SILAHA ILIYOANDALIWA KUNIANGAMIZA

Na Pastor Bryson Lema, Ufufuo na uzima Morogoro.
Utangulizi:Tunaposema silaha,  wengi wetu wanawaza sime, bunduki, mishale n.k. Mwindaji anapokuja kwako, huja akiwa na silaha. Imani yake mwindaji ni kuwa,  kwa silaha aliyoibeba,  wewe hutapita. Hata hivyo, Mungu  wetu naye ameandaa silaha. Tatizo kubwa hapa ni kuwa, silaha ya Mungu haionekani, kwa sababu Mungu wetu hubadilisha kitu kulingana na matumizi.  Mungu akimaua kugeuka sime,anafanya hivyo.

AMOSI 3:5..[Je! Ndege ataanguka mtegoni juu ya nchi, mahali asipotegewa tanzi? Mtego utafyatuka juu ya nchi, bila kunasa kitu cho chote?]…. Hii ina maana kuwa, umuonapo ndege kanaswa katika mtego, ujue kuna aliyeutega. Kila kitu na mtego wake, na kila silaha na mtu wake. Mtego wa ndege haumasni swala, na mtego wa swala haumnasi nyani.
Katika maisha ya kawaida, ipo mitego na pia wapo wawindaji.  Katika Biblia, shetani anaonekana akizuia Ibrahimu asipate uzao kupitia Sarah, kwa kuwa alishajua kupitia uzao wa Ibrahimu Baraka za Mungu zitafuatana na uzao wake. Shetani alitengeneza silaha za kumzuia Ibrahimu kupata motto, bila yeye na mkewe kujua. Mwishowe, baada ya  kukata tama kwa muda mrefu, hatimaye alipata mtotoo aitwae Isaka. Hata hivyo Isaka naye alipitia kipindi kigumu kama hiki cha Ibrahimu, kwa sababu tumbo la mkewe nalo lilifungwa asizae.
Hata uhai ulio nao ni sehemu ya miujiza.  Kumbuka kuwa,  Bwana amekupitisha katika  nyakati usizozijua na kukuepusha na mitego mingi  sana ya wawindaji. Kila jambo ulionalo maishani mwako lina sababu yake. Kwa kadiri unavyopiga hatua za maisha yako,  ujue kuna ………….
Kupitia Isaka, shetani aliwachonganisha Yakobo na Esau. Kupitia Yakobo, shetani alisababisha asimuoe Raheli kwa sababu alishaona ndani  ya tumbo la Raheli angepatikana Yusufu, yaani mkombozi wa wana wa Israeli, atakayewaokoa wasife kwa njaa. Hata baada ya Yusufu kuzaliwa,  shetani alitengeneza mipango mibaya ili Yusufu asifikie ndoto zake. Yusufu alitengenezewa mipango mibaya, pale ndugu zake walipomuuza kwa wafanyabiashara wa Kimisri. Kumbuka lengo  la shetani  siyo Yusufu auzwe Misri bali auae na afe. Hata Yusufu alipokuwa Misri, bado shetani aliendelea kuandamwa na shetani kiasi kwamba alitupwa gerezani, na hapo ikawa ndio mwisho  wa ndoto zake.

Yusufu akiwa gerezani, ndiposa Farao akota ndoto ambayo haikupata mtafsiri bali kwa kupitia kwa Yusufu peke yake. Yusufu alipotoka gerezani alienda moja kwa moja kuwa mtawala wa nchi ya Misri. Bwana atafungua mlango kwako

Baada ya Yusufu kuimaliza kazi yake ya ukombozi, alilala na baba zake. Mwanzoni mwa Kitabu cha Kutoka, habari za Mfalme mpya wa Misri asiyemjua Yusufu  zinaelezwa. Kila  vita husimama kwenye  kila hatua. Wazalishaji wa Kimisri wanaelekezwa wasiachie Waisrael kujifungua salama, na ikitokea hivyo, watoto  wa kiume wote wauae‼ kumbe aliyekuwa anawindwa hapa ni Musa,  ili   Israeli wasipate mtu wa kuwaongoza watoke utumwani. Hata wazazi wa Musa nao walishindwa jinsi  ya kumlinda, na kuazimia kumweka kando ya mto  na papo hapo Bwana akatengeneza njia ya kumuokoa. Kumbe basi, wanaddamu hufika mwisho na wakawa hawawezi.  Lakini ugumu wa wanadamu siyo ugumu wa Mungu Baba.
Usikate tama. Yamkini upo mahali ambapo madaktari wamekuambia ugonjwa ulio  nao hauna tiba,  lakini Bwana Yesu yupo kwa ajili ya shida yako, naye atafanya safina katika mito ya Misri. Kumbuka mwisho wa wanadamu ni  mwanzo wa Mungu. Katikati ya maadui, Musa alikuzwa na kukua. Musa alikula mbele ya Farao, na  kukulia ndani ya nyumba ya Farao. Mbinguni Mungu alikuwa akijua huyu ndiyo mbabbe wa Farao.  Musa akakua katikati ya adui zake. Daudi akasema, “waandaa meza mbele zangu,  machoni pa watesi wangu”. Ambaco Wamisiri hawakukijua ni kuwa, Musa ni kutoka juu na yupo kwa kazi maalumu. Kuku ni kuku,hawezi kuwa tai hata siku moja.

 

Comments