HUYO MWANZO ALIKUWA NI MUNGU.


Na Mtumishi Peter Mabula.
BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu.
Karibu tujifunze Neno hai la MUNGU wa mbinguni.
Leo tuna ujumbe mzuri sana.

’Hapo mwanzo kulikuwako NENO, naye NENO alikuwako kwa MUNGU, naye NENO alikuwa MUNGU. Huyo MWANZO alikuwako kwa MUNGU. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.-Yohana 1:1-3.’’

-Huyo Mwanzo alikuwepo tangu mwanzo.

-Huyo MWANZO alikuwako kwa MUNGU na tena huyo Mwanzo ni MUNGU.

-Yeye hakuanza maana vile tunavyodhani kwamba vilikuwepo mwanzoni kabla ya mwanadamu kama mbinguni na nchi, huyo Mwanzo ndiye aliyeviumba hivyo.

Wakolosai 1:14-17 ‘’ ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;  naye ni mfano wa MUNGU asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye.  ‘’

-Huyo Mwanzo amekuwapo kabla ya vitu vyote kuwapo.

-Anaitwa Mwanzo kwa sababu vile vyote ambavyo mwanadamu anaviona au kuvijua basi yeye Huyo Mwanzo ndiye aliyeviumba.

-Huwa nasema hivi ‘’Ukitaka MUNGU awe na mwanzo kama vile ambavyo kila kitu kina mwanzo utakosea’’. Ufahamu wa mwanadamu kuna mahali unagota au unafika mwisho. Inabidi tu tufikie mwisho wa ufahamu wa mwanadamu maana hapo hatuwezi kupavuka maana yanayovuka hapo ni ya MUNGU na anayajua MUNGU mwenyewe. Hatuwezi kumjua MUNGU zaidi ya ufahamu wetu wa mwisho kama binadamu. Ndio maana MUNGU anasema Neno hili
 ‘’ BWANA asema hivi, Mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake; bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ananifahamu mimi, na kunijua, ya kuwa mimi ni BWANA, nitendaye wema, na hukumu, na haki, katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo, asema BWANA,-Yeremia 9:23-24’’

-Kumbe sio wote wanaojisifu kwamba wanamjua MUNGU maana kuna wengine wanajisifu wanamjua MUNGU kumbe wala hawamjua na wanaabudu mnyama toka kuzimu(Ufunuo 13:1-9).

-MUNGU wa kweli amejifunua katika neno lake Biblia.

-Yeye MUNGU anasema  kama tutajisifu basi tujisifu tu kwa sababu tunamjua yeye MUNGU pekee na pia tunajua mpango wake wa dunia hii na pia tunajua kwamba yeye MUNGU anataka nini na hicho akitakacho yeye ndio tukishike  na kukiishi maisha yetu yote. Hapo ndio tutajisifu.

Huyo Mwanzo ni MUNGU maana yake hakuna chochote kabla yake maana yake maana yeye ndio huo Mwanzo na huo mwanzo tuujuao sisi wanadamu ni wa viumbe tu alivyoviumba yeye lakini yeye yuko tangu milele yote, hana Mwanzo wala mwisho.

Huyo Mwanzo ni MUNGU na wala hakuanza ila alikuwepo milele yote. Kitabu cha Mika kinadokeza kwamba Huyo Mwanzo alikuja kuishi duniani ili kuwaletea ukombozi wanadamu.

Mika 5:2 ‘’ Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele. ‘’

-Mwanzo akaja duniani ili kuwaokoa wanadamu, akipitia Bethlehemu. Akaacha Mamlaka yake mbinguni ,akaja akiwa hana utukufu hata kama alitenda matukufu mno.

Wafilipi 2:5-11 ‘’ Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya KRISTO YESU; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya MUNGU, naye hakuona kule kuwa sawa na MUNGU kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena MUNGU alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la YESU kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa MUNGU Baba.  ‘’

-Huyo Mwanzo alikuwa ni MUNGU.
-Huyo Mwanzo   hana mwisho wake wa kuishi.

Yohana 1:2-5 ‘’ Huyo mwanzo alikuwako kwa MUNGU. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.  Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza. ‘’

-Watu wengi haiwasumbui kusema YESU ni MUNGU lakini huchanganyikiwa zaidi pale ambapo MUNGU wa Biblia ni mmoja lakini amejifunua katika nafsi tatu.

Watu wengi wa leo wamechanganyikiwa katika hili kama walivyochanganyikiwa mitume ila wakauliza kwa BWANA YESU na kujulishwa ukweli.

Yohana 14:6-9 ‘’ YESU akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa BABA, ila kwa njia ya mimi.
 Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na BABA; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.  Filipo akamwambia, BWANA, utuonyeshe BABA, yatutosha.  YESU akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona BABA; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe BABA?  ‘’


Majibu haya ya BWANA YESU naomba yamsaidie kila rafiki yangu anayesoma ujumbe huu ili aijue kweli hii.

