Mwimbaji wa 
nyimbo za Injili Tanzania Bahati Bukuku  amejitokeza rasmi mbele ya 
uongozi wa chama cha muziki wa injili nchini Tanzania na kutoa taarifa 
yake rasmi  kuamua kusimama pamoja na mmoja kati ya wanaotangaza nia 
kuwania uraisi nchini Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi 
CCM,Mh.Edward Lowassa anayetarajia kutangaza nia yake mjini Arusha.
"Bahati Bukuku 
ametoa taarifa rasmi kwa uongozi wa Chama cha Muziki wa Injili nchini 
Tanzania CHAMUITA na kubainisha wazi kwamba  atakua ni miongoni mwa watu
 watakao kuwepo mjini Arusha katikaViwanja vya Shekh Amr Abedi kumuunga 
mkono Mh. Edward Lowasa  anapoenda kutangaza nia katika harakati za 
kusaka Uraisi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu 2015. 
  | 
Kutoka
 kushoto ni Rais wa CHAMUITA Addo Novemba, Mwimbaji wa nyimbo za Injili 
Tanzania Bahati Bukuku, na Katibu Muenezi wa CHAMUITA Stella Joel 
  | 
Mmoja wa Viogozi wa chama hicho cha Muziki wa injili Tanzania Katibu Muenezi wa CHAMUITA Stella Joel ameeleza
 kwamba wao kama viongozi wamemuelewa na wanamtakia kila la heri katika 
safari yake na shughuli nzima ya kumuunga mkono Mh. Edward Lowasa". 
Credit:Mjap inc blog  
 
Comments