JIOKOE NA KIZAZI HIKI CHENYE UKAIDI.

Na Peter Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.

 
BWANA YESU atukuzwe.
Nimepewa ujumbe huu nikujulishe ili ujiokoe na kizazi hiki chenye ukaidi.

Waefeso 5:16-17 Biblia inasema '' mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya BWANA. ''

Ndugu yangu, hizi ni zama za uovu mwingi hivyo nakusihi ujiokoe na kizazi hiki chenye ukaidi.
Jiokoe kwa kumkimbilia BWANA YESU.
Jiokoe kwa kuacha dhambi zote.
Usiige ubaya wala machukizo.
Jiokoe na kizazi hiki chenye ukaidi.
Kizazi hiki chenye ukaidi kinalisikia Neno la MUNGU lakini hakilitii wala kulifuata.
Wewe mpendwa wangu nakusihi ujiokoe na kizaz hiki chenye ukaidi.
Watu wengi leo wanalisikia Neno la MUNGU lakini wanaendelea na ukaidi wao.
Ni siku za mwisho hizi ndugu yangu, wewe nakuomba ujiokoe na kizazi hiki chenye ukaidi.
Nakuomba ishi maisha matakatifu maana huko ndiko kuukimbia ukaidi.
Usifuatishe namna na dunia hii ambayo imejaa uovu mwingi.

Ujumbe niliopewa ni kukutaka ujiokoe na kizazi hiki chenye ukaidi, wamewahi kupewa ujumbe kama huu watumishi wengi tu wa MUNGU. Mfano mmoja wao wa mtumishi wa MUNGU aliyeambiwa awaonye wanadamu ni huyu hapa Mtume Petro ambapo Biblia inasema juu yake kwamba '' Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi.-Matendo 2:40''

Ndugu, Kama nilivyoombiwa nikujulishe nakuomba jiokoe na kizazi hiki chenye ukaidi.
Jiokoe kwa kuamua kuokoka.
Jiokoe kwa kujitenga na uchawi.
Jiokoe kwa kuacha uzinzi na uongo.
Jiokoe kwa kuacha uovu wote.

Biblia inaendelea kusema ''Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda BABA hakumo ndani yake.Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na BABA, bali vyatokana na dunia.Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya MUNGU adumu hata milele.-1 Yohana 2:15-17 ''

Ninapoandika ujumbe huu roho yangu inaugua sana, natamani kila mtu ajue hasa kusudi la MUNGU kunipa ujumbe huu.
Natamani mzinzi mmoja aokoke na kuacha uzinzi wake.
Natamani dada anayetaka kutoa mimba aache na aokoke na kujitenga na dhambi hiyo.
Natamani mchawi mmoja aache uchawi wake leo kwa kukimbilia kanisani akaokoke.
Natamani mwizi mmoja atubu na kuachana na wizi.
Natamani ndugu mmoja ambaye ana tabia ya kutukana wazazi wake na kuwadharau aache na kuwaomba msamaha na aokoke.
Natamani mtu mmoja anayeimba nyimbo za kidunia aache na kuokoka.
Natamani mnajimu mmoja aachane na hila zake hizo na kuamua kumkimbilia BWANA YESU mwenye uzima wa milele.

Ndugu yangu wa kike nakuomba jiokoe na kizazi hiki chenye ukaidi, okoka na anza na BWANA YESU sasa.
Ndugu yangu wa kiume nakusihi sana jiokoe na kizazi hiki chenye ukaidi, mpokee BWANA YESU na anza kuishi maisha matakatifu.
Baba zangu, Mama zangu, Dada zangu, Kaka zangu, Babu zangu, Bibi zangu na wadogo zangu nawasihini sana wote mjiepushe na kizazi hiki chenye ukaidi.
Waliomchagua shetani waache lakini wewe mpendwa wangu mchague YESU KRISTO leo.
wanaoendelea na dhambi wewe waache lakini nakusihi wewe mpokee BWANA YESU na anza kuishi maisha matakatifu.
Wanaoishi maisha ya maigizo naomba wasikushughurishe ila wewe mtii MUNGU tu na Neno lake maana huo ndio uzima wako.
Neno la MUNGU linasema '' Kwa maana jinsi hii MUNGU aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana MUNGU hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa MUNGU.Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa. Bali yeye aitendaye kweli huja kwenye nuru, ili matendo yake yaonekane wazi ya kuwa yametendwa katika MUNGU.-Yohana 3:16-21 ''

Ndugu jioke na kizazi hiki chenye ukaidi.
BWANA YESU anakungoja sasa ili uamue vyema leo.
Ubarikiwe sana.Nakuomba pia nisaidie kuwasambazia na wengine ujumbe huu.
Ni mimi ndugu yako Peter Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.
Mabula1986@gmail.com
+255714252292.

Comments