SITANYAMAZA HADI NIPATE KILICHOIBIWA




Na:  STEVEN NAMPUNJU (AP),UFUFUO NA UZIMA MOROGORO.
Utangulizi: Ipo tofauti kati ya kunyamaza na kutulia. Mtu anapokuwa amenyamaza, anakuwa kimya, hatoi majibu wala maamuzi yoyote. Lakini Utulivu ni ile hali  ya kuwa kimya. Katika Biblia haipo mahali pengine popote ambapo Mungu ametoa ahadi kubwa kama hii ya kutonyamaza wala kutulia, kama ilivyoandikwa katika ISAYA 62:1…[1 Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia, hata haki yake itakapotokea kama mwangaza, na wokovu wake kama taa iwakayo.]...Yerusalem ni makao matakatifu wanapokaa watu wa Mungu. Vivyo hivyo, hata katika taifa lako, Mungu hawezi kutulia wala kunyamaza unapomuita. Mungu wetu ni kweli,  na anaposema kweli, kila uwongo hujitenga. Sayuni yako kwa leo ni Tanzania, ambayo kupitia hiyo, Mungu  anataka akutoe sehemu moja kwenda sehemu nyingine.
Sayuni ilikuwa “ngome ya Wayebusi”, na ikiwa sehemu moja na mji wa Yerusalemu. Imeandikwa katika ISAYA 65:1-7…[ Watu wasionitaka wanauliza habari zangu; nimeonekana na hao wasionitafuta; naliliambia taifa lisiloitwa kwa jina langu, 2 Nitazameni, nitazameni. Mchana kutwa nimewanyoshea mikono yangu watu walioasi, watu waendao katika njia isiyo njema, wakifuata mawazo yao wenyewe; 3 watu wanikasirishao mbele za uso wangu daima, wakitoa dhabihu katika bustani zao, na kufukiza uvumba juu ya matofali; 4 waketio kati ya makaburi, na kulala katika mahali pao pa siri; walao nyama ya nguruwe, na mchuzi wa vitu vinichukizavyo u katika vyombo vyao; 5 watu wasemao, Simama peke yako, usinikaribie mimi, kwa maana mimi ni mtakatifu kuliko wewe; watu hao ni moshi puani mwangu, moto uwakao mchana kutwa. 6 Tazama, neno hili limeandikwa mbele zangu. Sitanyamaza, lakini nitalipa, naam, mimi nitawalipa ujira wao vifuani mwao; 7 maovu yenu na maovu ya baba zenu pamoja, asema Bwana, ninyi mliofukiza uvumba juu ya milima, na kunitukana juu ya vilima; basi, kwa ajili ya hayo nitawapimia kwanza kazi yao vifuani mwao.]… Mungu anasema hawezi kunyamaza kwa ajili ya mtu anayetengwa na jamii yake.  Mungu anaweza kunyamaza kwa habari ya adui zangu, lakini kwa upande wetu Mungu hawezi  kunyamaza kamwe‼!.
Tunajifunza kuwa Samsoni alikuwa mnadhiri wa Mungu tokea akiwa tumboni. Kwa hali  hiyo, Mungu hawezi kumuacha mtu  kama huyu, kwa kunyamaza tu pale anapomlilia. Yapo mengi  yanayoweza kumfanya Mungu anyamaze unapomuita.
