MWIGIZAJI WA FILAMU YA YESU AKATAA KUABUDIWA.

Robert Powell katika filamu akiigiza kama Yesu wa Nazareti

Kuanzia mwaka 1977 ulimwenguni kote katika nyumba za ibada za Kikristo, kumekuwa na utamaduni wa kuweka picha za muigizaji Robert Powell ambaye ameigiza kama Yesu wa Nazareth kwenye filamu ya maisha ya Yesu Kristo.

Lengo la kuwepo kwa filamu hiyo ni kukuza imani ya Kikristo ulimwenguni kwa waumini na si kumuabudu Robert Powell, kwani kilichofanyika katika filamu hiyo na mwigizaji huyo ni kuwakumbusha waumini wa Kikristo kuishi maisha ya uchamungu kutokana na mateso aliyopitia Bwana Yesu alipomwaga damu yake ili kuuokoa ulimwengu.
Mwigizaji Robert Powell
Mwigizaji Powell alijikuta katika wakati mgumu baada ya kupata muonekano wa kinabii kupitia filamu ya mateso ya Yesu aliyoiigiza na kuanza kuabudiwa na jamii inayomzunguka. Yeye na familia yake walijikuta jamii ikiwapa utukufu na kuona kama familia ile ina mtoto anayeitwa Yesu na si Robert Powell.

Waumini wengi wa Kikristo wamejikuta wakimwabudu mwigizaji huyu na wengine kufikia hatua ya kumuona kwenye njozi kwa kupata taswira yake na kuamini Yesu amewatokea. Hali hii imempa ugumu wa maisha ya kawaida mwigizaji huyu na kushindwa kufanya mambo yake mengine ya binafsi.

Mwigizaji Robert Powell

Kaamua kusema “Iam not Jesus Christ, I am just an actor and  British comedian, I am hurt and tired of seeing my photos displayed in places of worship and others worship and pray to me, I just made a film for a living, so people should stop loving and praying to me, burn my pictures, repent from your sins, live righteously and worship the only God in truth who can only be found in your heart and bible” alisema hayo Robert Powell.

Comments