![]() |
Na: AMOS KOMBA (RP)
&
DR. GODSON ISSA ZACHARIA (SNP)
Utangulizi:
Kuna
laana nyingi zimeandikwa katika Biblia. Mathalani, miongoni mwa hizo laana ni
kama vile:-
1. Laana
za wazazi (kwa asiyemtii baba na mama),
2. Laana
ya wanadamu,
3. Laana zitokanazo na dhambi,
4. Laana
ya kutokulipa fungu la kumi
5. Laana
ya wachawi.
Je,
Laana ni kitu gani? Laana ni jambo/tukio baya linalokusudiwa na mtu mmoja ili
limpate mtu mwingine kwa minajili ya kuharibu maisha yake. Laana ni maneno
yanayotamkwa na mtu ili kumpata mwingine. Mfano katika Biblia, Nuhu alipokuwa
mkulima wa ardhi, alikunywa mvinyo na akalewa, akaanguka njiani na akabaki
uchi, na mwanae mdogo akaenda kuwaeleza ndugu zake mambo hayo. Hata hivyo wanae
wengine walichukua nguo wakarudi kinyumenyume wakamvisha nguo baba yao.
Nuhu alipozinduka akamlaani Kanaani
(mjukuu wake /mtoto wa mwanae aliyeuona uchi wake).
Wachawi
nao wanao uwezo wa kutamka laana katika maisha yetu. Lengo la laana mara zote ni
kusababisha mtu afe, au awe maskini, awe mgonjwa n.k. Nyakati nyingine wachawi hutamka laana siyo mtu afe, bali
kumtesa kwa magonjwa. Kumbuka kuwa maneno ni
roho. Imeandikwa YOHANA 6:63b
“maneno hayo niliyowaambia ni
roho, tena ni uzima.”
Mchawi akitamka maneno katika ulimwengu wa roho, anaziachilia roho.
Atamkapo ugonjwa, yale maneno hugeuka kuwa roho la ugonjwa
alioutamka na kufanya kile kilichokusudiwa kitokee.
Wachawi hutekeleza laana zao hizi katika madhabahu
za kichawi. Mchawi ni mwanadamu. Akiwa peke yake hawezi kukulaani. Anachokifanya
ni kuzitumia roho za kichawi ndani mwake
katika kufanya laana hiyo. Mchawi huyu huenda katika kikao cha wachawi kwa ajili ya kupeleka hoja / mashtaka dhidi ya mtu aliyekusudiwa. Msingi wa yote haya ni “wivu”.
Imeandikwa katika HESABU 22:1-3.. [Kisha wana wa Israeli wakasafiri na kupanga katika nchi tambarare za
Moabu ng'ambo ya pili ya Yordani karibu ya Yeriko. 2 Na Balaki mwana wa Sipori
akaona mambo yote ambayo Israeli wamewatendea Waamori. 3 Moabu akawaogopa hao
watu sana, kwa kuwa walikuwa wengi; Moabu akafadhaika kwa sababu ya wana wa
Israeli.]… Tatizo la Moabu hapa ni kuona wana wa Israeli wakiwa
wengi na yale matendo waliyowatendea Waamori. Inawezekana hata wewe una ndoa
nzuri, wapo wengine wanafadhaika kwa sababu hiyo. Inawezekana unajifungua
watoto wengi wazuri, na papo hapo wapo wengine wanafadhaika kwa sababu hiyo.
Imeandikwa katika HESABU 22:4 ...[Moabu akawaambia wazee wa Midiani, Sasa jeshi hili la watu litaramba
vitu vyote vinavyotuzunguka, kama vile ng'ombe arambavyo majani ya mashamba. Na
Balaki, mwana wa Sipori, alikuwa mfalme wa Moabu zamani zile.]…
Katika ulimwengu wa roho, kuna kamera za kumulika maendeleo ya watu wengine.
Uwoga wa wachawi ni kuona watu wakiwa wengi kwa sababu vitu vyao vitarambwa
kama ngo’mbe arambavyo majani. Kumbe ni vizuri kukusanyika sehemu ya pamoja
kanisani ili kuweza kuomba pamoja na kuramba vitu vya wachawi kwa Jina la Yesu.