Katika Yohana 10:30  Biblia ya kingeleza inasema hivi ‘’I and my Father are one. ‘’ 
Yaani BABA wa mbunguni na YESU KRISTO ni mmoja. Iliwachanganya Wayahudi  na kwa sababu walikuwepo hapo hapo walijua amekufuru maana amejiita MUNGU, 
Yohana 10:31-33‘’ Basi Wayahudi wakaokota mawe tena ili wampige.
YESU akawajibu, Kazi njema nyingi nimewaonyesha, zitokazo kwa BABA; kwa ajili ya kazi ipi katika hizo mnanipiga kwa mawe?  Wayahudi wakamjibu, Kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa mawe; bali kwa kukufuru, na kwa sababu wewe uliye mwanadamu wajifanya mwenyewe u MUNGU. ‘’

Iliwasumbua sana wayahudi lakini ukweli ndio huo na hakuna mjadala. Kumjua YESU KRISTO ndio kumjua MUNGU wa kweli wa pekee. Wakolosai 2:2b Biblia inasema ‘’ wapate kujua kabisa siri ya MUNGU, yaani, KRISTO;‘’ na Biblia inaendelea kusema

Ufunuo 1:8 '' Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema BWANA Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi. ''

MUNGU BABA ni alfa na Omega na pia MUNGU mwana ni alfa na omega. Unaweza pia kusoma (Ufunuo 22:12-21)
-Huyo mwanzo ni MUNGU Mwenyezi.
-Huyo Mwanzo ni Mwenyezi MUNGU, alikuweko zamani zote, yupo leo na atakuwepo milele yote.

-Wanadamu mara nyingi tukijifunza mwanzo huwa tunaanzia pale ambapo mbinguni na dunia na vilivyomo vilipoumbwa.
-Malaika waliumbwa na huyo Mwanzo.
-Viumbe vyote viliumbwa na huyo Mwanzo.
-Wanadamu waliumbwa na huyo Mwanzo.

Baada ya anguko la Adamu wanadamu  walianza kuishi katika makusudi yao na sio Makusudi ya MUNGU muumbaji wao.

Kwa Neema kuu Mwenyezi MUNGU akaja kutukomboa kwa Damu yake Mwenyewe.

Matendo 20:28 ‘’ Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo ROHO MTAKATIFU amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake MUNGU, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.‘’

-MUNGU alilinunua Kundi lake  kwa damu yake mwenyewe, kundi hilo ni wateule wa KRISTO wote wanaoiishi kweli ya MUNGU kupitia Wokovu wake.

-Kupitia Huyo Mwanzo tunamjua MUNGU wa kweli.
-Mwanzo ndiye MUNGU na Ibarahimu, Isaka na Yakobo.


Wanadamu wengi wanamkataa leo lakini wanasahau kwamba hakuna mbingu nyingine nje na yeye maana yeye ndiye aliyeumba hizo mbingu.

1 Yohana 5:11-13 ‘’ Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba MUNGU alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe.  Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa MUNGU hana huo uzima.
Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue ya kuwa mna uzima wa milele, ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa MUNGU.‘’



Wateule wake leo tunamtazamia MUNGU mkuu, maana alikuwepo milele yote.


Tito 2:13-14 ‘’ tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa KRISTO YESU, MUNGU mkuu na Mwokozi wetu;  ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema. '’

-Hata malaika watakatifu wanaitwa malaika wake. Na siku ya mwisho atakuja na malaika zake


Mwanzo huyu ametupa sisi ROHO wake, Tunatakiwa tumpokee MUNGU na tuanze kuishi katika kusudi lake. Asiye na ROHO wake huyo sio wake, 
Warumi 8:9 ‘’  Lakini ikiwa ROHO  wa MUNGU anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na ROHO wa KRISTO, huyo si wake. ‘’


-Ndugu zangu ukijitenga na MUNGU wa Biblia maana yake wewe umemchagua shetani.


-BWANA Mungu anakupenda sana na hataki uendo jehanamu.

-Maamuzi ya kwenda au kutokwenda jehanamu uko nayo wewe.

-Amua leo kumpokea na utafanya vyema


Warumi 10:9-10,13 ‘’ Kwa sababu, ukimkiri YESU kwa kinywa chako ya kuwa ni BWANA, na kuamini moyoni mwako ya kuwa MUNGU alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika. kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la BWANA ataokoka. ‘’


-Ukimpokea atakupa uzima sasa na uzima wa milele kama tu ukibaki katika pendo lake.

-MUNGU wetu ni ngome imara, tukikimbilia leo tunakaa salama
Mithali 18:10 '' Jina la BWANA ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama. ''

-Hakika ili tuiepuke jehanamu ni lazima tuwe upande wa MUNGU mwenye nguvu.

Kimbilia leo ndugu ili ukae salama.
-MUNGU wetu ni Mkuu sana
-Jina lake ni Kuu sana.
-Uweza wake ni Mkuu sana.
-Matendo yake ni Makuu sana.

SIKU YA MWISHO ATAKUJA KUMLIPA KILA MWANADAMU SAWASAWA NA MATENDO YAKE YA SASA AKIWA DUNIANI.
Ufunuo  22:12-13 " Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo. Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho. ''

Ukitubu leo yeye anakusamehe na anasema dhambi zako hatazikumbuka tena.

Kimbilia ili uwe salama.
Yeremia 10:10-13 '' Bali BWANA ndiye MUNGU wa kweli; Ndiye MUNGU aliye hai, Mfalme wa milele; Mbele za ghadhabu yake nchi yatetemeka, Wala mataifa hawawezi kustahimili hasira yake.
 Mtawaambia hivi, Miungu hiyo isiyofanya mbingu na nchi, hiyo itaangamia katika nchi, nayo itatoweka chini ya mbingu. Ameiumba dunia kwa uweza wake, Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake, Na kwa ufahamu wake amezitandika mbingu. Atoapo sauti yake, pana mshindo wa maji mbinguni, Naye hupandisha mawingu toka ncha za nchi; Huifanyia mvua umeme, Huutoa upepo katika hazina zake.'' 
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA. MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.

Comments