Mji  unaweza kufungwa, na hata viongozi wake kufungwa kwa malengo fulani. Imeandikwa katika YOSHUA 6:1-27 ..[ Basi Yeriko ulikuwa umefungwa kabisa kwa sababu ya wana wa Israeli; hapana mtu aliyetoka wala hapana mtu aliyeingia. 2 Bwana akamwambia Yoshua, Tazama, nimeutia Yeriko katika mkono wako, na mfalme wake, na mashujaa wake. 3 Nanyi mtauzunguka mji huu, watu wote wa vita, mkiuzunguka mji mara moja. Fanya hivi siku sita.4 Na makuhani saba watachukua tarumbeta saba za pembe za kondoo waume, mbele ya hilo sanduku; na siku ya saba mtauzunguka mji mara saba, nao makuhani watapiga tarumbeta zao. 5 Kisha itakuwa watakapopiga hizo pembe za kondoo waume kwa nguvu, nanyi mtakaposikia sauti ya tarumbeta, watu wote watapiga kelele kwa sauti kuu; na ukuta wa mji utaanguka chini pale pale, na hao watu watapanda, kila mtu akiendelea mbele kukabili.  6 Bali Yoshua, mwana wa Nuni, akawaita makuhani, akawaambia, Lichukueni sanduku la agano, tena makuhani saba na wachukue tarumbeta saba za pembe za kondoo waume mbele ya sanduku la Bwana.7 Naye akawaambia watu, Piteni mbele, mkauzunguke mji, na hao watu wenye silaha na watangulie mbele ya sanduku la Bwana. 8 Basi ikawa Yoshua alipokwisha kusema na watu, wale makuhani saba, wenye kuzichukua tarumbeta saba za pembe za kondoo waume mbele za Bwana, wakatangulia, wakazipiga hizo tarumbeta; nalo sanduku la agano la Bwana likawafuata. 9 Wale watu wenye silaha walikwenda mbele ya hao makuhani waliozipiga tarumbeta, na wale waliokuwa nyuma wakalifuata hilo sanduku; makuhani wakizipiga tarumbeta walipokuwa wakienda. 10 Yoshua akawaamuru watu, akasema Msipige kelele, wala sauti zenu zisisikiwe, wala neno lo lote lisitoke kinywani mwenu, hata siku ile nitakapowaamuru kupiga kelele, ndipo mtakapopiga kelele. 11 Basi akalipeleka sanduku la Bwana liuzunguke huo mji, likauzunguka mara moja, kisha wakaenda kambini wakakaa kambini. 

12 Yoshua akaondoka asubuhi na mapema, nao makuhani wakalichukua sanduku la Bwana. 13 Na wale makuhani saba wakazichukua tarumbeta saba za pembe za kondoo waume mbele ya sanduku la Bwana, wakaendelea wakazipiga tarumbeta; nao watu wenye silaha wakawatangulia, na hao waliokuwa nyuma wakalifuata sanduku la Bwana; makuhani wakizipiga tarumbeta walipokuwa wakienda. 14 Siku ya pili wakauzunguka mji mara moja, wakarejea kambini; ndivyo walivyofanya siku sita. 15 Ikawa siku ya saba wakaondoka asubuhi na mapema wakati wa mapambazuko, wakauzunguka mji vivyo hivyo mara saba; ila siku hiyo waliuzunguka huo mji mara saba. 16 Hata mara ya saba makuhani walipozipiga tarumbeta, Yoshua akawaambia watu, Pigeni kelele; kwa maana Bwana amewapeni mji huu. 17 Na mji huu utakuwa wakfu kwa Bwana, mji wenyewe na vitu vyote vilivyomo; isipokuwa Rahabu, yule kahaba, ataishi, yeye na watu wote walio pamoja naye nyumbani, kwa sababu aliwaficha hao wapelelezi tuliowatuma. 18 Na ninyi, msikose kujiepusha na kitu kilichowekwa wakfu; msije mkakitwaa kitu kilichowekwa wakfu, baada ya kukiweka wakfu; nanyi hivyo mtayafanya matuo ya Israeli kuwa yamelaaniwa na kuyafadhaisha. 19 Lakini fedha yote, na dhahabu, na vyombo vya shaba, na chuma, ni vitakatifu kwa Bwana; vitaletwa katika hazina ya Bwana. 20 Basi watu wakapiga kelele, na makuhani wakazipiga tarumbeta; hata ikawa, hapo watu waliposikia sauti ya tarumbeta hao watu wakapiga kelele kwa sauti kuu sana, na ule ukuta wa mji ukaanguka nchi kabisa, hata watu wakapanda juu, wakaingia katika mji, kila mtu akiendelea kukabili mbele; wakautwaa huo mji. 21 Basi wakaangamiza kabisa vitu vyote vilivyokuwa ndani ya mji, wanaume na wanawake, watoto na wazee, na ng'ombe, na kondoo, na punda, kwa makali ya upanga. 22 Naye Yoshua akawaambia wale wanaume wawili walioipeleleza nchi, Ingieni katika nyumba ya yule kahaba, mkamtoe huyo mwanamke mwenyewe na vitu vyote alivyo navyo, kama mlivyomwapia. 23 Basi wale vijana wapelelezi wakaingia, wakamtoa Rahabu, na baba yake, na mama yake, na ndugu zake, na vitu vyote walivyokuwa navyo, wakawatoa na jamaa zake wote pia; wakawaweka nje ya matuo ya Israeli. 24 Kisha wakauteketeza mji kwa moto, na vitu vyote vilivyokuwa ndani yake; bali fedha, na dhahabu, na vyombo vya shaba, na vya chuma, wakavitia katika hazina ya nyumba ya Bwana.25 Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu, yule kahaba, na watu wa nyumba ya baba yake, na vitu vyote alivyokuwa navyo; naye akakaa kati ya Israeli hata leo; kwa sababu aliwaficha wale wajumbe aliowatuma Yoshua ili kuupeleleza mji wa Yeriko. 26 Naye Yoshua akawaapisha kiapo wakati ule, akasema, Na alaaniwe mbele za Bwana mtu yule atakayeinuka na kuujenga tena mji huu wa Yeriko; ataweka msingi wake kwa kufiliwa na mzaliwa wa kwanza wake, tena atayasimamisha malango yake kwa kufiliwa na mtoto wake mwanamume aliye mdogo. 27 Basi Bwana alikuwa pamoja na Yoshua; sifa zake zikaenea katika nchi ile yote.]….Kuna mahali wana wa Israeli walipaswa kwenda, lakini Yeriko ikajengwa haraka ili kuwazuia. Kuna mahali ulipaswa uwe  au  ufike, lakini adui zako wakaufunga mlango ili usipenye kabisa.
