Na Peter M Mabula.
|
BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu.
Karibu tujifunze Neno la kutufanya tujue kile kitupasacho kujua.
Nimewahi kuulizwa swali hili zaidi ya mara kumi;
''Je nitamjuaje mchumba kutoka kwa MUNGU?''
''Je nifanyeje ili nijue kama huyu mchumba wangu ni chaguo la MUNGU kwangu au ni maamuzi yangu tu?''
''Nikitaka kupata Mke mwema/Mume mwema nifanyeje?''
Ni kweli kabisa haya ni moja ya mambo yanayowasumbua sana watu wengi sana.
Wengi hutamani kupata mke mwema lakini wao sio waume wema.
Wengi hutaka sana kupata waume wema lakini wao sio wake wema.
Kuna sifa nyingi ambazo mtu anayetaka kuoa/kuolewa huziangalia kwa huyo mwenzi.
Mithali 19:14 '' Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na BWANA.''
Mke mwema au mume mwema hutoka kwa MUNGU hakika.
Lengo la ujumbe wangu nataka ukaone tofauti hizi za kimwili au za kidunia na zile za kiroho. Baada ya kuzijua tofauti hizi basi unatakiwa utambue jinsi ya kubadili msimamo wako juu ya uchaguzi wako ili sasa umpate yule ambaye ana sifa za kiroho maana huyo ndio anastahili kwako.
Lakini pia unapohitaji mke mwema hakikisha wewe kaka unajichunguza kama kweli wewe ni mume mwema hata upewe mke mwema. Je unamcha MUNGU na unatembea katika utakatifu?
Kama dada unamhitaji mume mwema basi hakikisha wewe unafaa kuwa mke mwema kwa maana umeokoka na unaishi kwa kulitii Neno la MUNGU ndipo na wewe upewe mume mwema.
Mithali 19:22-23 '' Haja ya mwanadamu ni hisani yake; Ni afadhali maskini kuliko mwongo. Kumcha BWANA huelekea uhai; Atakaa ameshiba; hatajiliwa na ubaya. ''
Hebu sasa ona tofauti hizi za uchaguzi wa wachumba kulingana na kundi la mtu anayechagua.
=Kijana wa kiume asiyemcha MUNGU akihitaji mchumba hutaka sifa zifuatazo zote au baadhi ya sifa hizi.
1. Umbo zuri linalosifiwa na marafiki zake.
2. Sura nzuri inayowafanya marafiki zake wamsifie kwamba amepata kifaa.
3. Msomi kama yeye.
4. Anatoka familia nzuri.
5. Anamjua MUNGU japokua yeye muoaji ni mpagani.
6. Tabia nzuri japokua yeye muoaji hana tabia nzuri hata moja.
7. Atembee nae kwanza ili aone kama anafaafaa kumbe ni dhambi na hatari sana ya kuuvunja uchumba kabla hata ya ndoa.
Mithali 31:10 ''Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani. ''
=Binti asiyemcha MUNGU akihitaji mchumba hutaka sifa zifuatazo zote au baadhi ya sifa hizi.
1. Awe na pesa za kutosha zitakazomtosha katika mahitaji yake yote 100%.
2. Humtaka kijana aliyeokoka wakati yeye hajaokoka.
3. Awe Handsome na mchangamfu.
4. Awe na uwezo wa kumlinda hivyo awe na ka mwili kanakoweza kumpiga mtu mwingine kama atamchokoza huyo binti.
5. Awe na kazi nzuri sio tu kazi za ajabu ajabu.
6. Awe na elimu nzuri kuliko wote watakaomfuata.
7. Awe na usafiri au awe na mpango wa kununua usafiri mzuri.
Waebrania 13:4-6 '' Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi MUNGU atawahukumia adhabu. Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa. Hata twathubutu kusema, BWANA ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini? ''
=Binti aliyeokoka anapompenda mvulana hupendelea sifa hizi;
1. Awe anamjua MUNGU na ana hofu ya MUNGU.
2. Awe na kazi nzuri na huduma nzuri.
3. Awe na muonekano mzuri na mtanashati.
4. Awe na tabia nzuri na msimamo mzuri
5. Awe na lugha nzuri katika kinywa chake.
6. Awe na historia nzuri ya mwanzo.
7. Awe anakubarika kwa mchungaji.
Isaya 55:8-9 ''Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA. Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.''
