JINSI YA KUACHA UZINZI NA UASHERATI

Na Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.

Bwana YESU atukuzwe ndugu yangu.
Karibu tujifunze Neno la MUNGU.
'' Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.-1 Kor 6:18''
Hakuna namna bali amri ya MUNGU ni kila mwanadamu kuikimbia zinaa.
Zinaa ni nini?
Zinaa ni tendo la uasherati, ni tukio la uasherati na ni matendo ya uzinzi na uasherati.
Uasherati ni tabia ya kupenda kuzini.
Uzinzi ni matendo ya kuzini.
Mwasherati ni mtu yeyote ambaye hajaoa au kuolewa akifanya uzinifu.
Mzinzi ni mwanandoa akitoka nje ya ndoa yake kwenda kuzini.
Adhabu ya MUNGU kwa wazinzi na waashwrati wasiotubu na kuacha uovu wao huo ni jehanamu ya moto.
1 Kor 6:9 ''Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa MUNGU? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa MUNGU, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,''  

Kuna maroho mengi yanawatesa watu, mojapo ya maroho hayo ya shetani ni roho ya zinaa.
Roho ya zinaa ni roho ya shetani inayoingia kwa mtu ambaye hana YESU. Ni mapepo kama yalivyo mapepo mengine ambayo tuyatoa ndani ya watu kila Leo. 
Kama kuna mtumishi ni mzinzi basi anatakiwa ajiulize kwamba yeye ni mtumishi wa nani? Mtumishi wa YESU KRISTO hawi hivyo. 
Kama kuna Mkristo anayemtumikia MUNGU na  ni msaliti wa ndoa yake anatakiwa ajitambue kwamba yeye ni mtumishi hewa na sio mtumishi kamili. 
Kama kuna Mristo  ni mzinzi basi huyo yuko katika kundi la "Sio wote waitao Bwana Bwana wakaouridhi uzima wa milele" anatakiwa ahame kundi hilo upesi sana maana muda wa hukumu u karibu sana. Unaweza ukawadanganya wanadamu lakini sio MUNGU. Mkristo  kama huyo anaweza akawahadaa waumini lakini sio MUNGU.
1 Thesalonike 4"1-5 ''Iliyobaki, ndugu, tunakusihini na kuwaonya kwamba mwenende katika Bwana YESU; kama mlivyopokea kwetu jinsi iwapasavyo kuenenda na kumpendeza MUNGU, kama nanyi mnavyoenenda, vivyo hivyo mpate kuzidi sana. Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana YESU. Maana haya ndiyo mapenzi ya MUNGU, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati; kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;  si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua MUNGU.'' 
 
Ndugu zangu naomba tujue hili;
 Dhambi ya uzinzi wala sio ya kuikemea Bali ni ya kuikimbia na kuamua maamuzi magumu ya kujitenga na uzinzi. Kama wewe ni mwanaume Mkristo lakini umeng'ang'aniwa na  mwanamke Mzinzi basi naomba utambue kwamba huo ni mnyororo umekufunga ili kukupeleka jehanamu, badilika Leo ndugu. Natamani fahamu zako zilizoibiwa na huyo mwanamke zikurudie ili ujue kilichoko mbele yako. 
Kama wewe ni Mwanamke Mkristo lakini umenasa kwenye mtego wa mwanaume mzinzi naomba utambue kwamba chatu kuzimu ameacham ili kukumeza, geuka Leo ndugu maana mwisho u karibu.
 MUNGU akubariki kama umeelewa Ujumbe huu kwamba umeletwa kwako Leo ili kukurudusha kwa Bwana YESU mwenye uzima wako. Nakuonya ndugu geuka kutoka dhambini na anza kumtii KRISTO.
Waefeso 5:3 '' Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu; ''

Leo katika jamii kuna mambo mengi yaliyopo ndiyo yanachangia pia kuwakosesha na kuwafanya watende dhambi.
Simu yako usipoitumia vizuri inaweza kugeuka mungu wa kihindi kwako.
Umeweka password kwenye message, kwenye picha na kila sehemu kwa sababu tu njia zako haziko sawa mbele za MUNGU.
Mume unaenda kuoga bafuni na simu ili tu mke wako asione uovu wako.
Mke unaweka simu silent kipindi mumeo akiwa nyumbani kwa sababu njia zako ni mbaya.

