Siku ya jana kulifanya Tamasha
maalumu la kusaidia waimbaji wadogo/wanao chupukia wakishirikiana na KP
Tanzania,Bbn Production pamoja na Umoja Production. Lengo la Tamasha
hili ni kumsifu na kumwabudu Mungu pia kuwasapoti waimbaji wapya
wanaochipukia na kukosa sapoti katika huduma zao. Vilevile kufanya
biashara ya muziki wao katika kuutangaza kimataifa,kuwa na studio za
audio na video za kisasa…kwahiyo mwimbaji atakayekuwa kwenye umoja huu
kwa kujiunga kwa kiingilio cha Tsh 500000 tu atapata huduma za kurecordi
free audio,video na kazi yake kusambazwa pia atapata Bima ya afya kwa
mwaka mzima. Tamasha hili lilifanyika Urafiki Social Hall likiwa chini
ya Erick Brighton.
Comments