KUMJUA MUNGU

Na:     BRYSON LEMA (RP)        &
Dr. GODSON I. ZACHARIA (SNP)
Utangulizi: Imeandikwakatika 2KORINTHO 2:14….[Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa kazi yetu.]…Unaweza kumfahamu mtu lakini papo hapo usimjue huyo mtu. Kuna tofauti kubwa sana kati ya kumjua mtu na kumfahamu mtu. Kumjua mtu ni zaidi ya kumfahamu mtu husika.
Paulo aliwahi kuwauliza watu katika MATENDO  17:23, kama ilivyoandikwa ..[Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua. ]… Pengine hata wewe umewahi kujiuliza kwa nini hawa watu walifanya hivyo kwa kuyaandika maneno hayo?. Musa na wana wa Israeli walitofautiana katika kumjua na kumfahamu Mungu. Wakati wana wa Israeli walimfahamu  Mungu kuwa ndiye aliyewavusha Bahari ya Shamu, Musa alimjua zaidi kwa namna alivyokuwaanawasiliana naye ana kwa ana.
Ukijua jinsi Mungu wako anavyofanya kazi hata tatizo lako litaisha, kwa sababu unamjua Mungu  unayemtumika. Mtumishi wa Elisha alipotoka nje na kuona majeshi yaliyomzunguka, alirudi  ndani na kumwambia Elisha,  Bwana wangu na  Mungu wangu.” Ndiposa Elisha akamuuliza kwani kuna nini ulichokiona? Yule mtumishi akamwelezea vikosi  vya jeshi alivyoviona nje. 
Ukimjua unayemtumikia wala hatatishika.  Ungejua wapi tumaini lako lilipo utaishi  maisha mazuri sana. Ni kama vile Tanzania leo hii itangaze vita kupigana na Marekani leo hii, je unadhani Marekani itatishika hata kidogo? Hapana, kwa sababu Marekani inajua ilicho nacho cha kuiteketeza Tanzania. Tatizo la wakristo wengi hawamjui Mungu ila wanajua maandiko ya Mungu‼! Ukimuuliza mkristo andiko  fulanii lipo  wapi, atakutajia,lakini hajui Mungu aliyeyasema hayo maneno.
MITHALI 2:5…[Ndipo utakapofahamu kumcha Bwana, Na kupata kumjua Mungu.]…Kumbe kufunga,siyo kumjua Mungu. Kumbe kuomba siyo kumjua Mungu. Kumbe kuja kanisani siyo kumjua Mungu. Yamkini mtu anakuja kanisani kwa sababu zake binafsi, lakini kumjua Mungu anayemuamini hakupo. Wakristo wengi ni bingwa wa kubeba Biblia lakini siyo wa  kumjua Mungu. Kumjua Mungu huanza kwa “kusikia”, kwani  ndicho chanzo cha kumjua Mungu. Kabla ya kumjua Mungu unaanza kumfahamu Mungu  kwa njia ya kuzisikia habari zake.
Ndiyo maana katika Biblia kuna watu wanatajwa majina na wengine hawatajwi kabisa. Mfano ni "Tajiri mmoja" na "maskini mmoja jina lake Lazaro". Tajiri hajatajwa kwa sababu mbele za Mungu hakuwa na mahusiano yoyote. Lazaro ametajwa kwa sababu alimjua Mungu na kuwa na mahusiano na Mungu. Maisha ya  wokovu ni kukua  kutoka hapo ulipo na kwenda hatua nyingine. Maisha ya kila siku kama hayajabadilika ndiyo maana hata wewe hujabadilika‼
Mungu huangalia kile unachokihitaji wewe. Ndiyo maana Mungu maeiweka siku  ya hukumu,  kwa ajili ya kutuhukumu kwa matendo yetu.
WAFILIPI 3:8..[Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo;]… Paulo aliyaacha yote ya kumfanya asiwe na uhusiano na Mungu ,  na kuyahesabu kama hasara /  mavi kwake. Paulo ndani yake alikuwa na shauku  ya kutengeneza uhsiano na Mungu wake. Wapo watu wanatengenza mahusiano na kanisa au mchungaji kiongozi, na kuacha kuweka mahusiano na Mungu ambaye mwishowe kwake watatolea hesabu mbele zao zake. Shida ya watu ni kusahau kuwa, tunawajibika kwa Mungu mbinguni.  Je, Mungu anakuona wewe kama nani?  
