BWANA YESU
atukuzwe ndugu yangu.
Karibu
tujifunze Neno la MUNGU la kutusaidia kutambua na kuchukua maamuzi mazuri.
Yuda 1:4 ‘’ Kwa
maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu
hii, makafiri, wabadilio neema ya MUNGU wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye
aliye peke yake Mola, na BWANA wetu YESU KRISTO. ‘’
-Mara nyingi
shetani hutaka kuweka la kwake katika kila jambo jema. Japokuwa vitu orginal
vipo lakini shetani hupenda kuweka vitu
feki mahali pa vitu orginal ili wanadamu wakikaa vibaya wanaweza kujikuta hata
vitu orginal hawatavijua tena kama ni orginal na watajikuta wakidhani kwamba
vile orginal ndio feki na vile feki ndio orginal.
-Shetani ni
wa vitu feki tu.
Injili ni
habari njema za ufalme wa MUNGU ambao pekee unapatikana katika KRISTO YESU.
Injili ya KRISTO ni gari ya kuwabeba
watu tayari wa kuwapeleka uzima wa milele. Lakini shetani ana injili yake feki
ambayo lengo lake ni kuwapotosha wanadamu na hadi kuna wanadamu hudhani kwamba
injili feki ndio mpango wa MUNGU wakati si kweli. Biblia iko wazi kabisa
kwamba kuna watu wanaotumika vibaya, hawa wako upande wa
shetani hata kama wataitwa wahubiri, ni mawakala wa shetani maana wana mikataba
na shetani, ni makafiri waibadilio kweli
ya MUNGU kuwa ufisadi.
Wagalatia
2:4-5 ‘’ Bali kwa ajili ya ndugu za uongo walioingizwa kwa siri; ambao
waliingia kwa siri ili kuupeleleza uhuru wetu tulio nao katika KRISTO YESU, ili
watutie utumwani; ambao
hata saa moja hatukujitia chini yao, ili kwamba kweli ya Injili ikae pamoja
nanyi. ‘’
-Kwa sababu
ya kuingia kwao kwa siri katika injili wamepelekea baadhi ya watu kutokuwatambua. Wameweka baadhi ya
miongozo yao na kuwalazimisha wanadamu
waifuate hiyo badala ya kufuata Biblia takatifu. Wabaya hawa
wamewahamisha watu kutoka kuitegemea Biblia
na sasa wanategemea tu sheria za kanisa.
Warumi 15:18
‘’ Maana sitathubutu kutaja neno asilolitenda KRISTO kwa kazi yangu, Mataifa
wapate kutii, kwa neno au kwa tendo, ‘’
Kazi ya watu
hawawaongo kulingana na Yuda 1:4 ni;
1. WANAIBADILI
NEEMA YA MUNGU KUWA UFISADI.
-Wanaondoa watu kwenye kusudi la MUNGU la uzima wa milele.
-Hawaihubiri injili ya kweli.
-Wanaunganisha ukweli na uongo pamoja na kuwakosesha maelfu ya waumini.
-Wanahubiri kwa kulaghai ili wapate pesa.
-Wanahalalisha yaliyo machukizo kwa MUNGU.
=Baadhi ya waongo hawa waliojiingiza kwa siri katika injili ni hawa;
a. Wanaruhusu ushoga na kufungisha
ndoa hizo za mashoga katika makanisa yao.
b. Wanaabudu sanamu badala ya
Kumwabudu MUNGU wa mbinguni.
c. Wanadanganya watu kwa
kufundisha kwamba hakuna jehanamu.
d. Wanafundisha watu kwamba pombe
ni halali tu.
e. Wanamkataa ROHO MTAKATIFU wala hawamhitaji katika makanisa au huduma
zao.
f. Wanakataa wokovu na wanakataza watu kuokoka.
g. Wanaibadili Biblia kwa lengo la
kunufaisha uongo wao walioingia mkataba na shetani.
h. Wanairekebisha Biblia ili Biblia iwafuate wao badala ya wao kuifuata
Biblia.
2 Petro 2:1-3 ‘’ Lakini kuliondokea manabii wa uongo katika wale watu,
kama vile kwenu kutakavyokuwako waalimu wa uongo, watakaoingiza kwa werevu
uzushi wa kupoteza, wakimkana hata BWANA aliyewanunua, wakijiletea uharibifu
usiokawia. Na wengi watafuata ufisadi wao; na kwa hao njia ya kweli itatukanwa.
