MACHO YAKO YANAONA SAHIHI?

Na Mtumishi Dr. Frank P. Seth
“BWANA akamtokea Ibrahimu karibu na mialoni ya Mamre, alipokuwa ameketi mlangoni pa hema yake mchana wakati wa hari. Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Naye alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi, akasema, Bwana wangu, kama nimeona fadhili machoni pako nakuomba usinipite sasa mimi mtumwa wako. Na yaletwe basi maji kidogo mkanawe miguu, mkapumzike chini ya mti huu. Nami nitaleta chakula kidogo, mkaburudishe moyo, baadaye mwendelee, iwapo mmemjia mtumwa wenu. Wakasema, Haya, fanya kama ulivyosema. Basi Ibrahimu akaenda hima hemani kwa Sara, akasema, Himiza vipimo vitatu vya unga safi, uukande, ufanye mikate. Ibrahimu akapiga mbio kwenda kundini, akaleta ndama wa ng’ombe aliye laini, mzuri, akampa mtumishi, naye akahimiza kuiandaa. Akatwaa siagi na maziwa, na ndama aliyoiandaa, akawaandikia mbele yao, akasimama karibu nao chini ya mti, nao wakala. Wakamwambia, Yu wapi Sara mkeo? Akasema, Yumo hemani. Akamwambia, Hakika nitakurudia wakati huu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake. Basi Ibrahimu na Sara walikuwa wazee, na umri wao mkubwa, na Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake. Kwa hiyo Sara akacheka moyoni mwake, akisema, Niwapo mkongwe, nitapata furaha, na bwana wangu mzee? BWANA akamwambia Ibrahimu, Mbona Sara amecheka akisema, Mimi kweli nitazaa mwana, nami ni mzee? Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume. Akakana Sara, akisema, Sikucheka, maana aliogopa. Naye akasema, Sivyo, umecheka.”
‭‭MWA.‬ ‭18:1-15‬ ‭SUV‬‬

Fikiri nyumbani mwako wanakuja wageni watatu, mume anawaita jina moja "Bwana" kwa sababu haoni watatu ila anamwona Bwana! Ghafla! Anawasujudia hata nchi...na kuanza kukimbia mbio huku na kule kuwahudumia. Ibrahim alifanya mwenyewe uchaguzi wa aina ya chakula na akaamuru waandaliwe hicho chakula halafu akawapa yeye...hiki ni kiwango kikubwa cha heshima!
Angalia mkewe. Muda wote mama anaona watu watatu na sio Bwana! Wala hakujua kwamba ni wakati wa kupokea muujiza wake. Anacheka moyoni mwake kwa sababu "hawa watu" wanazungumza mambo yasiyowezekana....Sara anajua siku zake zimekoka....hawa wageni hawajui chochote....maana Sara aliona watu sio Bwana! Hata hao wageni walipomjibu kama Bwana, bado hakuelewa, akajikuta anabishana na Mungu...Bwana anaona Sara amecheka, japo alicheka moyoni ...kwa sababu Sara hakucheka kwa sauti...Sara alijua hakuna "mtu" ameona hiyo...akabisha...Muda wote huu hakujau aliyekuja kwake ni Bwana!
Kwanini Sara hakujiuliza sababu za mumewe kuwa na mapokezi yasiyo ya kawaida? Gahfla mzee Ibrahim anakimbia hovyo, anawasujudia, anakuwa na adabu isiyo ya kawaida. Ibrahim Anajiita kwao "mtumwa"! Je! Macho ya Sara yaliluwa yanaona nini?
Unaweza kumlaumu Mungu kwa kuchelewesha muujiza wako, kumbe! Kila akija kwako anakukuta na hali ya Sara, Unamchukulia Mungu "powa"! Unacheka! Unafanya mambo kama uko na shemeji zako, unabisha tu na kuleta mzaha! Kumbe, uwaonao mbele zako ndio waleta muujiza wenyewe. Je! Macho yako yanaona sawa?
Mara nyingi kwenye maisha yetu tumedhani kwamba mambo yanayotuathiri ni yale ambayo watu wanajua! Kwa hiyo ukiweza kufuta mdomo vizuri unajifariji uko salama! Sara akabisha...swali ni Je! Unaona sawa sawa?
Frank P. Seth

Comments