NINI MAANA YA UPENDO

Shalom watu wa Mungu;
Leo napenda tukajifunze maana halisi ya neno upendo. Sisi vijana tunatumia sana neno upendo. Love….

I love you!
Biblia katika kitabu cha Marko12:29-31 inasema upendo ni “amri ya kwanza”. Katika kitabu cha Mathayo 22:36-40 biblia inasema upendo ni “amri kuu”. Tunaona upendo ni kitu cha msingi sana katika maisha yetu ya ukristo.

Embedded image permalinkUpendo?
Biblia inasema “upendo ni Mungu” 1Yoh.4:8b; 16. Biblia inaendelea kusema katika upendo Mungu anakaa ndani yetu nasi ndani yake. Mungu anakaa ndani yetu katika Roho mtakatifu (1Yoh.3:24).

Point: Kuwa na upendo ndani yako ni kuwa na Mungu ndani yako.
Mungu ni mtakatifu; hivyo aliye na Mungu ndani yake naye ni mtakatifu. Upendo hutuongoza katika mema yote.
Neno la Mungu linasema; 1Yoh.3:18 tusipende kwa ulimi wala kwa neno, bali kwa tendo na kweli. Tusipende kwa midomo; kwamba unamtangazia mtu kuwa unampenda; unatongoza! bali mwenye upendo wa dhati anaonesha katika matendo.

Vijana wengi wamepotea kwa kudhania kitofauti matendo yanayoashiria upendo. Wengine wamedhania uzinzi; lakini hapo wameangukia katika kifo au dhambi. Biblia inasema tena, 2Petro2:13-14 kuna watu ambao wasiokoma kutenda dhambi, wenye macho yajaayo uzinzi, wenye mioyo iliyozoezwa kutamani… wana wa laana!
Kumbe wapo ambao wanadhani wanapenda kumbe wanatamani tu; wana wa laana! hao ni hatari kwa karamu yenu ya upendo. Wanatamani zinaa na anasa zote; hawakufai kwa kuwa hao watakutenganisha na Mungu wako, yaani watauondoa upendo ndani yako. Haleluya!
Upendo ni kutenda matendo mema. Biblia inasema tupatapo nafasi tuwatendee mema watu wote, Galatia 6:9-10. Tena Neno la Mungu linasema, utawezaje kumpenda Mungu usiyemwona wakati unamchukia ndugu yako unayeishi naye?
Biblia inasema Marko12:31 mpende Bwana Mungu wako; 1.kwa moyo wako wote, 2.kwa akili zako zote na 3.kwa nguvu zako zote. Sehemu ingine Yesu anasema nilipokuwa mgonjwa hamkuja kuniona; nilipokuwa na kiu hamkuninyesha maji; nilipokuwa na njaa hamkunilisha… Mlivyokuwa mnawatendea wale ndugu ndivyo mlinitendea.
Point: ili kumpenda Mungu; kwa moyo wote, kwa akili zote na kwa nguvu zote hatuna budi kufanya hivyo kwa ndugu zetu tunaoishi nao.
Luk10:30-37 tunakuta mfano alioutoa Bwana Yesu; mtu mmoja aliyekuwa akisafiri kutoka Yeriko kwenda Yerusalem aliangukia mikononi mwa wanyang’anyi, vibaka, majambazi… Wakamnyanganya kila kitu hata nguo; walimpiga sana wakamtupa akiwa mahututi karibu kufa.
Alipita kuhani, akamwangalia akampuuza; akafuata mlawi akamwona akampuuza lakini alipita msamaria akamwona akamhurumia. Akamsaidia kwa moyo wake wote, kwa akili zake zote na kwa nguvu sake zote. Msamaria huyo alikuwa na upendo ndani yake; alikuwa na Mungu ndani yake, alikuwa na roho mtakatifu.
Tujitahidi wapendwa kuwa na upendo ndani yetu, kuwa na Mungu ili tuishi katika misingi imara ya wokovu. Mungu awabariki sana.
E-mail: ospau2808@gmail.com
WatsApp: +255 788 574 220

Comments