KUVUNJA NA KUKATAA MAGONJWA YANAYOTOKEA KWA WAKATI MAALUMU


Na Mchungaji Mkama, Ufufuo na uzima Kigoma

Kuna watu wanaugua kwa wakati maalumu, yaani ikifika jioni anaugua, huo ni wakati maalamu uliopangwa ili ukifika augue,Lakini kuna mtu mwingine mwisho wa mwezi ukifika (mshahara) magonjwa yanatokea, kuna mapepo yamejiiandaa kusababisha magonjwa kwa wakati huo ili atumie mshahara wake kutibia magonjwa na sio kufanya mabo ya maana; mwingine akitaka tu kwenda shule anaugua , hii ni kwasababu wachawi wameweka wakati huu kuwa maalumu kwa ajiili ya mtu ili augue,
Wachawi wanatumia photocopy kutoka kwa Mungu, Mungu hasahau akiamua kufanya kitu kwa wakati Fulani lazima akifanye, alimuahidi SARA kupata mtoto kwa wakati Fulani na wakati huo ulipofika SARA alipata mtoto, mapepo pia hayasahau, kama watu wanakaa vikao na kuweka wakati maalumu kwa kutumia miungu, jua, mwezi ili muda Fulani ukifika augue ama wanaweza kupanga baada ya miaka kumi na tano augue, muda huo ukifika unaugua maana mapepo hayasahau. Au wanaweza kuyatuma mapepo baada ya kuanza masomo asifauru, basi muda huo ukifika hatafauru.
Kuna mwingine akichukua jembe kwenda kulima anaugua, au akipanga kwenda kazini anaugua,leo tunakwenda kuvunja na kukataa magonjwa yaliyowekwa kwaajili ya wakati maaalum.
Kumbukumbu 4:15-19
Wachawi wanapanga muda maalumu wakumtesa mtu, mwingine saa 2 ni muda wake maalumu wa kuugua kwakuwa kuna watu walikaa vikao nakuuweka wakati huo. Kuna dua ikisomwa mchana kila ifikapo mchana unauguua. Na hapo watu hudhani ni magonjwa ya vipindi kumbe ni mapepo yamewekwa ili kuleta magonjwa wakati huo.
Kuna dua zingine hasomwa siku saba, kuna zingine haziruhusiwi kufanya ukiwa umekaa. Na anapofanya haya anayafanya kwa wakati maalumu.Anaweza kuchukua yai lililooza kwamujibu wa madhabahu yake, nakusema kwamba yai hili linavyochukiwa na biashara yake ichukiwe namna hii. Kwakuwa amekwenda kusujudu kwenye miungu na ikampa nguvu yakuachilia balaa na mikosi, sasa hapo bila Damu ya Yesu huwezi kutoka salama.
Yeremia 8:2
Kuna wakati ukipata hela unaugua na hela zikiisha tu unapona. Hii ni kwasababu wataalamu wamekusoma kwa kupitia nyota,mwezi na majeshi ya mbinguni. Kumbe kuna magonjwa yanayotusumbua leo na kutuhangaisha leo kwakuwa kuna watu walipanga katika madhabahu zao ili muda Fulani ukifika uhangaike.
Kuna wengine magonjwa au matatizo ni ya sehemu maalumu, utakapoingia ofisi yoyote kufanya kazi uugue kwakuwa kuna pepo ambao wameachiliwa ili ufikapo mahali Fulani unaugua, na kwakuthibitisha hili ukijaribu kuhama sehemu ya kazi unafanikiwa. Je ni eneo gani ambalo ukikaa matatizo au magonjwa yanakupata. Ukiona hivo ujue pepo wamewekwa ili ukienda mahali Fulani usifanikiwe.Wakati mwingine eneo/sehemu maalumu inaweza kuwekwa kwaajili ya kukutesa.
2 wafalme 17:16
Unaweza kusema unaumwa, hakuna maagano ambayo yanaweza kutolewa bila sadaka kuwepo mahali hapo
Kutoka 13:5__Mungu anawapangia waisrael kuwa muda huu wataushika utumishi huu. Hivo hivo na upande washetani wanatumia photocopy kutoka kwa Mungu. Muda Fulani wanauweka maalumu kwaajili yakufanya kitu au jambo
Kutoka 13:1 __Mungu aliwaambia wamtakasiye yeye wazao wa kwanza wote, wa watu na wawanyama, hivyohivyo hata shetani anawataka wazaliwa wa kwanza ili kupitisha mambo yake.utashangaa wazaliwa wakwanza walio wengi hawana muelekeo au wanauguaugua.
Kutoka 20:4


 

Comments