MAOMBI YA KUHARIBU KAMBI ZOTE ZA MAADUI ZAKO.

Na Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.

Shalom Mteule wa KRISTO upendwaye sana na MUNGU Baba.
Namshukuru MUNGU sana maana hili ni somo langu la 600 Tangu nimeanza kufundisha Mtandaoni Mwishoni mwa mwaka 2012.
Haikuwa rahisi lakini kwa JEHOVAH imewezekana.
Natambua kabisa ''Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema BWANA  wa majeshi.-Zakaria 4:6'
Natambua Kibinadamu nimetumia gharama nyingi mno, nimetumia muda mwingi mno na vita ni kali  Lakini Bwana YESU aliye Mwokozi wangu na ambaye mimi siku zote humhubiri yeye, anasema ''Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, BABA atamheshimu.-Yohana 12:26''  
Kama umebarikiwa na masomo yangu MUNGU akubariki sana na hata ukipenda kunisapoti MUNGU akubariki sana sana.
Baada ya hayo karibu sasa tujifunze Neno la MUNGU la zamu ya leo la kuhusu maombi kisha tuombe maombi ya ushindi mkuu sana.
Ni siku chache zimepita ambapo katika maombi usiku nilisikia sauti rohoni mwangu ikisema tuombe kuharibu kambi za maadui zetu wote katika ulimwengu wa roho.
Leo kabla ya kukuandikia somo hili niliangalia Kamusi  ili kupata kujua maana ya neno ''Kambi'' na nimekuta Neno hilo lina maana hizi;
=Kambi ni mahali msafara fulani unapotua.
=Kambi ni makao ya muda ya vikundi vya watu.
=Kambi ni malago yaani ni mahali ambapo watu hukaa kwa muda kwa ajili ya kufanya kazi maalumu.
Kumbuka kwamba mambo yote huanzia katika ulimwengu wa roho kabla ya kuja kutimia katika ulimwengu wa mwili.
Kama watu wa MUNGU ni lazima sana kupigana vita ya kiroho ndipo tutashinda, kumbuka '' Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)-2 Kor 10:3-4'' 
Kumbe ni lazima sana tupambane katika ulimwengu wa roho maana kuna maadui wengi na hao wakati mwingine huweka kambi kuhakikisha hatufanikiwi katika mipango yetu au maisha yetu au huduma zetu. Biblia inatujulisha juu ya maadui hao.
Waefeso 6:11-22 '' Vaeni silaha zote za MUNGU, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.''
Kumbe ni lazima sana kuwa na silaha za kiroho.
Tunao maadui wengi sana na hao huweka kambi katika sehemu za karibu na vitu vyetu ili watuharibie, Leo tunaharibu kambi zao zote kwa jina la YESU KRISTO.
Kuna maadui wanaoitwa majeshi ya pepo wabaya, hao pepo wabaya wakati mwingine huwaingia watu ili hao watu watumike kishetani ili kutudhuru, leo kambi zao tunaziharibu kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina kuu la YESU KRISTO.
Kuna falme za shetani, kuna mamlaka za kipepo na kuna wakuu wa giza, hao wote ni maadui zetu na vita hiyo hupiganwa katika ulimwengu wa roho. Leo hakikisha hakuna kambi ya adui zako inabaki bila kuharibiwa.
Ukifungua biashara katika eneo ambalo mkuu wa giza ameweka kambi hakika huwezi kufanikiwa hadi pale ambapo utaweza kuiharibu kambi yake kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Wachawi wakiweka kambi katika ndoa yako, uchumba wako, afya yako au uchumi wako unatakiwa uiharibu kambi yao ndipo utapata furaha njema na mafanikio uyatakayo.
Mapepo yakiweka kambi katika mwili wako itakuwa vigumu wewe kumtii MUNGU, Utakuwa na maamuzi ya kishetani kwa sababu mashetani wamepiga kambi ndani yako.
Ndoa fulani ilikuwa na mgogoro mkubwa sana kwa sababu tu shetani alikuwa amepiga kambi katika ndoa hiyo kwa kupitia msichana wa kazi(House girl)
Ndugu leo haribu kambi za maadui zako wote katika ulimwengu wa roho.