=Kijana wa kiume aliyeokoka sifa anazopendelea kwa binti ni hizi;
1. Awe ameokoka kweli kweli kama yeye.
2. Awe ni mpole, mtii na mnyenyekevu na msikivu na mwelewa.
3. Awe na sura nzuri na muonekano kuwazidi wengine wote kanisani kwao.
4. Awe hana matumizi makubwa sana ya Pesa.
5. Awe anavaa mavazi yenye heshima yanayomstiri.
6. Awe anatoka familia ya wanaojiheshimu hasa dada zake wawe hawajawahi kubebeshwa mimba hovyo hovyo.
7. Awe na upendo wa kweli.
Yeremia 17:5-7 ''BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA. Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu. Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA, Ambaye BWANA ni tumaini lake.''
=Sifa za kiroho za mchumba anayekufaa wewe unayehitaji mchumba ni hizi;
1. Utii kwa MUNGU na Neno lake(Yakobo 4:7)
2. Awe na nia ya KRISTO ndani yake(Warumi 12:2)
3. Awe na hofu ya MUNGU(Mithali 8:13)
4. Awe Hana cha kumtenga na upendo wa MUNGU ulio katika KRISTO YESU(Warumi 8:35-39)
5. Amfanye KRISTO kuwa namba moja maishani mwake kabla hata ya wazazi au kabla ya huyo mchumba wake( Zaburi 34:8)
6. Awe mwana maombi(Waefeso 6:18)
7. Awe na kiasi na lugha nzuri(1 Petro 1:13-14)
8. Awe anavaa mavazi ya heshima kwa MUNGU na kwa wanadamu(Mathayo 11:8)
9. Awe ni mvumilivu na mkarimu(Yakobo 5:8-9)
10. Awe Mwaminifu kwa MUNGU na kwa wanadamu(Mithali 28:20)
Karibu tujifunze Neno la kutufanya tujue kile kitupasacho kujua.
Nimewahi kuulizwa swali hili zaidi ya mara kumi;
''Je nitamjuaje mchumba kutoka kwa MUNGU?''
''Je nifanyeje ili nijue kama huyu mchumba wangu ni chaguo la MUNGU kwangu au ni maamuzi yangu tu?''
''Nikitaka kupata Mke mwema/Mume mwema nifanyeje?''
Ni kweli kabisa haya ni moja ya mambo yanayowasumbua sana watu wengi sana.
Wengi hutamani kupata mke mwema lakini wao sio waume wema.
Wengi hutaka sana kupata waume wema lakini wao sio wake wema.
Kuna sifa nyingi ambazo mtu anayetaka kuoa/kuolewa huziangalia kwa huyo mwenzi.
Mithali 19:14 '' Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na BWANA.''
Mke mwema au mume mwema hutoka kwa MUNGU hakika.
Lengo la ujumbe wangu nataka ukaone tofauti hizi za kimwili au za kidunia na zile za kiroho. Baada ya kuzijua tofauti hizi basi unatakiwa utambue jinsi ya kubadili msimamo wako juu ya uchaguzi wako ili sasa umpate yule ambaye ana sifa za kiroho maana huyo ndio anastahili kwako.

Kama dada unamhitaji mume mwema basi hakikisha wewe unafaa kuwa mke mwema kwa maana umeokoka na unaishi kwa kulitii Neno la MUNGU ndipo na wewe upewe mume mwema.
Mithali 19:22-23 '' Haja ya mwanadamu ni hisani yake; Ni afadhali maskini kuliko mwongo. Kumcha BWANA huelekea uhai; Atakaa ameshiba; hatajiliwa na ubaya. ''
Hebu sasa ona tofauti hizi za uchaguzi wa wachumba kulingana na kundi la mtu anayechagua.
