UKWELI WA LEO NI "KUOKOKA NI HAPA HAPA DUNIANI"


Fuatana Nami Katika Hili Ili Ujue Ukweli Wa NENO "KUOKOKA"
Watu Wanadanganywa Eti Hakuna Kuokoka, Jambo Ambalo Wanapotosha.

YEHOVA/BWANA aliwajulisha mapema Watumishi Wake Kuwa Watu WATAOKOKA.

YOELI 2:32 Na Itakuwa Ya Kwamba Mtu Awaye Yote Atakayeliita Jina La BWANA ataponywa; kwa kuwa katika mlima Sayuni na Katika Mlima Yerusalemu Watakuwako Watu Watakaookoka, Kama BWANA alivyosema; na katika mabaki, hao awaitao BWANA.

Kuokoka Katika Sayuni Na Yerusalemu, Hapo Duniani.
OBADIA 1:17 Bali Katika Mlima Sayuni Watakuwako Wenye Kuokoka, Nao Utakuwa Mtakatifu; Na Nyumba Ya Yakobo Watamiliki Milki Zao.

Hapa Panataja Kuokoka, Hapa Hapa Duniani.
YESU AKATAJA KUOKOKA TENA, MAANA ALIKUJA KUOKOA.

MATHAYO 18:11 [Kwa maana Mwana Wa Adamu Alikuja Kukiokoa Kilichopotea]

Kilichookoka Ni Mwanadamu Hapa Hapa Duniani.
LUKA 19:10 Kwa Kuwa Mwana Wa Adamu Alikuja Kutafuta Na Kuokoa Kile Kilichopotea.

Kilichookaka Ni MWANADAMU na si kingine.

YOHANA 5:34 Lakini Mimi Siupokei Ushuhuda Kwa Wanadamu; Walakini Ninasema Haya Ili Ninyi Mpate Kuokoka.
Yesu Anasema Watu Waokoke.

MATENDO 2:21,47
21 Na Itakuwa Kila Atakayeliitia Jina La Bwana Ataokolewa.
47 Wakimsifu Mungu, Na Kuwapendeza Watu Wote. Bwana Akalizisha Kanisa Kila Siku Kwa Wale Waliokuwa Wakiokolewa.
Hapa Watu Walikuwa Wanaokoka/wanaokolewa Hapa Hapa Duniani.

Wewe Unaokoka Kisha Ukifariki Unapewa Ujira Wako Tu.
NDUGU YANGU KWA HAYA MACHACHE Nadhani Umeelewa Kuwa KUOKOKA NI HAPA HAPA DUNIANI, na ukifa ni Hukumu

Waebrania 9:27 Na Kama Vile Watu Wanavyowekewa Kufa Mara Moja, Na Baada Ya Kufa Hukumu.

Baada Ya Kufa Ni Hukumu Na Si KUOKOKA.
OKOKA SASA ili Hukumu Isikuangamize.
KUOKOKA NI HAPA HAPA DUNIANI, MBINGUNI NI UJIRA au ZAWADI KWA MEMA ULIYOYATENDA
MUNGU akubariki.
By Albert Wilson

Comments