RAIS JOHN MAGUFULI AAPISHWA KUSHIKA AWAMU YA TANO.

Rais John Magufuli akikagua gwaride kwa mara ya kwanza kabisa kama Amiri jeshi mkuu wa majeshi ya Tanzania na rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania


Mh.John Pombe Joseph Magufuli ameapishwa rasmi siku ya leo Alhamis 5,2015 kuwa rais wa awamu ya tano na Amiri jeshi mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sherehe zilizofanyika leo katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam na Kuhudhuriwa na Viongozi wa Kitaifa na Marais wa nchi mbalimbali za Afrika na Dunia pamoja na mabalozi wa nchi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania.Rais Magufuli anaanza rasmi Uongozi wake ikiwa pia ni siku ya kustaafu rasmi kwa aliyekua rais wa awamu ya nne wa Mh.Jakaya Mrisho Kikwete.

Picha za tukio zima la Uapishwaji wa rais John Magufuli ni kama zinavyoonekana hapa
Rais John Magufuli akila Kiapo cha kulitumika taifa la Tanzania kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Rais John Magufuli akisaini Kupokea Uongozi kama Rais wa Tanzania






Makamu wa Rais Mh.Samia Suluhu akila Kiapo cha kulitumikia taifa la Tanzania kama Makamu wa Rais
Rais John Magufuli akipewa pongezi toka kwa  Rais Uhuru Kenyata wa Kenya baada ya kuapishwa

Rais Magufuli akiwa na Marais mbalimbali wa nchi za Afrika
Rais John Magufuli akiwa na Rais Uhuru Kenyata na Mh.Raila Odinga 

Wake wa marais wa nchi za Afrika Mashariki 






























Comments