Uhusiano wako na Mungu kama una kasoro, amka usingizini na kuweka mahsuaino mazuri na Mungu‼ Hivi mimi na Mungu tunashauriana? Kanisa haliwezi kukua na watu wanafiki, bali na wale walioamua ndani kuwa na Yesu Kristo. Siyo muda wa kufumbia  macho dhambi.  Kanisa linaanzia nyumbani, na maisha ya kila siku yapaswa yakuelezee jinsi ulivyo.  Ili uweze kuwa wa thamani kwa Mungu, tengeneza uhusiano wako na Mungu. Fanya mazoezi ya kuwa na Mungu ndanimwako. Yesu Kristo akae ndani yako.Wokovu wako uwe  wa kila saa na kila dakika. 
Unajua kuna vitu  vingine vinatupata kwa sababu ya kutotengeneza mahusiano yetu naMungu? Ukristo unakoelekea kwa sasa ni kubaya. Wokovu unakoelekea kwa sasa ni kwenye kuwa “DINI”.  Hii ni  kwa sababu hakuna mabadiliko ya ndani. Mtu alikuwa mwizi anaacha kuiba. Mtu alikuwa kahaba anaacha ukahaba. Leo hii wote hawa na tabia zao wanakuja kanisani nakutoa sadaka zao wakiwa na tabia zile zile. Hii ni kwa sababu watu wanapenda kumfurahisha mchungaji kiongozi badala ya kumpendezesha Mungu.
Biblia inasema “Usimpe ibilisi nafasi.” Lakni  je, hii nafasi tunampa je shetani? Ni kwa sababu hatutaki kutengeneza mahusiano na Mungu. Kwani Mungu wako ni  wa wakati wa kuumwa tu? Mungu wako ni  wa ndani kwa ndani tu?  Hapana. Ifike mahali watu wakikuona wamuone Mungu  unayemtumikia.  Inafaa kila mahali  tunapotembea Mungu wetu adhihirishwe. Ndiyo maana Biblia ikasema,  mtoto Yesu akakua katika kummjua Mungu  na kuwapendezesha wanadamu.
2 PETRO 1:2-3…[Neema na iwe kwenu na amani iongezwe katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu. 3 Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.]… Nikianza mimi kumjua Mungu  ananikirimia ili  kupata vyote. Kuna vitu unavishikilia ambavyo kwa Mungu ni dhambi, na hivyo huwezi kusaidiwa na Mungu kwa kujichanganya changanya. Kumbuka aliyewaokoa wana wa Israeli,  ni huyo huyo aliyewaangamiza Wamisri.
Shetani ana uwezo wa kukujengea ukuta kiasi kwamba kuomba kwako kukashindikana. Mtu wa aina hii, ni mzuri sana katika kusoma magazeti ya udaku au 'kucheza games' katika simu lakini kuomba Mungu hayupo tayari. Mchana wa leo, tunaenda kuvunja kila  uzio ambao adui amekuwekea ili kusababisha kukosekana kwa kiu ya maombi. Leo tutamuomba Bwana atupe kiu ya kujifunza neno la Mungu,  na kiu ya kusikiliza neno  la Mungu.
Kila kitu ukifanyapo huanzia ndani. Endapo  ndani  kukitaa, huwezi kufanya lolote. Shetani hupenda kuleta mawazo ya kukataa kufanya maombi. Hii  ni kufanya mahusiano yako na Mungu yasiwepo. Tumejifunza kuwa, ukimjua Bwana unapata vyote. Maisha yako yatabadilika  pindi tu  mtu akijenga mahusiano haya na Mungu.
 Kama  mtu uliyepo hapa hujaokoka, na kumwamini  Yesu Kristo kuwa  Bwana na Mwokozi wako, leo ndiyo  fursa ua kufanya hivyo. Na hata kama uliwahi kuokoka na baadae kuacha wokovyi, leo pia ni vizuri kufanya maamuzi upya na kugeuka ili  kuanza upya na Bwana Yesu.
UKIRI
Leo ninasambaratisha kila mashetani  walionizuia, kila mashetani mliokaa ili kunifunga,  kila  waliotumwa ili kunifunga ili  nisitengeneze mahusiano ya kudumu na Mungu leo nawasambaratisha Kwa Jina la Yesu Kristo. Amen
 

Comments