=Kijana wa kiume asiyemcha MUNGU akihitaji mchumba hutaka sifa zifuatazo zote au baadhi ya sifa hizi.
1. Umbo zuri linalosifiwa na marafiki zake.
2. Sura nzuri inayowafanya marafiki zake wamsifie kwamba amepata kifaa.
3. Msomi kama yeye.
4. Anatoka familia nzuri.
5. Anamjua MUNGU japokua yeye muoaji ni mpagani.
6. Tabia nzuri japokua yeye muoaji hana tabia nzuri hata moja.
7. Atembee nae kwanza ili aone kama anafaafaa kumbe ni dhambi na hatari sana ya kuuvunja uchumba kabla hata ya ndoa.
Mithali 31:10 ''Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani. ''
=Binti asiyemcha MUNGU akihitaji mchumba hutaka sifa zifuatazo zote au baadhi ya sifa hizi.
1. Awe na pesa za kutosha zitakazomtosha katika mahitaji yake yote 100%.
2. Humtaka kijana aliyeokoka wakati yeye hajaokoka.
3. Awe Handsome na mchangamfu.
4. Awe na uwezo wa kumlinda hivyo awe na ka mwili kanakoweza kumpiga mtu mwingine kama atamchokoza huyo binti.
5. Awe na kazi nzuri sio tu kazi za ajabu ajabu.
6. Awe na elimu nzuri kuliko wote watakaomfuata.
7. Awe na usafiri au awe na mpango wa kununua usafiri mzuri.
Waebrania 13:4-6 '' Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi MUNGU atawahukumia adhabu. Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa. Hata twathubutu kusema, BWANA ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini? ''
=Binti aliyeokoka anapompenda mvulana hupendelea sifa hizi;
1. Awe anamjua MUNGU na ana hofu ya MUNGU.
2. Awe na kazi nzuri na huduma nzuri.
3. Awe na muonekano mzuri na mtanashati.
4. Awe na tabia nzuri na msimamo mzuri
5. Awe na lugha nzuri katika kinywa chake.
6. Awe na historia nzuri ya mwanzo.
7. Awe anakubarika kwa mchungaji.
Isaya 55:8-9 ''Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA. Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.''
=Kijana wa kiume aliyeokoka sifa anazopendelea kwa binti ni hizi;
1. Awe ameokoka kweli kweli kama yeye.
2. Awe ni mpole, mtii na mnyenyekevu na msikivu na mwelewa.
3. Awe na sura nzuri na muonekano kuwazidi wengine wote kanisani kwao.
4. Awe hana matumizi makubwa sana ya Pesa.
5. Awe anavaa mavazi yenye heshima yanayomstiri.
6. Awe anatoka familia ya wanaojiheshimu hasa dada zake wawe hawajawahi kubebeshwa mimba hovyo hovyo.
7. Awe na upendo wa kweli.
Yeremia 17:5-7 ''BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA. Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu. Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA, Ambaye BWANA ni tumaini lake.''
=Sifa za kiroho za mchumba anayekufaa wewe unayehitaji mchumba ni hizi;
1. Utii kwa MUNGU na Neno lake(Yakobo 4:7)
2. Awe na nia ya KRISTO ndani yake(Warumi 12:2)
3. Awe na hofu ya MUNGU(Mithali 8:13)
4. Awe Hana cha kumtenga na upendo wa MUNGU ulio katika KRISTO YESU(Warumi 8:35-39)
5. Amfanye KRISTO kuwa namba moja maishani mwake kabla hata ya wazazi au kabla ya huyo mchumba wake( Zaburi 34:8)
6. Awe mwana maombi(Waefeso 6:18)
7. Awe na kiasi na lugha nzuri(1 Petro 1:13-14)
8. Awe anavaa mavazi ya heshima kwa MUNGU na kwa wanadamu(Mathayo 11:8)
9. Awe ni mvumilivu na mkarimu(Yakobo 5:8-9)
10. Awe Mwaminifu kwa MUNGU na kwa wanadamu(Mithali 28:20)
Comments