Posted by
Peter Mabula
- Get link
- X
- Other Apps
Namshukuru MUNGU pikipiki iliyoibiwa imepatikana na mwanangu ameokoka
Naitwa Dorah Juliasi,
namshukuru MUNGU kwa MATENDO yake ya AJABU, Mwanangu alinunua pikipiki,
ilikuwa ni siku ya Jumatano na Alhamisi akamkabidhi ndugu yake (mdogo
wake) aifanyie kazi (biashara) kwa ajili ya kuendesha bodaboda.
Ilipofika siku ya Jumamosi ikaibiwa, mwanangu akanipigia simu akaniambia
kuwa imeibiwa nikamwambia usijali mimi kesho (Jumapili) naenda
Kanisani, akasema twende kwa mganga mimi nikamkatalia, nikamwambia Mimi
nina Imani na MUNGU, Mimi nitamtazama
MUNGU, ila yeye akaenda na akaambiwa apeleke jina la mtu anayemuhisi
kuwa kachukua, akarudi nyumbani ili apange siku ya kupeleka hilo jina.
Mume wa mwanangu aliyenunua hiyo pikipiki, naye akaenda kwa mganga
akaambiwa apeleke hela nyingi tu na yeye akarudi nyumbani ili ajipange
kupeleka hizo pesa. Mimi nilipofika Kanisani nikawashirikisha Viongozi
wangu wa Eneo la Yerusalemu tukaomba, na ilipofika Jumatatu nikafunga
huku namlilia MUNGU na siku ya Jumanne pikipiki IKAONEKANA. Huku kati ya
mwanangu na mume wa mwanangu wakiwa Hawajafanikiwa kurudi kwa mganga,
namshukuru MUNGU sana kwa mengi aliyonitendea, baada ya hayo huyu
Mwanangu wa Kiume ambaye Pikipiki aliibiwa, akaniambia “Mama nataka kuja
huko Kanisani EFATHA”, kweli Jumapili iliyopita alikuja Kanisani hapa
na AKAOKOKA na leo nimekuja naye ili Tumshukuru MUNGU pamoja. Mganga
wetu ni YESU KRISTO, Husipate tatizo ukakimbilia kwa mganga mwingine
bali njoo kwa YESU maana YEYE ndiye Kila kitu Kwako na Kwake tunapata
USHINDI.
Nimefaulu First class ya Chuo Kikuu
Naitwa Anthony John Bosko,
namshukuru Mungu kwa mengi aliyonifanyia katika elimu yangu. Wakati
ninaanza shule (yaani darasa la kwanza) kulikuwa na changamoto kwa maana
kuanzia darasa la kwanza nilikuwa ninaandikiwa nimeshindwa katika
mitihani yangu lakini ninamshukuru Mungu nikafaulu (second selection).
Nilipofika kidato cha pili (form 2) nikaokoka (Efatha) na hali ya masomo
yangu ikabadilika sana nikaanza kupata 80 hadi 100 wanafunzi wenzangu
tuliokuwa nao toka shule ya msingi walidhani kuwa ninabahatisha ila kumbe ilikuwa ndio Mungu ameanza kunibadilisha.
Nikafanikiwa kuingia kidato cha tano na cha sita na baada ya hapo nikaingia chuo Kikuu cha Mzumbe, nilipoingia chuo nikamwambia Bwana Yesu nataka nitoke na first Class nikawa ninaandaa sadaka maalum kwa ajili ya mitihani yangu na kila mtihani niliokuwa nafanya nilikuwa napata A tu. Namshukuru Mungu nikaweza kutoka na kile nilichokuwa nakihitaji (first class), sio kwa nguvu wala uweza wangu bali ni kwa YEYE anayeweza yote MUNGU mwenye NGUVU. Wokovu unamaana sana na wokovu ni Kipawa cha kukufanya uende mahali pa UTUKUFU mimi nimeshuhudia.
Nikafanikiwa kuingia kidato cha tano na cha sita na baada ya hapo nikaingia chuo Kikuu cha Mzumbe, nilipoingia chuo nikamwambia Bwana Yesu nataka nitoke na first Class nikawa ninaandaa sadaka maalum kwa ajili ya mitihani yangu na kila mtihani niliokuwa nafanya nilikuwa napata A tu. Namshukuru Mungu nikaweza kutoka na kile nilichokuwa nakihitaji (first class), sio kwa nguvu wala uweza wangu bali ni kwa YEYE anayeweza yote MUNGU mwenye NGUVU. Wokovu unamaana sana na wokovu ni Kipawa cha kukufanya uende mahali pa UTUKUFU mimi nimeshuhudia.
Mwanangu amefunguliwa kutoka katika vifungo vya kichawi
Naitwa
Mboni Mwaminifu namshukuru Mungu kwa Kumkomboa na Kumponya mwanangu
kutoka katika nguvu za kichawi. Shetani alimtumia kuharibu vitu vingi na
kufanya mambo mengi ya kipepo, tulihangaika makanisa mengi bila kupata
msaada, lakini siku moja tukaamua kumleta hapa Efatha ambapo aliombewa
na siku ya tarehe 14/8/2016 tulienda Precious Center Kibaha ambapo
kulikuwa na Ibada, Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias
Mwingira alitamka kuwa kila uchawi na ulozi mwisho leo, na tukashiriki
meza ya Bwana baada ya Ibada ile alitapika sana na sasa amekuwa mzima
kwa kuwa amefunguliwa kutoka katika nguvu hizo ambazo alipewa na Bibi
yake. Hakika Mungu ni mkuu na anatenda mambo ya ajabu Sifa na Utukufu
namrudishia yeye aliye mwenye uweza wote.
Comments