HUDUMA YA KINABII(2)

Na Mtumishi Generali Geoffrey Mwanza Wambua,
The Global Evangelism Ministries (Kenya)

Bwana Yesu asifiwe?
6.NABII WA MAARIFA
Huyu anafunuliwa madawa ya mimea na chakula; vilevile ana uwezo wa kufunuliwa chanzo cha matatizo yako.
Ezekieli 47:12 "Na karibu na mto juu ya ukingo wake upande huu na upande huu utamea kila mti wa chakula ambao majani yake hayatakauka wala matunda yake hayatatindika kamwe...."
Nabii wa maarifa anapotumika katika utumishi wake; atapata mafunuo ya Roho ya uponyaji kupitia mimea; nafaka na matunda kwa ajili ya matatizo au magonjwa ya aina mbalimbali.
Namba yake ya utumishi inatembea katika mchepuo huu tofauti na manabii wengine.
Ufunuo 22:2-3 "Katikati ya njia kuu yake; upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima uzaao matunda aina kumi na mbili wenye kutoa matunda yake kila mwezi na majani ya mti huo ni kuwaponya mataifa..."
Nabii huyu wa maarifa anatumika na aina hii ya utumishi unaotoka kstika kiti cha enzi kwa kuwa MUNGU ndiye aliyeiumba miles kwa ajili ya binadamu na viumbe wengine.
Upinzani anaopata nabii wa maarifa ni kuwa anapingwa sana na watumishi maana wanafananisha anachokifanya kwa nuru na shetani.
Wengi wanaompinga nabii huyu wamekosa ufahamu wa Neno na hawana nuru ya ufahamu(Efeso 1:17-18)

6.NABII WA BARAZA
1Wafalme 22:19 "Mikaya akasema; sikia basi Neno la Bwana; nalimwona Bwana ameketi kitini chake cha enzi...."
Nabii huyu huudhuria vikao/baraza za mbinguni; Maeneo yake ni ya kanuni sana.
Akipatikana Kanisani kama huyu; Kanisa litafaidika kiroho na kiuchumi.Kwa sasa manabii wa aina hii ni wachache maana macho ya daraja hii in adimu sana hapa duniani.
Wakati MUNGU anakaa vikao mbinguni nabii huyu anaenda kuhudhuria kile kitakachozungumzwa na kuamriwa; yeye ataona na kusikia kwa ufasaha.
Unabii wake huwa umenyooka kweli kweli.



7. NABII WA NENO
Isaya 38:1-5 -Nabii huyu hutoa unabii wa papo kwa hapo; anajaa unabii tumboni wakati wowote na ana uwezo wa kutoa unabii.
Ndani ya nabii wa Neno kuna aina ya nabii anayetumika na wapiganaji wa mbinguni.
Nabii huyu anatumika kukomesha watu wote wanaothubutu kuitukana kazi ya MUNGU kwa ujeuri.
2 Wafalme 20:1-10 - Katika Biblia nabii Isaya alitumika katika eneo hili wakati fulani wa enzi za mfalme Hezekia.
8.NABII NA KUHANI
Ezekieli 1:3 "Neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani means wa Buzi kwa dhairi katika nchi ya Wakaldayo karibu na mto Kebari na mkono wa Bwana ulikuwa hapo juu yake"
Yeremia 18:18 "Hapo ndipo waliposema njooni tufanye mashauri juu ya Yeremia maana sheria haitampotea mwenye hekima wala neno halitampotea nabii..."
Nabii wa aina hii ana sehemu ya ukuhani ndani yake;amekirimiwa uwezo wa kubariki; kuwaomngezea watu siku za kuishi na ni mtetezi wa watu mbele za MUNGU .
Siyo kila mtu ni kuhani kama wengi wadhanivyo bali kuhani ni mtumishi mwenye heshima ya juu kiroho kuliko nabii mbele za MUNGU na unawekwa na MUNGU mwenyewe sio wewe unajiweka kuwa kuhani au kupewa kienyeji na wanadamu.
Nabii Samweli alitumika katika ngazi hii.
9.NABII ANAYEZUNGUMZA NA MUNGU MDOMO KWA MDOMO
Hesabu 12:8 "Kwake nitanena mdomo kwa mdomo; waziwazi sio kwa mafumbo na umbo la
Bwana yeye ataliona"

Nabii huyu hutokewa waziwazi na Bwana Yesu; RohoMtakatifu na MUNGU Baba na kuongea nao ana kwa ana (Kutoka 33:3-12).
Nabii wa aina hii anatokewa aidha na malaika; Yesu Kristo au MUNGU Baba bila kificho(Luka 9:28-34).
Aina hii ya nabii hufunuliwa mambo ya mbinguni peupe; huyu amepewa uwezo wa juu sana kuutawala ulimwengu wa roho na wakati wowote MUNGU akiwa na Neno hujifunua kwake.
10: NABII WA DHAMIRI SAFI
Warumi 9:1 "Nasema kweli katika Kristo; sisemi uongodhiri yangu ikinishuhudia katika RohoMtakatifu".
Nabii huyu anatumika na dhamiri safi kutoka ndani ya moyo wake kwa neema ya RohoMtakatifu na ni fundi wa imani.


