Mkazi mmoja wa Lusaka nchini Zambia 
ambaye wiki mbili zilizopita alijikuta akipoteza mguu wake mmoja baada 
ya kupata ajali,siku chache kabla ya harusi yake,hatimaye amefanikisha 
azma yake baada ya kufunga ndoa na mchumba wake huyohuyo huku  yeye 
akiwa amelazwa kitandani katika Hospitali moja nchini humo
Suzyo Muzuri mwenye umri wa miaka 28 
amefunga ndoa hiyo  na bi Diniwe Bowa mwenye umri wa miaka 27 katika 
harusi  iliyofanywa chini ya Askofu  Andrew Mwenda  wa kanisa la  Bethel
 Christian Center harusi iliyofanyika ndani ya wodi namba 11 ya 
Hospitali iliyopo ndani ya chuo kikuu  UTH.
Sherehe hiyo ya ndoa imehudhuriwa na ndugu jamaa na wanafamilia wa familia za bwana na bibi harusi ambao walisimama kushuhudia wawili hao waliopendana wakifunga ndoa yao na kuanza maisha mapya kama mume na mke
Hayo ndiyo yaliyojiri huko Lusaka,Nasi 
tunawatakia maisha mema na yenye baraka tele katika ndoa yao maharusi 
hawa ambao wameonesha Upendo kwa Vitendo na sio kwa maneno tuu

Sherehe hiyo ya ndoa imehudhuriwa na ndugu jamaa na wanafamilia wa familia za bwana na bibi harusi ambao walisimama kushuhudia wawili hao waliopendana wakifunga ndoa yao na kuanza maisha mapya kama mume na mke

Credit: Mjap in blog. 

Comments