Imeandikwa katika HESABU 22:5-6…[Basi Balaki akatuma wajumbe kwa Balaamu mwana wa Beori, hata Pethori,
ulio kando ya Mto, mpaka nchi ya wana wa watu wake, kwenda kumwita, akisema,
Tazama,kuna watu waliotoka Misri; tazama, wanaufunika uso wa nchi, tena wanakaa
kunikabili mimi. 6 Basi, njoo wewe, nakusihi unilaanie watu hawa; maana wana
nguvu kunishinda mimi. Labda nitawaweza, tupate kuwapiga, niwafukuze watoke
katika nchi yangu, kwa maana najua ya kuwa yeye umbarikiye hubarikiwa, na yeye
umlaaniye hulaaniwa.]… Hapa Balaki aliona wingi wa wana wa Israeli na kujua hakika akipigana
nao watamshinda. Kumbe mtu mwenye nguvu huwezi
kumshinda kirahisi, bali wachawi
wanachoweza kufanya ni kumlaani wemnye nguvu‼!.
UKIRI
Mashetani wote wa laana majini, wote wa laana, leo
naipiga laana zenu kwa Damu ya Yesu. Wasimamizi wa laana kwenye maisha yangu,
leo nawaondoa kwa Jina la Yesu. Imeandikwa
neno la Bwana ni moto, na mimi leo
nageuka na kuwa moto kwa jina la Yesu. Amen
|
Imeandikwa katika HESABU 22:7-12...[Wazee wa Moabu, na wazee wa Midiani, wakaenda, wakichukua ujira wa
uganga mikononi mwao; wakamfikilia Balaamu, wakamwambia maneno ya Balaki. 8
Akawaambia, Kaeni hapa usiku huu, nami nitawaletea jawabu kama Bwana
atakavyoniambia; wakuu wa Moabu wakakaa na Balaamu. 9 Mungu akamjia Balaamu,
akasema, Ni watu gani hawa ulio nao pamoja nawe? 10 Balaamu akamwambia Mungu,
Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu, amewatuma kwangu, akisema, 11 Tazama,
kuna watu waliotoka Misri, wanaufunika uso wa nchi; basi njoo unilaanie watu
hawa; labda nitaweza kupigana nao, na kuwafukuza. 12 Mungu akamwambia Balaamu,
Usiende pamoja nao; wala usiwalaani watu hawa, maana wamebarikiwa..]…
Mtu mwenye laana hawezi kufanikiwa. Hata hivyo, sisi tuliookoka tunao uwezo wa kubadili laana zao na kufanyika
baraka kwetu kwa Jina la Yesu.
UKIRI
Kila kilichotoka kwenye mikono yangu halafu
kikanifunga nakataa kwa Jina la Yesu.
maneno yoyoyte yaliyotamkwa leo nayafuta kwa Jina la Yesu. Ninauteka ulimwengu wa roho,
ulimwengu uliojaa laana nauteka kwa Jina la Yesu. Amen
|
Imeandikwa katika ISAYA 54:17…[Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi
utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa
watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana.]…Kila
anayelaani anao ulimi. Leo tunaenda kuhukumu ndimi za kina mama na kina baba
zilizoinuka kinyume nasi kwa Jina la Yesu. Kila laana za wachawi zinazohusu
taifa la Tanzania, leo tunaziondoa kwa Damu ya Yesu.
Maombi yetu leo yatalenga maeneo makuu matatu:
1.
Maombi ya kutoka kwenye laana. Ili
ufanikiwe ondoa laana kwanza. Ukiondoa laana ujue matunda ya laana hayatamea
tena.
2.
Kuyaondoa Mashetani yanayosimamia
laana. Yapo mashetani yanafanya kazi kwa
njia mbili: Yakiwa nje ya mwili wako au
yakiwa ndani ya mwili wako.
3.
Kuzishinda damu /sadaka za laana
zote. Leo tutanyamazisha damu zingine
zote kwa kutumia Damu ya mjumbe wa Agano
Jipya (Yesu Kristo).
Hata hivyo kama haujaokoka siyo rahisi kuweza kuzitoa laana. Utakapookoka utapata faida za aina mbili: Yesu ambaye ana vitu vyote ataingia ndani mwako na kisha atakupa vyote unavyohitaji. Faida ya pili ni kuwa na nguvu ya kuwashinda wachawi na laana zao.
Comments