Hebu tuone Biblia inasemaje juu ya kambi za maadui;
Waamuzi 7:7-14 ''BWANA akamwambia Gideoni, Kwa watu hawa mia tatu walioyaramba maji nitawaokoa, nami nitawatia Wamidiani katika mikono yako; lakini watu hawa wote wengine na waende zao, kila mtu mahali pake. Basi wale watu wakachukua vyakula vyao mikononi mwao, na tarumbeta zao; naye akawapeleka watu wote wa Israeli, kila mtu hemani kwake; bali aliwazuia wale watu mia tatu; na KAMBI YA  Wamidiani ilikuwa chini yake, bondeni. Ikawa usiku uo huo BWANA akamwambia, Ondoka, shuka KAMBINI; maana nimeitia katika mikono yako. Lakini, ukiogopa kushuka, shuka pamoja na Pura mtumishi wako KAMBINI; nawe utasikia wanayoyasema, na baada ya haya mikono yako itatiwa nguvu; ushuke KAMBINI. Ndipo akashuka pamoja na Pura mtumishi wake hata kufikilia mwisho wa watu wenye silaha waliokuwa KAMBINI. Nao Wamidiani na Waamaleki na, hao wana wa mashariki walikuwa wametua bondeni, mfano wa nzige kwa wingi; na ngamia zao walikuwa hawana hesabu; mfano wa mchanga wa ufuoni, kwa wingi. Hata Gideoni alipofika, tazama, palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa akimhadithia mwenziwe ndoto, akasema, Tazama, naliota ndoto, na tazama, mkate wa shayiri ulianguka katika KAMBI YA Wamidiani, ukafika hata hema moja, ukaipiga hata ikaanguka, nao ukaipindua, hata ikalala chini. Mwenzake akamjibu akasema, Habari hii haikosi kuwa upanga wa Gideoni, mwana wa Yoashi, mtu wa Israeli. MUNGU amewatia Wamidiani na jeshi lote katika mkono wake.''
Ukiendelea kusoma maandiko yanayofuata utagundua kwamba kambi ile ya wamidiani ambao walikuwa maadui wa waisraeli iliharibiwa na wamidiani wakashindwa katika vita.
Tunajifunza nini?
Kwanza kambi ya wamidiani kama maadui ilikuwa bondeni, Kambi ya maadui zako leo iko wapi katika maisha yako?
Shetani anaweza akakusanya watu  na watu hao wakaweka kambi ili kukuzimisha, leo futa kambi za maadui zako kwa maombi.
Ngoja nikupe siri hii; Wakati mwingine umewapiga maadui zako kwa maombi na wakakimbia, na baada ya muda wanarudi tena unawapiga. Unaweza ukamaliza mwaka unapigana na adui mmoja tu ambaye akija unampiga anakimbia kisha baadae atarudi tena. Kwanini inakuwa hivyo?
Ni kwa sababu ukimpiga huyo adui hukimbilia kambini kujipanga na ndio maana huwa unamuona anarudi tena.
Dawa ni kuiharibu kambi nzima ya adui huyo ndipo hatarudi tena kwako maana ukimpiga akikimbilia kambini atakuta na kambi umeiharibu yote kwa damu ya YESU.
Hata wafanya kazi wenzako wanaweza kugeuka kambi ya kukujadili ili wakuharibie kazi yako kwa wewe kufukuzwa au kusimamishwa kazi, leo haribu kambi za maadui zako wote katika ulimwengu wa roho.
Leo haribu kambi zote za wanaokuendea kwa waganga wa kienyeji.
Ni kina nani wamepiga kambi  ili kuhakikisha uchumba wako unakufa?
Ni akina nani wamepiga kambi ili kuhakikisha huoi au huolewi?
Ni akina nani wamepiga kambi ili kuhakikisha ndoa yako inakufa?
Kumbuka kambi ni jambo maalumu la muda maalumu katika kipengele maalumu, Hivyo unaweza ukapanga mipango fulani ya kuitekeleza mwaka huu, lakini mawakala wa shetani baada ya kujua mipango yako huweka majini ili kuhakikisha katika hayo hufanikiwi. Ndio maana unashangaa mipango yako ya kila mwaka haifanikiwi yote au katika mipango saba wewe hufanikiwa katika mpango mmoja tu. Ndugu hao maadui walioweka kambi kuhakikisha mipango yako haifanikiwi hakikisha unaharibu kambi zao kwa jina la YESU KRISTO na kwa damu ya YESU KRISTO.
