DONDOO KUTOKA KWA DK MITIMINGI KUHUSU UCHUMBA NA NDOA.

Mchungaji Dk Peter Mitimingi
SIFA ZA MSICHANA ILI AWEZE KUOLEWA!
Katika agano la kale ili msichana aweze kuolewa ilikuwa lazima awe na sifa zifuatazo:

1. UZURI WA USO WAKE (“Naye yule msichana alikuwa mzuri sana uso wake)
2. AWE NI MSICHANA BIKIRA (bikira, wala mwanamume hajamjua bado).
3. AWE MSICHANA CHAPA KAZI ZA MIKONO (akashuka kisimani, akajaza mtungi wake, akapanda.”)

Mwanzo 24:16“Naye yule msichana alikuwa mzuri sana uso wake, bikira, wala mwanamume hajamjua bado; akashuka kisimani, akajaza mtungi wake, akapanda.”
Katika ziku hizo sifa kuu za msichana zilikuwa zinaangaliwa katika maeneo haya matatu:

Wadada mpo hapooo!!



 WACHUMBA WASIFANYE MIPANGO WALA MIRADI YA KIPESA KATIKA KIPINDI CHA UCHUMBA MPAKA WATAKAPOKUWA WAMEOANA TAYARI.
1. Msichange na kununua gari lenu mkiwa wachumba
2. Msichange na kununua shamba, kiwanja au nyumba yenu mkiwa wachumba.
3. Msianzishe biashara ya pamoja mkiwa wachumba.
4. Msikopeshane kiwango kikubwa cha pesa mkiwa wachumba.
5. Msishirikiane kukopa kiwango kikubwa Bank au kwenye taasisi za fedha mkiwa wachumba.
6. Haishauriwi kabisa kwa watu ambao ni wachumba kushirikiana kifedh na mipango iliyotajwa hapo juu wakati wakiwa ni wachumba. Mambo hayo hapo juu yanapaswa yafanywe na watu ambao tayari ni wanandoa.
7. Uchumba sio ndoa, hauna "garantee" wala hauna mashiko. Unaweza kuvunjika dakika yoyote ile na kama mlikuwa mmesha wekeza kila mmoja kwa mwenzake kwa kuamini kwamba si mtakuja kuoana, uzoefu unaonyesha kwamba mara nyingi mmoja kati ya wachumba hao ambaye mali ilikuwa imeandikishwa kwa jina lake huishia na mali ile na kumdhurumu mwenzake bila kujali kwamba mali hizo walikuwa wamechanga wote wawili wakati ule wa mapenzi moto moto na kuacha jeraha na maumivu makubwa sana kwa mmoja aliyedhurumiwa kitu ambacho kama hakitashughulikiwa vizuri katika ushauri "counseling" huweza kuleta athari za kimahusiano kwa mchumba atakayefuata na hata mwanandoa atakaye oana naye ataumizwa kwasababu ya lile jeraha la kudhurumiwa ambalo mchumba alitoka nalo kule.


 MAMBO YA VIJANA KUJITAYARISHA KINYUME NA MATARAJIO: (The unexpected)
Utachukua hatua gani kama jambo hili litajitokeza katika ndoa yako Baada ya Kuona?
1. Unagundua kuwa hauwezi kupata watoto.
2. Mwenza wako anaugua na kuumwa sana.
3. Anakosa kazi au amefirisika sana.
4. Mnahitajika kuhamia katika makazi ambayo ni ya hadhi ya chini sana.
5. Analazimmika huhamia katika nchi au mji hatarishi.
6. Anakumbwa na hali ngumu sana ya kiuchumi.
7. Kifo cha mtoto.
8. Ukagundua kuwa mwenza wako sio mwaminifu kwako.
9. Mwenza wako amepoteza kiungo fulani.
10. Unakuja kubaini kumbe mwenza wako anajihusisha na shughuli haramu kama:
• Ujambazi
• Uchawi
• Kuuza madawa ya kulevya
• Kununua na kuuza viungo vya binadamu nk.


UMUHIMU WA WANANDOA KUTUMIA MUDA PAMOJA NA KUWEKA MIKAKATI - TIME SPENT TOGETHER
1. Ni kwanjia gani mtatumia muda pamoja
2. Muda wa mke na mume wawili tu
3. Muda wa mke mume na watoto.
4. Muda wa mume na watoto tu
5. Muda wa mke na watoto tu.
6. Muda wa watoto peke yao tu.
7. Muda wa mume, mke, watoto wao na watoto wengine.

Ni muhimu sana kutenga muda kama huu wa kuwa na "time together" na mwenzi wako na familia yako kwa ujumla.
Mara nyingi unahitaji kupanga na sio kusubiria nafasi ijitokeze maana huenda isijitokeze nafasi kama hiyo maana mambo ni mengi na yote yanahitaji pesa hivyo inahitaji kuamua na kujipanga na kulazimisha vinginevyo haitawezekana.

 KWA HUDUMA ZA USHAURI WASILIANA NAMI
Counseling Psychologist - Dr. Mitimingi - 0713 18 39 39

Comments