11. NABII WA NENO, MAONO NA MAFUNUO YA MUNGU
Hii ni ngazi ya juu ya nabii anayetabiri na kufunuliwa maneno kutoka kwa MUNGU moja kwa moja.
Amepewa mamlaka ya juu sana na anachokitaka moyoni mwake kinakuwa saa hiyo iyo na akitamka neno linatokea saa hiyo iyo.
Anaweza akakubariki au akakulaani; Ni nabii wa pekee sana na aina hii ni adimu sana hapa duniani.
Hesabu 24:1-5 " Sasa Balaamu alitambua kwamba MUNGU alipenda kuwabariki Waisraeli kwa hivyo hakwenda kupiga bao tena...."
12.NABII KATIKA IDARA YA MWONAJI
Kazi ya nabii wa aina hii ni kuangalia mashauri ya MUNGU juu ya kazi yake; jamii na watu binafsi; lengo la MUNGU hapa ni:
-Kuwatahadharisha watu wasimwasi MUNGU.
-Kukosoa pale inapobidi au inapoonekana kasoro ndani ya taifa; jamii au Kanisa.
-Kujenga kiroho na kuimarisha kazi ya MUNGU hapa duniani.
Katika aina hii anaitwa nabii kwa kuwa anapata line muunganiko au mtandao wa moja kwa moja kutoka kwa MUNGU na anaitwa mwonaji kwa kuwa anapewa maono ya MUNGU .

2 Samweli 24:11-19, Yeremia 1:4-11.
13. NABII MWENYE MAMLAKA YA KULIITIA JINA LA BWANA AKAITIKWA.
Nabii wa aina hii ni moja ya wale waliopewa mamlaka ya juu sana katika utumishi mwenye kuliitia jina la Bwana,kusikilizwa na kuitikwa papo kwa hapo.
Nabii huyu amepewa neema ya kushusha mbingu chini na utukufu (shakaina glory)
Wingu linaloshuka hapa linaleta mambo yafuatayo:

-Mambo ya kutisha kutoka mbinguni.
-Matendo makuu ya MUNGU wa mbinguni.
-Maajabu kutoka mbinguni.
-Katika hali hii kila hitaji linapata jawabu.

Zaburi 99:6-8 " Musa na Haruni walikuwa makuhani wake.Samweli alikuwa miongoni ya waliomlilia.Walimlilia MUNGU naye akawasikiliza.Alisema nao katika mnara wa wingu.Walizingatia matakwa yake na amri alizowapa.Ee MUNGU wetu wewe uliwasikiliza"

14.NABII WA MATAIFA
Nabii wa aina hii hupewa neema ya juu sana na MUNGU ya kuhudumu katika mataifa mbalimbali.
Kazi zake huwa ni:
-Kung'oa.
-Kubomoa.
-Kuaribu.
-Kuangamiza
-Kujenga.
-Kupanda.

Yeremia 1:4-10 "Kisha Neno la Bwana likanijia kusema;kabla hujachukuliwa mimba mimi nilikujua; kabla hujazaliwa Mimi nilikuweka wakfu;nilikuchagua uwe nabii wa mataifa....Leo nimekupa mamlaka juu ya mataifa na falme; uwe na mamlaka ya kung'oa na kubomoa; mamlaka ya kuharibu na kuangamiza; mamlaka ya kujenga na kupanda"
KUFAFANUA MAMLAKA:
Kung'oa -kung'oa kila mapando ya shetani ndani ya watu; ardhi au eneo Fulani.
Kubomoa-Upako wa kubomoa ngome na falme za giza kwa jina la YESU KRISTO na kwa ufunuo atakaopewa na ROHO MTAKATIFU.
Kuharibu- Kuharibu kazi za shetani; mizimu; wachawi na mitego yote ya shetani kwa watu/ maeneo.
Kuangamiza- Kuangamiza majeshi ya mapepo yanayotesa wanadamu.
Kujenga- Kujenga ufalme wa MUNGU kwa neema ya pekee aliyokirimiwa na MUNGU katika jina la YESU kwa utumishi wake.
Kupanda- Kupanda mbegu njema ya Neno la MUNGU na kazi ya MUNGU hapa duniani kupitia kuhubiri injili ya kutubu na kuokoka.
MAMBO MUHIMU ZAIDI YA KUJUA:
Yafuatayo ni mambo muhimu zaidi ya kujua baada ya mwisho wa somo hili leo:
-ROHOMTAKATIFU amenipa ufunuo huo nifundishe somo hilo kwani watu wengi wanayo huduma hii ndani yao ila hawakupata mwalimu wa kuwafundisha wanatumika katika ofisi gani ya kinabii.
Huduma hii haiwezi kukuhakikishia kuingia mbinguni ni lazima UOKOKE na uache dhambi huku ukiyaishi maisha ya utakatifu ndani ya Bwana YESU.
Wacha kudanganywa na watu wanaojiita manabii kwa kukupira mali zako heti wameonyeshwa mambo yako uwatumie sadaka wakuombee.
Kuna watu wanaowadharau na kuwasema watumishi wa MUNGU ; tafadhali hii tabia ikome maana ukiendelea utapata mapiga na pengine maafa.
Unabii wa MUNGU wa mbinguni unaenda sambamba na Neno lake; haupingi Neno; wala Neno halipingi unabii wa MUNGU.
Mwisho kabisa: Mathayo 7:15 " Jihadharini na manabii wa uongo wanaowajieni kama kondoo kumbe ndani yao ni mbwa mwitu"
KAMA HAUJAOKOKA; NIPIGIE SIMU TUOMBE PAMOJA UOKOKE SASA MAANA HAKUNA MUDA MWINGINE WA KUTUBU NA KUOKOKA.
Generali Geoffrey Mwanza Wambua;
The Global Evangelism Ministries (Kenya);
+254 724 656 653;
geoffreymwanza@yahoo.com

Comments