KURUDISHA KILICHOIBIWA

Ufufuo na uzima Morogoro.
Na: DR. GODSON ISSA ZACHARIA (SNP)
Utangulizi wa Somo: Imeandikwa katika Isaya 42:22….[Lakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa; wote wamenaswa katika mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana aokoaye; wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha.]
Imeandikwa katika  Efeso 6:12 ..[Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.]

Tunashindana na falme katika ulimwengu wa roho, kuna wenye mamlaka wanaoshindana, wakuu wa giza, jeshi la mapepo wabaya. Tunapopiga majeshi tunashindana na majeshi ya kuzimu.

Yapo majeshi ya aina tatu,
·        Majeshi ya Mungu
·        Majeshi ya wanadamu.
·        Majeshi ya kuzimu
 

Sauti yako ya kusema kwa ukakamavu na mamlaka inamaanisha kile unachoongea,ipo nguvu katika kukiri. Kila kitu ufanyacho fanya kwa nguvu zako zote, si kwa ulegevu. Mmarekani akifanya jambo anafanya kwa nguvu zake zote. Umepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nnge, ina maana sumu ya nyoka iko kichwani na sumu ya nnge iko mkiani, hiyo mamlaka uliyo nayo ina uwezo pande zote.

Mtu anaweza kuibiwa na kutekwa na kufichwa shimoni(yaani wako msukuleni), kuna mashimo yanayoficha watu. Kuna watu ambao ni wanadamu, lakini wameibiwa wako magerezani,wamefichwa na aliyewaiba ni mkuu wa giza.

Imeandikwa katika 2Wakorin12:2 [Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata sasa miaka kumi na minne, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua). Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu.]

Mwanadumu ni muunganiko kati ya mwili, nafsi na roho. Roho ya mtu ikitoka nafsi inapotea pia. Mtu akifa maana yake ni ametengana na roho. Mtu anaweza kuibiwa akatolewa ndani ya mwili wake, na kuwekewa roho nyingine. Mtu anapochukuliwa msukule anaenda kutumikishwa, na yule mtu halisi anabakia na mateso,magonjwa, taabu n.k.

Imeandikwa katika Yohana 5:25…[Amin, amin, nawaambia, Saa inakuja, na sasa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai].

Imeandikwa katika 1Samweli 30:1-19…[Ikawa, Daudi na watu wake walipokuwa wamefika Siklagi siku ya tatu, hao Waamaleki walikuwa wameshambulia Negebu, na Siklagi, nao wameupiga Siklagi, na kuuchoma moto; 2 nao wamewachukua mateka wanawake waliokuwamo wakubwa kwa wadogo; hawakuwaua wo wote, ila wakawachukua, wakaenda zao. 3 Basi Daudi na watu wake walipoufikilia mji, tazama, ulikuwa umechomwa moto; na wake zao, na watoto wao, waume kwa wake, wamechukuliwa mateka. 4 Ndipo Daudi na watu waliokuwa pamoja naye wakainua sauti zao na kulia, hata walipokuwa hawana nguvu za kulia tena. 5 Na hao wake wawili wa Daudi walikuwa wamechukuliwa mateka, Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, aliyekuwa mkewe Nabali, wa Karmeli. 6 Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika Bwana, Mungu wake. 7 Kisha Daudi akamwambia Abiathari, kuhani, mwana wa Ahimeleki, Tafadhali niletee hapa hiyo naivera. Naye Abiathari akamletea Daudi naivera huko. 8 Daudi akauliza kwa Bwana, akasema, Je! Nikiwafuata jeshi hili, nitawapata? Naye akamjibu, Fuata; kwa kuwa hakika utawapata, nawe hukosi utawapokonya wote. 9 Basi Daudi akaenda, yeye na wale watu mia sita waliokuwa pamoja naye, nao wakakifikilia kijito Besori, ambapo wale walioachwa nyuma walikaa. 10 Lakini Daudi akakaza kufuata, yeye na watu mia nne; kwa maana watu mia mbili walikaa nyuma, ambao walitaka kuzimia hata hawakuweza kukivuka hicho kijito Besori. 11 Nao wakamkuta Mmisri mavueni, wakamleta kwa Daudi, na kumpa chakula, naye akala; nao wakampa maji ya kunywa; 12 kisha wakampa kipande cha mkate wa tini, na vishada viwili vya zabibu; naye akiisha kula roho yake ikamrudia; kwa maana alikuwa hakula chakula wala kunywa maji, siku tatu mchana na usiku. 13 Ndipo Daudi akamwuliza, Wewe u mtu wa nani; nawe umetoka wapi? Naye akasema, Mimi ni kijana wa Misri, mtumwa wa Mwamaleki mmoja; bwana wangu aliniacha, kwa sababu tangu siku hizi tatu nalishikwa na ugonjwa. 14 Sisi tulishambulia Negebu ya Wakerethi, na ya milki ya Yuda, na Negebu ya Kalebu; na huo mji wa Siklagi tukauchoma moto. 15 Daudi akamwambia, Je! Wewe utaniongoza chini hata nilifikilie jeshi hilo? Naye akasema, Uniapie kwa Mungu, ya kwamba hutaniua, wala kunitia mikononi mwa huyo bwana wangu, nami nitakuongoza chini hata kulifikilia jeshi hilo. 16 Na hapo alipokuwa amewaongoza chini, tazama, hao walikuwa wametawanyika juu ya nchi yote, wakila na kunywa, na kufanya karamu, kwa sababu ya hizo nyara kubwa walizochukua katika nchi ya Wafilisti, na katika nchi ya Yuda. 17 Naye Daudi akawapiga tangu ukungu wa jioni hata jioni ya siku ya pili; hakuna aliyeokoka, ila vijana mia nne waliopanda ngamia na kukimbia. 18 Daudi akawapokonya wote waliokuwa wamechukuliwa na Waamaleki; naye Daudi akawaokoa wakeze wawili. 19 Wala hawakupotewa na kitu, mdogo wala mkubwa, wana wala binti, nyara wala cho chote walichojitwalia hao; Daudi akavirudisha vyote.]
UKIRI
Leo tulazimishe kila kilichoibiwa katika maisha yetu kirudi katika jina la Yesu. Tunageuza karamu zao za kufurahia mateso yetu kuwa kilio katika jina la Yesu.Wote waliochukuliwa lazima warudishwe kwa jina la Yesu. Amen
 

Comments