Swali: Kwa nini Yeriko ifungwe kwa wajli  ya wana wa Israeli? Hata wewe, kuna waliojenga ukuta kukuzuia usifanikiwe au kufikia kule ambapo Mungu alikusudia.Siri ya kufanikiwa kwa wana wa Israeli ilikuwa kupiga kelele‼! Ndani ya ule  mji waliteka nyara, wakatwaa utajiri,kila kilichokuwa chema ndani ya huu mji. Unapozuia taifa la Mungu, wakiingia kwako wanaondoka na vile vyako. Ndicho  kulichotokea kwa wana wa Israeli.
UKIRI
Leo sitanyamaza, katika Jina la Yesu. Chochote kilichowekwa mbele yangu ili ninyamaze, leo sitanyamaza kwa Damu ya Yesu. Amen.
Unapkutana na vikwazo pande zote, ujue kuwa umebeba muujiza ndani mwako. Katika hali yoyote unayoipiita, usimwache Bwana. Kuna nyakati ambapo,  baraka na mafanikio yanakuwa yamefichwa ndani ya taabu zako. Kwenye Goliath kulitukana taifa la Israeli, ufalme wa Daudi ulikuwepo. Unapompiga Goliath,  ufalme unakuja kwako.  Wapo watu ambao  hawawezi kuupata ushindi kamili, kwa sababu ya kuvunjwa moyo au kukumbana na vikwazo mbalimbali. Unapaswa kukataa kunyamazishwa, ung’ngane kwa namna yoyote ile hadi ukombozi wako uwe dhahiri kwa kuonekana katka Jina la Yesu.
Sayuni ni tafsiri ya mji ulioimarika. Ahadi za Mungu  kwa ajili ya Sayuni zimeandikwa pia katika ZABURI 87:2…[Bwana ayapenda malango ya Sayuni Kuliko maskani zote za Yakobo.]… Shetani hawezi kutawala popote au  kumtumikisha mtu yeytoe kama hana faida. Baada ya Daudi kuiteka Sayuni, ulipewa jina la Mji wa Daudi. Imeandikwa katika 2SAMWELI 5:1-10…[ 1 Ndipo kabila zote za Israeli wakamwendea Daudi huko Hebroni, wakasema naye, wakinena, Tazama, sisi tu mfupa wako na nyama yako. 2 Zamani za kale, hapo Sauli alipokuwa mfalme juu yetu, wewe ndiwe uliyewaongoza Israeli watoke nje, na kuingia ndani. Naye Bwana akakuambia, Wewe utawalisha watu wangu Israeli, nawe utakuwa mkuu juu ya Israeli. 3 Basi wazee wote wa Israeli wakamwendea mfalme huko Hebroni, naye mfalme Daudi akapatana nao huko Hebroni mbele za Bwana; wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya Israeli. 4 Daudi alikuwa amepata miaka thelathini alipoanza kutawala, akatawala miaka arobaini. 5 Huko Hebroni alitawala miaka saba na miezi sita; na katika Yerusalemu alitawala miaka thelathini na tatu juu ya Israeli wote na Yuda. 6 Kisha mfalme na watu wake wakaenda Yerusalemu ili kupigana na Wayebusi, wenyeji wa nchi ile; hao ndio waliomwambia Daudi, wakisema, Usipowaondoa vipofu, na viwete, hutaingia humu kamwe; huku wakidhania ya kuwa Daudi hawezi kuingia humo. 7 Lakini Daudi aliipiga ngome ya Sayuni; huu ndio mji wa Daudi. 8 Naye Daudi alisema siku hiyo, Yeye atakayewapiga Wayebusi, na apande kwenye mfereji wa maji, na kuwapiga viwete, na hao vipofu, ambao roho yake Daudi inawachukia. Kwa sababu hii watu husema, Wako vipofu na viwete hawawezi kuingia nyumbani. 9 Basi Daudi akakaa ndani ya ngome hiyo, akaiita mji wa Daudi. Kisha Daudi akajenga toka Milo na pande za ndani. 10 Naye Daudi akazidi kuwa mkuu; kwa maana Bwana, Mungu wa majeshi, alikuwa pamoja naye.]… Sayuni  ilikuwa ngome,  ambayo baada ya kupigwa na Daudi,  ilibadilishwa jina. Wapo Wayebusi waliokaa katika hatima yako.