Najua naongea na wateule wa MUNGU hapa wenye mipango mizuri kwa utukufu wa MUNGU.
Kama hujaokoka kwanza okoka ndugu.
Ni akina nani wamepiga kambi  ili kuhakikisha familia yenu inasambaratika?
Leo ita damu ya YESU KRISTO ili kuziharibu kambi za maadui zako hao kwenye ulimwengu wa roho.
Ita jina la YESU KRISTO utashinda na tumia Neno la KRISTO ili kuharibu kambi zote za kipepo zinazopanga mabaya dhidi yako.
Hebu ona hili;
1 Samweli 17:4-11 ''Ndipo akatoka shujaa katika KAMBI YA  Wafilisti, aliyeitwa Goliathi, wa Gathi, ambaye urefu wake ulikuwa mikono sita na shibiri moja. Alikuwa na chapeo ya shaba kichwani, tena amevaa darii ya shaba; na uzani wake ile darii ya shaba ulikuwa shekeli elfu tano za shaba. Tena amevaa mabamba ya shaba miguuni mwake, naye alikuwa na mkuki wa shaba kati ya mabega; yake. Na mti wa fumo lake ulikuwa kama mti wa mfumaji; na kichwa cha mkuki wake kilikuwa shekeli mia sita za chuma uzito wake; na mtu aliyemchukulia ngao yake akamtangulia.  Naye akasimama, akawapigia kelele majeshi ya Israeli akawaambia, Mbona mmetoka kupanga vita? Je! Mimi si Mfilisti, na ninyi si watumishi wa Sauli? Jichagulieni mtu, akanishukie mimi. Kama akiweza kupigana nami na kuniua, sisi tutakuwa watumwa wenu; nami nikimshinda yeye na kumwua, ninyi mtakuwa watumwa wetu, na kututumikia. Yule Mfilisti akasema, Nayatukana leo majeshi ya Israeli; nipeni mtu tupigane. Basi Sauli na Israeli wote waliposikia maneno hayo ya Mfilisti, wakafadhaika na kuogopa sana.'
Kutoka katika Kambi ya wafilisti ambao wallikuwa maadui za waisraeli alitokea shujaa aitwaye goliathi. Ukiendelea kusoma utaona jinsi ambavyo adui aliyetoka katika kambi ya wafilisti aliuawa na kijana Daudi aliyekuwa anamtegemea MUNGU.
1 Samweli 17:42-51 '' Hata Mfilisti alipotazama huku na huku, akamwona Daudi akamdharau; kwa kuwa ni kijana tu mwekundu, tena ana sura nzuri. Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake. Mfilisti akamwambia Daudi, Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni. Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la BWANA wa majeshi, MUNGU wa majeshi ya Israeli uliowatukana. Siku hii ya leo BWANA atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko MUNGU katika Israeli. Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba BWANA haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya BWANA, naye atawatia ninyi mikononi mwetu. Ikawa, hapo Mfilisti alipojiinua, akaenda akamkaribia Daudi, ndipo Daudi naye akapiga mbio, akalikimbilia jeshi ili akutane na yule Mfilisti. Daudi akatia mkono wake mfukoni, akatwaa humo jiwe moja, akalitupa kwa kombeo lake, akampiga Mfilisti katika kipaji cha uso; jiwe hilo likamwingilia kipajini, akaanguka chini kifudifudi. Hivyo Daudi akamshinda yule Mfilisti kwa kombeo na jiwe, akampiga Mfilisti, akamwua; walakini Daudi hakuwa na upanga mkononi mwake. Ndipo Daudi akapiga mbio, akasimama juu ya Mfilisti, akautwaa upanga wake, akaufuta alani mwake, akamwua, akamkata kichwa kwa upanga huo. Nao Wafilisti walipoona ya kuwa shujaa wao amekufa, wakakimbia. ''
Kutoka katika kambi ya wafilisti alipouawa shujaa wao wafilisiti walikimbia na kambi yao ikafutika na wao kutawanyika na vita ikaisha.
Kumbuka habari kama hizi za Waisraeli na za agano la kwanza na za akina Gideoni na akina Daudi ziliandikwa ili kutusaidia sisi tuliofikiliwa na miisho ya zama hizi.
