MATUKIO YA KICHAWI




Na: DR. GODSON ISSA ZACHARIA (SNP)
STEVEN NAMPUNJU(RP), UFUFUO NA UZIMA MOROGORO

Utangulizi wa Somo: matukio ya Kichawi ni matukio yanayotokea kufuatana na uchawi kuhusishwa. Duniani leo, zipo nguvu nyingi za giza zinazotumiwa na wanadamu, na nguvu hizo ni  UCHAWI. Malengo ya wachawi au wanadamu kutumia  uchawi ni:
·        Kuwaumiza watu wengine kimazingara
·        Watu wengine hutumia uchawi ili kujilinda
·        Wengine tu huutumia uchawi kwa ajili ya kujifurahisha. Hawa ni wale ambao wakiwatesa watu wengine hufurahia kuona mateso yale. Yesu alisema, “furaha yangu ni kuona mapeznzi ya Baba yangu yanatimia”. Upande wa shetani wao hufurahi kuona mabaya yakitokea.
·        Wengine hutumia uchawi kwa ajili ya kufanya miujiza /mazingaumbwe n.k.
Imeandikwa katika HESABU 23:23…[Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!]…. Inamaanisha kuwa,  endapo uchawi haupo, basi mtu anaweza kufanya jambo nalo likafanikiwa.
Wachawi huwa na mawasiliano ya karibu na roho za mashetani.
Katika Biblia wapo amaboa waliwahi kutengenezewa matukio:
Mfano 1: MATHAYO 9:32-34…[Hata hao walipokuwa wakitoka, tazama, walimletea mtu bubu mwenye pepo. 33 Na pepo alipotolewa, yule bubu alinena, makutano wakastajabu, wakasema, Haijaonekana hivi katika Israeli wakati wo wote. 34 Lakini Mafarisayo wakasema, Kwa nguvu za mkuu wa pepo atoa pepo.]… Hapa Yesu anamsaidia mtu bubu ambaye madaktari na familia yake walikuwa na taarifa tofauti ambayo Yesu aliibadilisha historia na taarifa hizo kuwa uponyaji wa kudumu. Yamkini hata wewe kwenye ukoo wako yapo mambo ambayo mnayazoea kama yahusuyo ukoo wenu. Ukimwamini Yesu atabadili historia yako.
Mfano 2: MARKO 9:14-18…[Hata walipowafikia wanafunzi, waliona mkutano mkuu wakiwazunguka, na waandishi wakijadiliana nao; 15 mara mkutano wote walipomwona walishangaa, wakamwendea mbio, wakamsalimu. 16 Akawauliza, Mnajadiliana nini nao? 17 Mtu mmoja katika mkutano akamjibu, Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako, ana pepo bubu; 18 na kila ampagaapo, humbwaga chini, naye hutoka povu na kusaga meno na kukonda; nikasema na wanafunzi wako wamtoe pepo, wasiweze.]… Mzazi wa huyu kijana alipogundua matatizo ya mwanae, alijua kuwa ni pepo na kwamba matukio haya ni ya kutengenenezwa. Kitendo  chake cha kumwaamini Yesu  kilimfanya amlete huyu mwanae kwa Yesu.
Matukio  ya huyu  kijana (mfano wa 2) ni  ya kubwagwa chini‼:  Kwamba akiwa kitandani, mapepo yakimpanda yanambwaga chini. Kwamba angekuwa yupo kwenye ndoa baadae anabwagwa chini (kuachika). Tukio  lingine ni  kukonda. Unaweza kutumia virutubisho vyote kwa mwanao lakini bado anaendelea kukonda tu.
Imeandikwa MARKO  9:19-21…[Akawajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, nikae nanyi hata lini? Nichukuliane nanyi hata lini? Mleteni kwangu. 20 Wakamleta kwake; hata alipomwona, mara yule pepo alimtia kifafa; naye akaanguka chini, akagaagaa, akitokwa na povu. 21 Akamwuliza babaye, Amepatwa na haya tangu lini? Akasema, Tangu utoto.]…Unaweza kuwa na  matukio maishani unayoyaona kama ya kuzaliwa nayo. Ukimwamini Yesu matukio  kama haya yanango’oka kwa Jina la Yesu. Hata kama taabu uliyo nayo ni ya miaka mingi, itaondoka tu.
