BAHATI BUKUKU AFIWA NA MAMA YAKE MZAZI.


 
Bahati Bukuku.

Muimbaji wa nyimbo za injili Bahati Bukuku amefiwa na mama yake mzazi ambaye amefariki Jana usiku wa January 11 2016. 

Umauti umemfika mama mzazi wa muimbaji huyo huko mkoani Mbeya ambapo alikuwa akiuguzwa maradhi ya Moyo. 

Kwa upande wake Bahati Bukuku yupo njiani kuelekea Mbeya kwa ajili ya msiba huo ambao upo Mwanjelwa. 

Taarifa zaidi zitakujia kwakadri ambavyo tutakuwa tukizipata. Mungu azidi kumtia Nguvu na kumfariji Bahati Bukuku pamoja na familia yake kwa ujumla. 

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA, JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.

Comments