1 Kor 10:11 '' Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.''
 Akina Gideoni waliziharibu kambi za maadui zao katika ulimwengu wa mwili lakini sisi tunaharibu kambi za maadui zetu katika ulimwengu wa roho.
Ni vyema sana maadui wote katika kambi za shetani waharibiwe ndipo maadui wataachia baraka zetu.
Leo haribu kambi zote za maadui zako katika ulimwengu wa roho.
Katika kambi za kipepo kuna mipango inapangwa kukuhusu.
Katika kambi za kipepo wanaweza kuwa hata na nguo yako ya ndani au kitu chako chochote walichochukua ili kwa hicho wakupate vyema kwenye kusudio lao, Leo haribu kambi zote za maadui zako wote katika ulimwengu wa roho.
Maombi haya naomba yamsaidie muombaji mchanga ili ajue kuomba akiliendea hitaji lake binafsi.
Kwa waombaji wazoefu naamini baada tu ya kujifunza amejua aharibu wapi katika kambi za maadui zake.
Pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA  kinakaribia kutoka ila napungukiwa na pesa ya kukichapisha, ukiguswa unaweza kunisadia na kitabu hicho kitawasaidia maelfu ya watu.

MAOMBI YA KUHARIBU KAMBI ZA MAADUI WOTE WA ROHONI.

Nakutukuza BABA wa mbinguni maana wewe u mwema kwangu.
Nakushukuru umenipa uzima na umenipa nafasi hii ya kuomba kwako kupitia jina la YESU KRISTO.
MUNGU wangu naomba unisamehe na unitakase mwili wangu, nafsi yangu na roho yangu katika jina la YESU KRISTO Mwokozi wangu. Nipe kuishi maisha matakatifu ya wokovu wa KRISTO YESU Mwana wako wa pekee.
Kila kambi ya kipepo iliyokaa ili kuniharibia katika jambo lolote naiharibu kwa jina la YESU KRISTO.
Kila adui aliyeweka kambi katika mwili wangu hata nateseka kwa magonjwa, sasa hivi naiharibu kambi yake kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila adui aliyeweka kambi katika kazi yangu au biashara yangu, leo naiharibu kambi hiyo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila mganga au mchawi aliyetuma majini ili yaweke kambi katika ndoa yangu, uchumba wangu, uzao wangu au chochote changu,  sasa naharibu kambi hizo na kuzitoweshwa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Walioweka kambi kazini kwangu ili nisipande cheo, naiharibu kambi yao na kuifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO. Na sana napanda cheo  kwa jina la YESU KRISTO.
Kila kambi ya shetani iliyowekwa katika maisha yangu  naiharibu yote kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila kambi ya shetani iliyowekwa  kwenye sura yangu naiharibu  kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila kambi ya wachawi iliyowekwa kwa  Mke/Mume wangu
naiharibu yote kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila kambi ya wachawi iliyowekwa katika tumbo langu la uzazi 
naiharibu yote kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila kambi ya kipepo iliyowekwa katika mwili wangu naiharibu yote kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila kambi ya kishetani iliyowekwa katika kazi yangu naiharibu yote kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila kambi ya maadui zangu iliyowekwa katika kipato changu na uchumi wangu naiharibu yote kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila kambi ya shetani iliyowekwa katika ufahamu wangu naiharibu yote kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila kambi ya shetani iliyowekwa kwa wazazi wangu hata hatuelewani naiharibu kambi hiyo yote kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila kambi ya shetani iliyowekwa katika uchumba wangu ili ufe naiharibu yote kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila kambi ya shetani iliyowekwa katika huduma yangu na kanisa naiharibu yote kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila kambi ya shetani iliyowekwa katika ardhi au bahari  ili kunidhuru  naiharibu yote kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila kambi ya shetani kokote iliko katika maisha yangu
naiharibu yote kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Katika jina la YESU kila kambi za maadui zangu zimeharibika na kwa njia hiyo hakuna kitu kibaya chochote kitakachonipata kutoka kwao.
Nakushukuru JEHOVAH MUNGU wangu maana umenishindia.
Katika jina la YESU KRISTO nimeomba na kupokea ushindi.
 Amen Amen.


Asante kama umelielewa Neno la MUNGU ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa BWANA YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.

Comments