Imeandikwa MARKO 9:22-27…[Na mara nyingi amemtupa katika moto, na katika maji, amwangamize; lakini ukiweza neno lo lote, utuhurumie, na kutusaidia. 23 Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye. 24 Mara babaye yule kijana akapaza sauti, akasema, Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu. 25 Naye Yesu akiona ya kuwa mkutano unakusanyika mbio, akamkemea yule pepo mchafu, akamwambia, Ewe pepo bubu na kiziwi, mimi nakuamuru, mtoke huyu, wala usimwingie tena. 26 Akalia, akamtia kifafa sana, akamtoka; naye akawa kama amekufa; hata wengi wakasema, Amekufa. 27 Lakini Yesu akamshika mkono akamwinua naye akasimama.]…Matukio yaliyofuatia maombi ya Bwana Yesu ni: Kijana kutiwa kifafa sana, pepo akamtoka, akawa kama amekufa.
Jamii yako  yaweza kuleta visa wanapokuona umeletwa kanisanai kuombewa. Wengine watasema unaonekana kama umekufa. Hata biashara yako yaweza kuonekana kama imekufa baada ya kuombewa. Wachawi wakitengeneza tukio baya la ubaya au mauti, Mungu hulibadilisha na kuwa tukio jema la wokovu kwa Jina la Yesu.
Bwana ametutuma kutabiri uzima mahali pasipo na uzima kwa Jina la Yesu. Ezekieli alioneshwa bonde lenye mifupa mikavu, na  Bwana akamwambia aitabirie ile mifupa ili  iwe na uzima tena. Baada ya pale ulitokea upepo ambao uliifanya ile mifupa kuingiwa na nyama na uzima tena kwa ile mifupa.
HASARA ZA MATUKIO YA KICHAWI KUWEPO:
         1.         Matukio haya juweza kuzuia kutajwa kwa habaari ya mtu fulani:- Kivipi? Endapo ni ofisini, habari za mtu zinaweza kuzuiwa zisitajwe. Ni kama mchujo vile unafanyika. HESABU 23:23….[Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!]…Matukio  ya kichawi yakiondolewa, habari zako zitasemwa. Sasa, habari zangu zitasemwa. Endapo uchawi na uganga vitaondolewa, habari zako zitaanza kutangazwa na kusemwa.
         2.         Matukio ya kichawi huweza kumfanya mtu aache imani:- MATENDO 13:6-12.. [Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake BarYesu; 7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu. 8 Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), akashindana nao, akitaka kumtia yule liwali moyo wa kuiacha ile imani. 9 Lakini Sauli, ambaye ndiye Paulo, akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho, 10 akasema, Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka? 11 Basi, angalia, mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu, usilione jua kwa muda. Mara kiwi kikamwangukia na giza, akazungukazunguka na kumtafuta mtu wa kumshika mkono na kumwongoza. 12 Ndipo yule liwali, alipoyaona yaliyotendeka, akaamini, akiyastaajabia mafundisho ya Bwana.]… Tukio la kichawi hushindana na hatimanzuri ya mtu. Wapo watu wameacha waume au wake zao ichwai.
UKIRI
Achia habari zangu kwa Jina la Yesu. Ewe silaha ya kuacha imani kwa nguvu za kichawi,  leo achia kwa Jina la Yesu. Aliyetengenezea tukio  kwa ajili  ya misha yangu, nakataa kwa Jina la Yesu.
 

         3.         Matukio ya kichawihuweza kusbabisha magonjwa, hasasra na matatizo: Utagundua kuwa matukio kama haya yakiwemokatikafamili,matatizo nayo  huwa hayakosekani. 
NJIA IPI YA KUZISHINDA MATUKIO YA KICHAWI?
         1.         Ili  uweze kushinda, njia nzuri  ni kumpokea Yesu  Kristo  maishani mwako. Imeandikwa katika  YOHANA 1:12..[ Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;]… kwa hiyo,unapokuwa mwana wa Mungu,  siyo rahisi kwa wachawi na mawakala wao kukuletea matukio  ya magonjwa, au  misiba au mikosi.
         2.         Njia nyingine ni kuomba mwenyewe. Ni vizuri uweze kuomba ukiwa mwenyewe, kwa sababu siyo mara zzote  unaweza kuwa na wachungaji karibu na wewe kwa ajiliya kukuombea unapopatwa na matukio ya kichawi.

Comments