Na katika kutamani watajipatia faida kwenu kwa maneno yaliyotungwa; ambao
hukumu yao tangu zamani haikawii, wala uvunjifu wao hausinzii. ‘’
2. HUMKANA MUNGU BABA NA BWANA
YESU.
-Wanamkataa YESU KRISTO japokuwa wanaitwa wakristo maana wameingia
mkataba na shetani ili kupeleka watu jehanamu.
-Wanamkata MUNGU kwa sababu ya kufundisha kwao uongo.
-Hawahubiri toba bali mambo ya dunia tu.
-Wanamkana MUNGU kwa sababu wanaipenda dunia na anasa zake kuliko
kumpenda BWANA MUNGU.
-Wanamkana JEHOVAH MUNGU wa kweli kwa wao kuvaa mavazi ya kikahaba na
kufuata elements za majini.
-Wanamkana MUNGU kwa wao kukataa kuwa chini yake MUNGU muumbaji wao.
-Wanamkana MUNGU kwa wao kujipa vyeo vya KRISTO jambo ambalo ni baya sana
maana kuna wengine hata hudai kwamba wao ndio Kristo wa pili waliotumwa na
MUNGU kukamilisha kazi ya ukombozi maana BWANA YESU KRISTO alishindwa kuimaliza
kumbe ni uongo tu wa shetani ili kuhakikisha wanadamu hawafiki uzima wa milele.
-Wanamkana MUNGU BABA kwa wao kuabudu wafu.
-Wanamkana BWANA mbele za ulimwengu.
-Wanamkana BWANA YESU kwa wao kukataa kazi yake.
-Wanamkana MUNGU kwa wao kusema wametumwa na yeye kumbe ni uongo wao tu
wa kutaka kupeleka wanadamu jehanamu.
-Husema kwamba MUNGU ni wa huruma sana hivyo hawezi kuwaangamiza
wanadamu. Ndugu zangu, hatuwezi kumzidi MUNGU huruma ambaye ndiye aliyeleta
ukombozi wetu kupitia YESU KRISTO, Haitakuwepo huruma kwa mwanadamu
atakayemkataa YESU na bila kutubu hadi kifo chake maana ndivyo maandiko
yasemavyo. MUNGU ana huruma sana lakini sodoma na gomora waliangamia wote maana
walikataa maonyo ya MUNGU, Wakati wa Nuhu MUNGU aliangamiza ulimwengu wote kwa
sababu ya wanadamu kujitenga na MUNGU muumba wao. Na hata sasa mwisho ukifika
ataangamiza waasi wote maana wameikataa kweli yake ambayo ni KRISTO.
-Wanamkana MUNGU kwa wao kuwabebesha wanadamu mizigo mizito ambayo mizigo
hiyo wala haitokani na MUNGU wala Neno lake.
1 Yohana 2:22-23 ‘’ Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa YESU ni KRISTO? Huyo ndiye
mpinga Kristo, yeye amkanaye BABA na MWANA. Kila amkanaye MWANA, hanaye
BABA; amkiriye MWANA anaye BABA pia. ‘’
Ndugu yangu, jitenge na hao haijalilishi wapo tangu miaka 1800 iliyopita,
jitenge na waongo hao haijalishi wapo tangu miaka 200 iliyopita.
-Ukiona injili yeyote inamkataa BWANA YESU kama Mwokozi pekee wa wanadamu
wote tambua kwamba injili hiyo haikutoka kwa MUNGU mbinguni.
-Ukiona kanisa au dhehebu wanaoukataa uungu wa BWANA YESU hao jitenge
nao.
-Ukiona dhehebu au kanisa ambalo mwanzilishi wake wanampa heshima ya
KRISTO hao jitenge nao.
-Ukiona kanisa wanaabudu wafu hao tambua kabisa wanahitaji kusaidiwa wao,
jitenge nao.
-Ukiona kanisa wana Biblia yao peke yao hao wakimbie tena ni matapeli
maana wameirekebisha Biblia ili Biblia iwafuate wao badala ya wao kuifuata Biblia. Kuna waongo
hata Biblia kwao hawaiti Biblia bali wanaita ‘’kitabu cha Bwana’’ kumbe huyo
Bwana anayeitwa kwamba kitabu cha Bwana ndiye mwanzilishi wa dhehebu hilo na si
BWANA yaani MUNGU.
