Skip to main content
Ajali ya Basi yapoteza Maisha ya wachungaji wawili na wake zao wakitokea kwenye Kongamano
Ajali ya basi iliyotokea mkoani singida
jumatatu usiku baada ya basi kugongana na Lori imefahamika kwamba ndani
ya basi hilo walikuwemo wachungaji wawili na wake zao ambapo kwa pamoja
walikua wakitoka jijini Dar es Salaam kwenye Kongamano la Wachungaji wa P A G
ambalo lilifanyika katika kanisa la Dar es Salaam Pentecostal Church.
Kutoka kwenye Ukurasa wa facebook wa kanisa hiloo wameandika kama ifuatavyo na kuweka picha za wachungaji hao
DPC inasikitika kutangaza kifo cha wachungaji wawili waliopoteza maisha
yao jana kwa ajali ya basi wakiwa safarini kuelekea Geita, Wachungaji
hao ni kati ya wale waliotembelea kanisa la DPC na tuliabudu nao siku ya
jumapili kuanzia ibada za asubuhi na Ibada ya kusifu na kuabudu. Askofu
Lema Geita amefariki kwenye ajali hiyo. Habari kuhusu Mkewe bado
tunaendelea kufuatilia, Tafadhali chukua wakati kuombea watoto wao
waliowaacha na pia ombea makanisa waliokua wakiyaongoza, Mungu awe ndiye
Nguzo ya kila kitu, Amina.
Comments