Ndugu unaweza ukamficha mwanadamu lakini sio MUNGU.
Dhambi yako haitaondoka mpaka utakapotubu na kuacha uovu wako.
Mhubiri 12:14 '' Kwa maana MUNGU ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.''

Katika kuepukana na uasherati Ndugu napenda kukushauri pia kwamba usipende kukaa muda mrefu bila jambo jema la kiMUNGU la kufanya.
Jifunze kwa Daudi.
2 Wafalme 11:1-5 ''Hata ikawa, mwanzo wa mwaka mpya, wakati watokapo wafalme kwenda vitani, Daudi akampeleka Yoabu, na watumishi wake pamoja naye, na Israeli wote; wakawaangamiza wana wa Amoni, wakauhusuru Raba. Lakini Daudi mwenyewe akakaa Yerusalemu. Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho. Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bath-sheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti?
Basi Daudi akapeleka wajumbe, akamtwaa; naye akaingia kwake; naye akalala naye; (maana yule mwanamke amekwisha kutakasika unajisi wake); kisha akarudi nyumbani kwake. Yule mwanamke akachukua mimba; basi akapeleka na kumwambia Daudi, akasema, Ni mja-mzito.''


Huyu Daudi alikosea kwa sababu ya mapumziko yasiyo sahihi na yasiyo na maana. Dhambi yake ilileta adhabu kwake kutoka kwa MUNGU.
Point yangu ni kwamba Mapumziko ya haraka na kukosa uvumilivu wakati mwingine yanaweza kumfanya mtu akatenda dhambi.
Vijana wengi wametenda dhambi kwa sababu ya kukosa uvumilivu.
Kuna vijana kama wangevumilia kidogo tu hakika MUNGU angewapa baraka zao.
Dhambi ndizo huwafanya watu wengi kupishana na baraka zao.
Kukosa uvumilivu ndiko huwafanya vijana wengi kupishana na baraka zao.
Mpango wa MUNGU ni kumngoja yeye hadi wakati timilifu.

Unaweza kumuona mtu anatembea njiani lakini amekufa kirohokwa sababu ni mzinifu.
Unaweza kumwona mtu anaimba lakini amekufa kiroho kwa sababu ni mwasherati.
Unaweza ukamuona mtu anahubiri ana kufundisha lakini amekufa kiroho kwa sababu ni mzinzi.
Unaweza kumwona mtu ni kiongozi mzuri kanisani lakini amekufa kiroho ni mzinzi.
Unaweza kumwona mtu ana hekima sana lakini rohoni amekufa kwa sababu tu ya zinaa.
Ndugu, Kwa KRISTO wala hakuhitajiki mbwembwe Bali anahitajika utakatifu tu.
Isaya 55:6-7 " Mtafuteni BWANA, maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yu karibu;
Mtu mbaya na aache njia yake, Na mtu asiye haki aache mawazo yake; Na amrudie BWANA, Naye atamrehemu; Na arejee kwa MUNGU wetu, Naye atamsamehe kabisa."



MUNGU akusaidie wewe ambaye utaanza uzinzi na uasherati baada ya kujifunza Neno la MUNGU.
Najua kabisa  kuna watu huwa  ni viwete wa kiroho hata ukiwaonya kwa Neno la MUNGU, Neno hilo litateleze tu ndani yao na huondoka.
Fikra zao zimefungwa na shetani hata hawaiwazii toba ya kweli.
Wokovu kwao ni mzigo na hata uzima wa milele hawauwazii.
Kanisani huenda lakini ni wazinzi wakubwa, hawana tofauti na watu wa mataifa.
Wamejaa dhambi miguuni hadi kichwani, ufahamu wao shetani ameuchukua, ni hatari sana kwao.
Wamebaki na viburi tu huku kazi yao ni kuwasema uongo watumishi wa MUNGU.
Wakati mwingine akili zao zinawadanganya kwamba labda MUNGU hayupo.
Ndugu zangu ni heri kumtii MUNGU na kujitenga mbali na maovu.

MUNGU anasema ''Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie.-Zaburi 34:14 '' 

MUNGU akubariki na pia Ukipenda kunisapoti kwa sadaka katika huduma yangu karibu sana na pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane nitakujulisha jinsi ya kukipata.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa BWANA YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.
0714252292.
0786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.

Comments