Muimbaji Bahati Bukuku ajitokeza Rasmi Kumuunga mkono Mh.Edward Lowassa mbio za Urais 2015.


Mwimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania Bahati Bukuku  amejitokeza rasmi mbele ya uongozi wa chama cha muziki wa injili nchini Tanzania na kutoa taarifa yake rasmi  kuamua kusimama pamoja na mmoja kati ya wanaotangaza nia kuwania uraisi nchini Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM,Mh.Edward Lowassa anayetarajia kutangaza nia yake mjini Arusha.
"Bahati Bukuku ametoa taarifa rasmi kwa uongozi wa Chama cha Muziki wa Injili nchini Tanzania CHAMUITA na kubainisha wazi kwamba  atakua ni miongoni mwa watu watakao kuwepo mjini Arusha katikaViwanja vya Shekh Amr Abedi kumuunga mkono Mh. Edward Lowasa  anapoenda kutangaza nia katika harakati za kusaka Uraisi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu 2015. 

Kutoka kushoto ni Rais wa CHAMUITA Addo Novemba, Mwimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania Bahati Bukuku, na Katibu Muenezi wa CHAMUITA Stella Joel
Mmoja wa Viogozi wa chama hicho cha Muziki wa injili Tanzania Katibu Muenezi wa CHAMUITA Stella Joel ameeleza kwamba wao kama viongozi wamemuelewa na wanamtakia kila la heri katika safari yake na shughuli nzima ya kumuunga mkono Mh. Edward Lowasa". 

Credit:Mjap inc blog

Comments