|
||||||||
1.TUNAJARIBIWA
KWASABABU YA KIBURI
|
||||||||
Dhambi zote
mama yake ni kiburi ambapo kiburi hicho chaweza kuwa ni
kiburi cha elimu, pesa, mali au majivuno tu.
Watu wengi hushindwa kufika makanisani wakisingizia kuwa
wana majaribu ambayo yanawasumbua katika maisha yao na
husahau kuwa Mungu anawataka watu ili awashushe mizigo
yao.
|
||||||||
Alitolea
mfano kuwa watu wengine hufikiri kulemewa na baadhi ya
dhambi kama uzinzi ni kuwa na mizigo kumbe ni
kuendekeza tamaa za mwili.
|
||||||||
Nje ya dhambi wengine hajidanganya kuwa hawamuhitaji
Mungu na hii hutokana na kuwa na mahitaji yao yote ya
kimwili kwa wakati huo au kuwa na mali nyingi pasipo
matatizo. Kumbe wanajidanganya kwani Mungu huweza
kuondosha mali hizo kwa dakika chache tu wakabaki hawana
kitu hivyo ni nzuri kuacha kiburi na kumuheshimu Mungu
katika kila hali.
|
||||||||
2.
TUNAJARIBIWA KWASABABU YA UCHUNGU
|
||||||||
Waefeso 4:31,
‘Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na
matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya’.
|
||||||||
Uchungu pia ni njia moja wapo ya kufanya watu
wajaribiwe. Mfano ; Katika moja ya sehemu
zangu nilizokuwa nikifanya huduma nilikutana na dada
mmoja ambaye alikuwa na ujauzito wa miezi kumi na miwili
ambapo alikuwa hapati uchungu wa kujifungua. Dada huyo
alinifuata na kuniomba nimuombee ili apate uchungu na
azae lakini Roho wa Mungu alimuonesha kuwa kuna tatizo
katika familia yake.
|
||||||||
Ndipo
nilipomwambia aende kumwita mama yake mzazi ambapo baada
ya mama huyo kufika aliniambia kuwa binti yake huyo
alimtukana matusi mazito na ndipo nilipomwambia yule
binti amuombe maama yake msamaha na baada ya kufanya
hivyo ghafla alipata uchungu na kukimbizwa hospitali na
alifanikiwa kujifungua mtoto wa kiume.
|
||||||||
Wakati
mwingine unaweza kuwa na uchungu juu ya ndugu, jamaa na
marafiki kutokana na mateso mbalimbali ambayo
wamekutendea lakini unapaswa kutoa uchungu huo ili
kuuachilia moyo kwa BWANA ndipo utakapompa nafasi ya
kukubariki. Lakini hali hiyo hutokana na kuweka mambo
mengi ya kuumiza moyoni hivyo kufanya kushindwa
kuachilia na kusamehe.
|
||||||||
Mara nyingi
wanawake wamekuwa ni watu wa kuhifadhi mambo katika
mioyo yao na wakati mwingine kuyafanya mambo kuwa
makubwa hata kama ni madogo.
|
||||||||
3.
TUNAJARIBIWA ILI TUJIFUNZE KUMTEGEMEA MUNGU KWA ASILIMIA
MIA MOJA
|
||||||||
Unajua
wakati mwingine Mungu hutujaribu ili tujifunze
kumtegemea, nakumbuka waakti mke wangu ni mjamzito na
alipofikisha muda wa kujifungua sikuwa na pesa hata
kidogo katika akiba yangu, hivyo ilipofika wakati
anaumwa uchungu nikuwa na kiasi cha shilingi mia na
hamsini (150) katika akiba yangu , pesa ambayo
nisingeweza kumhudumia kwa kitu chochote. Ndipo
nilipoamua kumzalisha mwenyewe japo kuwa sikuwa na ujuzi
wowote wa ukunga.
|
||||||||
|
||||||||
Mfano;
Kuna dada
mmoja alikuwa mtumishi mzuri tu kanisani lakini alikuwa
na roho ya ubinafsi, alikuwa anavuna mahindi mengi sana
lakini hakuwa kumbuka watu hata kidogo. Kutokana na hali
hiyo Mungu aliruhusu jaribu ambapo wakati yeye yupo
ibadani, nyumbani kwake walivamia majambazi ambapo
walikusanya kila kitu katika nyumba yake yote hiyo
ilikuwa ni katika kuhakikisha anamrekebisha tabia yake’.
|
||||||||
Unapaswa
kufurahia mafanikio ya watu wengine ndipo Mungu atakapo
shughulika na maisha yako pia wivu huchangia kwa kiasi
kikubwa kuharibu maisha ya kiroho.
|
||||||||
6.TUNAJARIBIWA
ILI TUWE NA HURUMA
|
||||||||
‘Ambaye
hakulala na njaa hawezi kujua ni sehemu gani chakula
kipo’.Hivyo
usipopitia matatizo huwezi kujua ni kwa namna gani
unaweza kuwafariji wanaopitia matatizo.
|
||||||||
2wakoritho1:3-5,
‘Na
ahimidiwe Mungu bab wa BWANA wetu Yesu Kristo, Baba wa
rehema, Mungu wa faraja, atufarijie katika dhiki zetu
zote ili nasi tunapate kuwafariji wale walio katika
dhiki ya namna zote, kwa faraja hizo tunazofarijiwa na
Mungu. Kwa kuwa kama vile mateso ya Kristo yanavyozidi
kwetu, vivyo hivyo faraja yetu inazidi kwa njia ya
Kristo’.
|
||||||||
Bila
matatizo hatuwezi kuoneana huruma.
|
||||||||
7.TUNAJARIBIWA
ILI TUTHIBITISHE IMANI YETU.
|
||||||||
Wakati
mwingine watu hupita katika wakati mgumu ili kuweza
kupimwa imani zao kwa Mungu.
|
||||||||
Mfano;
Wakati naanzisha huduma yangu kijijini nilikuwa na
waumini wanne tu yaani mimi na mke wangu, na mzee wa
kanisa na na mke wake, jambo la kusikitisha ilikuwa ni
katika kipindi cha sadaka ambapo wote tulikuwa hatuna
kitu basi ilikuwa kama mchezo wa kuigiza.
|
||||||||
|
||||||||
Pamoja na
maombezi hayo wapo watu wengine waliompokea BWANA YESU
kuwa mwokozi wa maisha yao kwa kuongozwa sala ya toba.
|
||||||||
|
||||||||
Comments