Wayebusi waliokaa ndani ya Sayuni, walikaa pamoja na Israeli. Yoshua alishindwa kuwondoa Wayebusi kwa sababu walikuwa watu hodari. Hata hivyo, Daudi alikuja kuuteka huu mji na ngome yao na kubadilisha Jina la Mji huu  kuitwa Mji wa Daudi.
1 WAFALME 8:1…[Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa kabila, wakuu wa mbari za mababa wa wana wa Israeli, wamwendee mfalme Sulemani huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la agano la Bwana kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni.]… Huu ni udhihirisho wa Mji wa Sayuni, uliotekwa na Daudi na kuitwa Mji wa Daudi.

2NYAKATI 5:2…[Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa kabila, wakuu wa mbari za mababa wa wana wa Israeli, huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la agano la Bwana kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni.]…Kupitia Sayuni, ukoo wa Yesu ulitokea hapo.
UKIRI
Ngome yoyote iliyopewa jina ili kunizuia nisipate vyangu niachie kwa Jina la Yesu. Achia leo kwa Jina la Yesu. Yeyote unayekuja ili uninyamazishe, leo uniachie kwa damu ya Yesu. Kuanzia leo, na kuanzi sasa roho yoyote iliyotumwa kwangu ili kuninyamazisha leo naikataa kwa Damu ya Yesu. Kuanzia leo sitanyamaza kwa Jina la Yesu. Achia maisha yangu, leo nakataa kunyamaza katika Jina la Yesu. Amen
Mungu  anaposema kwa ajili  ya Sayuni hatanyamza ni kwa sababu Sayuni ni mji wake na israeli ni Taifa lake. Kwenye maisha yetu, Mungu hawezi kunyamaza pia. Shetani  anaweza kuona miisho ya jambo kabla ya hilio jambo kutokea.
Vita inapotokea kwako ni ili unyamaze. Magonjwa yanapokuja kwako ni ili unyamaze. Shetani alitaka kumnyamazisha Ayubu lakini Ayubu akakataa kunyamazishwa. Shetani akatumiambinu zote,ikiwemoyakumtumia mke wa Ayubu,lakini Ayubu akakataa kunyamazishwa. Ukikataa kunyamaza Mungu ataingilia kati na utashinda.
Paulo na Sila walikatazwa wasihubiri kwa habari za Yesu Kristo, na walipokataa kunyamazishwa wakawekwa gerezani. Wakiwa ndani ya gereza, waliendelea kupiga kelele za shangwe na kumwimbia Bwana Mungu. Usiku ule  ule, malaika wa Bwana alikuja na kuondoka na wale waliokuwa wakimwimbia Bwana na wafungwa wengine wakabaki mle  ndani wakishangaa. Kataa kunyamazishwa kwa Jina la Yesu hadi ushindi wako utokee.
Kama sina watoto sitanyamaza‼ Kama sijapata afya sitanyamaza‼. Raheli alikataa aina zote za faraja za wanadamu, akiulizia wapo wapi watoto wake? Wakiweza kukunyamazisha,  maana yake wamefanikiwa kumiliki hatima yako. Bartimayo wakati akitaka kuupata muujiza wake, walitokea watu wa kumnyamazisha. Hata hivyo, Bartimayo hakukubali kunyamazishwa na aliendelea kupaza sauti yake,  hata alipopata uponyaji  wake. Ngome yoyote mbele yako ipo kwa ajili ya kuzuia mafanikio yako. Anayekunyamazisha ni yule anayetaka ukae katika hali  ulioyo nayo.
Endapo yupo mtu ambaye haujaokoka, na upo katikati yetu, ni vyema leo kufanya maamuzi ya kuja kwa Yesu na  kuokoka.

Comments