-Kuna madhehebu hawataki kusikia uungu wa YESU japokuwa ukweli ni kwamba kuna maandiko mengi sana ambayo yanamtambua
YESU kama ni MUNGU lakini wao wameyabadili maandiko hayo katika Biblia zao.
Mfano kuna makanisa andiko la Yohana 1:1
ambalo linamtaja BWANA YESU kama MUNGU mkuu, wao badala ya kuaandika ‘’Mungu’’
Kama ilivyo katika Biblia zote wao kwenye Biblia yao wameandika ‘’mungu’’
ambayo kibiblia mungu maana yake ni shetani. Inawasumbua kuandika kwamba YESU
KRISTO ni MUNGU na wao wanaandika katika Biblia yao hiyo ya kipekeyao kwamba
YESU ni mungu, hii ni matokeo ya mwanzilishi wa dhehebu hilo kuwa wakala wa
shetani. Hao ni wa kuwakimbia. Katika
Biblia takatifu ukiona Neno ‘’mungu’’ ya kuanza na herufi ya kwanza ndogo hiyo
inamaanisha shetani mfano
2 Kor 4:3-4 ‘’ Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao
wanaopotea; ambao
ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru
ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu. ‘’
-Kupitia andiko hilo tunamuona kwamba shetani ni mungu ikianza na herufi
ndogo lakini pia andiko hilo hilo linamtaja MUNGU BABA wa mbinguni, hivyo hawa
kitendo chao cha Yohana 1:1 kuibadili ni taarifa tu kwako kwamba wao ni
mawakala wa shetani.
Ukiwauliza kwanini YESU kwenye andiko hilo wamemwita mungu badala ya
Mungu wanakosa jibu. Hawa ni wapinga KRISTO waliojipenyeza kanisani na
kupotosha maelfu ya watu ndio maana hadi Biblia wameibadili.
BWANA YESU mwenyewe anawataja waongo hawa.
Mathayo 24:11 ‘’ Na
manabii wengi wa uongo watatokea, na kudanganya wengi. ‘’
Ndugu yangu, usijitenge na uzima wa milele kwa kushika na kufuata
mafundisho yaliyo kinyume na Biblia ya kweli.
-Ndugu achana na mafundisho ya mashetani ya wapinga Kristo.
-Ndugu yangu achana na mafundisho yanayotokana na roho zidanganyazo.
1 Timotheo 4:1-2 ‘’ Basi ROHO anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga
na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; kwa unafiki wa
watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe; ‘’
-Waongo hawa hufundisha kwamba dhehebu lao tu ndio watakaoingia uzima wa
milele maana yake ukiwa nje ya dhehebu hilo huendi uzima wa milele kitu ambacho
ni uongo mkubwa. Watu hawaingii mbinguni kwa tiketi ya dhehebu bali wokovu
uliotimia katika utakatifu.
Ndugu yangu injili ya kweli ipo na inahubiriwa, ifuate hiyo katika
makanisa ya kweli ya kiroho.
-injili ya kweli humhubiri KRISTO anayeokoa.
Kumb 13:4 ‘’ Tembeeni kwa kumfuata
BWANA, MUNGU wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi
mtumikieni na kushikamana naye. ‘’
-Ndugu naomba uutendee kazi ujumbe huu.
Namshukuru ROHO MTAKATIFU kwa kunipa ujumbe huu leo kwa ajili ya ndugu
zangu wote watakaosoma na kuutendea kazi.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula
0714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili. MUNGU Akubariki.
N.B. (Kwa wale wanaobadilisha masomo yangu sehemu za mwisho na kujiandika wao na kuweka namba zao za simu na kuomba pesa za kukuza huduma zao kupitia ujumbe wangu,hiyo ni mbaya. share somo, weka katika blog yako ila usibadilishe chochote na pia fundisha watu kupitia ujumbe huu, print na usambaze kokote kwa njia yeyote maana hapo utakuwa unahubiri injili. mmepewa bure toeni bure. binafsi sijawahi kuandika masomo ili nipate pesa hata kama nina uhitaji wa pesa. ubarikiwe)
Comments