SHAMBULIO LA BOMU KANISANI LAUA WATU 9


Mmoja wa waumini akiwa katika huzuni kubwa.
Polisi katika jimbo la South Carolina nchini Marekani wamesema kuwa mtu mmoja aliyejihami kwa bunduki amewapiga risasi na kuwaua watu tisa ndani ya kanisa la kimethodist.

Polisi wa eneo hilo la Charleston wameelezea kuwa kwa sasa wanamtafuta mshukiwa huyo anayeaminiwa kuwa kijana wa kizungu katika miaka ya ishirini.


Shambulio hilo limefanyika ndani ya kanisa la Emmanuel African Methodist Church, kanisa linaloaminiwa kuwa la zamani zaidi la kiafrika nchini Marekani
Polisi wamesema kuwa shambulio hili ni la chuki ya rangi ya ngozi. 

Waumini wakiomba kwa umoja nje ya eneo la tukio.
Polisi wakiwa katika eneo la tukio.
Polisi wakiweka uzio kwenye eneo la tukio.

Comments