huo mchoro ni wa kuniua,  ujue umekosea, kwa sababu hilo tatizo ulilotengeneza kwangu linamfanya Yesu aliye ndani  yangu atoke nje na kuondoa kila  mchoro ulioniwekea. Hakuna tatizo la kunipoteza, kwa sababu mimi niliwahi kufa, naikazikwa na siku ya tatu nikafufuka. Wewe uliyenichorea mchoro  imenifanya nifahamu  kuwa kumbe mimi ni  shujaa, na kile nilichoa nacho kinawasumbua mioyo yenu.
Ole wako wewe uliyechora mchoro maisha yangu. Ole wako wewe unayecheza na ndoa yangu bila kujua kuwa mume na mke watoka kwa Bwana. Huo mchoro wenu uliua lile jitu lenye kutenda dhambi, na sasa ameibuka mwingine asiyekufa tena,  Kwa sababu hakuna kufa zaidiya mara moja. Kumbe ilitakiwa ule mwili wa dhambikupitia mchoro wenu. Hii ni saa ya kuvaa ule  utukufu. Yusufu alitoka jela na kwenda kutawala. Kama alivyotoka Yesu Kristo toka kaburini, siku ile  ya tatu na wale walinzi wakapigwa usingizi wakaamka wakalikuta kaburi li tupu, vivyo hivyo na wewe uliyenichorea mchoro ninakupiga usingizi, na utakapoamka utakuta mchoro na kaburi uliloniweka lipo  tupu. Vita ikiibuka mtu hubadilishiwa jina.hata askari atokapo  vitani haitwi tena askari, bali hiitwa shujaa. Shida huleta ushindi. Yesu ambaye analo jina kuu kulikomajina yote,alizaliwa katika shida,kwenye hori  ya kulishia ng’ombe. Hata Samsoni alipokuwa anaendelea kusaga ngano katika mateso yake,  zile nywele zikaanza kuota tena.
Kama wewe upo hapa na haujaokoka ni ngumu  kuondoka kwenye huo  mchoro. Ni saa yako kuamua kumpa Yesu Kristo maisha yako  na kupata uwezo wa kuitumia Damu ya Yesu ili  kufuta michoro  iliyotengenezwa kwa ajili  ya maisha yako.
                          © Information Ministry (Ufufuo Na Uzima - Morogoro)

Mtaa wa Nguvu Kazi, (Minara Mitatu), Mkundi-Morogoro.

 /or

Contact our Senior Pastor:

 Dr. Godson Issa Zacharia

 (Ufufuo Na Uzima – Morogoro)

Cellphone: (+255) 757 550878 / +255 719798778

Comments