![]() |
Na Mtumishi Generali Geoffrey Mwanza |
Karibu kujifunza.
Wakati umewadia; nikupe tena wosia;
Ni lini utasikia;nikishakwambia;
Maonyo umesikia;na bado wanililia;
Siyo yote ni Makanisa;mengine ni makaburi.
Dhambi yashabikiwa;na bado Bwana asifiwe,
Ni wapi karuhusiwa;dhambi ishabikiwe,
Miujiza mwauziwa;haja yenu mbarikiwe,
Siyo yote ni Makanisa;mengine ni makaburi.
Usipoiacha dhambi;jehanamu yakungojea,
Sio moto wa tambi;siku zinasongea,
Usiifiche dhambi; maana inaongea,
Siyo yote ni Makanisa;mengine ni makaburi.
Nilichokutabiri; sasa kinatendeka,
Ili upate kukiri;na kweli utaanguka,
Rudia MUNGU si siri;na utakubalika,
Siyo yote ni Makanisa; mengine ni makaburi.
Achana navyo vitisho; kitambo nilikuonya,
Shetani anao mwisho;na sasa mekutawanya,
Itakuwa thibitisho; tena hamna mwanya,
Siyo yote ni Makanisa;mengine ni makaburi.
Generali nimemaliza; mie mwana wa Mwanza,
Yesu anakuwaza;moyo wako aupate kwanza,
Safari imeanza;tafuta ufalme kwanza,
Siyo yote ni Makanisa; mengine ni makaburi.
Imetungwa nami Generali Geoffrey Mwanza nikila lunch mahali tu nikahisi ujumbe umenijia (13:37pm)
Ubarikiwe sana ndugu mpendwa na kama hujaokoka; okoka sasa hivi.
Ni lini utasikia;nikishakwambia;
Maonyo umesikia;na bado wanililia;
Siyo yote ni Makanisa;mengine ni makaburi.
Dhambi yashabikiwa;na bado Bwana asifiwe,
Ni wapi karuhusiwa;dhambi ishabikiwe,
Miujiza mwauziwa;haja yenu mbarikiwe,
Siyo yote ni Makanisa;mengine ni makaburi.
Usipoiacha dhambi;jehanamu yakungojea,
Sio moto wa tambi;siku zinasongea,
Usiifiche dhambi; maana inaongea,
Siyo yote ni Makanisa;mengine ni makaburi.
Nilichokutabiri; sasa kinatendeka,
Ili upate kukiri;na kweli utaanguka,
Rudia MUNGU si siri;na utakubalika,
Siyo yote ni Makanisa; mengine ni makaburi.
Achana navyo vitisho; kitambo nilikuonya,
Shetani anao mwisho;na sasa mekutawanya,
Itakuwa thibitisho; tena hamna mwanya,
Siyo yote ni Makanisa;mengine ni makaburi.
Generali nimemaliza; mie mwana wa Mwanza,
Yesu anakuwaza;moyo wako aupate kwanza,
Safari imeanza;tafuta ufalme kwanza,
Siyo yote ni Makanisa; mengine ni makaburi.
Imetungwa nami Generali Geoffrey Mwanza nikila lunch mahali tu nikahisi ujumbe umenijia (13:37pm)
Ubarikiwe sana ndugu mpendwa na kama hujaokoka; okoka sasa hivi.
Comments