HARIBU MADHABABU ZA KIPEPO ZOTE.

Na Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.


Bwana YESU atukuzwe ndugu yangu.
Karibu tujifunze ujumbe huu muhimu.
Kuna watu watapona leo kupitia ujumbe huu.
Kuna aina mbili za madhabahu.
Kuna madhabahu ya MUNGU na kuna madhabahu ya kipepo.
Nimeshafundisha sana masomo kuhusu madhabahu lakini na leo kwa ufupi naomba kumsaidia ndugu hapa ili ashinde kwa jina la YESU KRISTO yale yote yanayomtesa yakitokea kwenye madhabahu za kipepo.



Hebu kwanza ngoja niizungumzie madhabahu ya MUNGU kwa ufupi ili mwishoni nikikuambia juu ya kujiunganisha na madhabahu ya MUNGU ujue kwa urahisi.


Madhabau ni daraja kutoka ulimwengu wa roho kuja ulimwengu wa mwili.


Ili kitu kije kutoka ulimwengu wa roho basi ili kifike ulimwengu wa mwili basi ni lazima kipite katika madhabahu.


Madhabahu ya MUNGU kazi yake ni kwa ajili ya watu kutembea katika utakatifu na baraka za MUNGU.
Madhabahu ya MUNGU ni pahali pa MUNGU kukutana na wateule wake.
Madhababu ya MUNGU ni moja tu maana MUNGU wa kweli ni mmoja tu yaani JEHOVAH.


Zaburi 83:16 '' Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, Ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote. ''



Na JEHOVAH amejifunua kwetu kupitia tu YESU KRISTO.
Hivyo madhabahu iliyo hai ya MUNGU aliye hai ni madhabahu katika KRISTO YESU pekee.


Mteule wa KRISTO popote uliko unatakiwa kukutana na MUNGU wako madhabahuni kwake.

Utakutana na MUNGU kwa njia ya maombi na ibada.


Usisahau pia kwamba wewe ni hekalu la MUNGU maana ROHO MTAKATIFU anakaa ndani yako.
Hivyo inakupasa sana kuishi maisha matakatifu, maombi na kuliishi kusudi la MUNGU katika Wokovu wa Bwana YESU.


Ndugu iheshimu madhabahu ya MUNGU na pambana na kila madhabahu za kipepo na zivunje kwa jina la YESU maana ukiziacha madhabahu za kipepo zitakutesa.

Kumbuka madhabahu za kipepo ni pahali wachawi wanalitaja jina lako ili wakuroge, wewe wapige kwa maombi katika jina la YESU KRISTO.


Madhabahu za kipepo ni pahali mambo kukuhusu wewe yanatajwa hivyo haribu madhabahu zote za kipepo wanakokutaja.


Madhabahu ya kipepo ukiiacha ni hatari sana kwako maana wakati mwingine maisha yako na hatima yako vinaweza kuunganishwa na madhabahu za kipepo hivyo usipojitenga na madhabahu hizo za kipepo zitakutesa na hautafanikiwa.


Wakuu wa giza wameweka hadi madhabahu za kipepo za taifa, madhabahu za mji, kijiji au jamii, hivyo kama mteule wa MUNGU usikubali kunaswa na madhabahu za ukoo au za mji bali jitenge na kila madhabahu za kipepo, jitenge kwa jina la YESU KRISTO.


Kuna mabaya yanaweza kukupata yakitokea kwa wazazi wako au mababu zako ambao wajiungamanisha na madhahabu za kipepo.


Maombolezo 5:7-8 ''7 Baba zetu walitenda dhambi hata hawako; Na sisi tumeyachukua maovu yao. Watumwa wanatutawala; Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao. ''

Ndugu, futa laana ya kuchelewesha ambayo ina chanzo katika mababu zako.
Huo ni mnyororo ambao usipoukata utachelewa kufanikiwa katika kila baraka yako.


Biblia inasema wababu zetu na baba zetu walifanya mabaya na mabaya hayo yametupata hadi sisi.


Leo jiondoe katika madhabahu za kipepo zilizoshikilia ukoo wako au familia, jitoe kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.


Inawezekana ni madhababu ya kufuta kibali chako cha kufanikiwa katika jambo fulani.


Inawezekana ni madhabahu ya kukuondolea madaraka yako au cheo.


Wapo watu wengi sana wameathiriwa na madhabahu za kipepo.
Kuna wanandoa wanaume/Wanawake madhabahu za kipepo zimewafanya kuwachukia wake zao au waume zao bila hata sababu ya msingi.


Mwanandoa nakuomba haribu kila madhabahu ya kipepo aliyounganishwa nayo mwenzi wako maana unaweza ukashangaa kinafika kipindi anakuchukia tu bila kosa lolote kumbe ni kwa sababu ya madhabahu ya kipepo iliyomfunga.


Madhabahu za kipepo kazi yake nyingine ni kuwafanya watu wasio na YESU KRISTO wawe vipofu wa kiroho.
Unaweza ukasumbuka sana kumsaidia kiroho mtu kumbe unatakiwa kwanza upambane na madhabahu ya kishetani iliyomkamata.


Kuna madhababu ya magonjwa, hivyo ni muhimu sana kuombea uponyaji lakini usisahau kuibomoa madhabahu ya magonjwa.


Tangu zamani MUNGU aliagiza wateule wake waziharibu madhabahu za kipepo maana zina madhara makubwa sana kama zikiendelea kuwepo katikati ya wateule.


Kumb 7:5 ''Lakini watendeni hivi; zivunjeni madhabahu zao zibomosheni nguzo zao, yakateni maashera yao, ziteketezeni kwa moto sanamu zao za kuchonga. '' 


Haribu kila madhabahu ya kipepo iliyokufunga.


Haribu kila madhabahu za kipepo zilizowafunga watu wanaokuhusu.


Maombi yako katika jina la YESU KRISTO ni muhimu sana kwa ajili ya ushindi wako na kustawi kwako kiroho na kimwili.


Moja ya kitu muhimu sana kukiombea na kukikomboa ni kibali chako cha utawala katika ulimwengu wa roho.
Mawakala wa shetani kama kuna kitu hutaka kukikamata kwanza ni kibali chako kutoka kwa MUNGU.


Naomba uwe unaombea kibali chako mara kwa mara maana kikikamatwa kibali chako rohoni hakika utahangaika sana sana.


Mtu asiye na kibali huwa hapendwi popote.
Mtu mwenye kibali hupendwa popote.
Inawezekana watu hawakupendi bila sababu na haujui ni kwanini. Ndugu ombea kibali chako na iharibu madhabahu ya giza iliyokufunga kibali chako.


Omba neema ya MUNGU baada ya kujifungua kutoka vifungo maana kama huna neema ya MUNGU huwezi kupendwa pia.
Laana inaweza ikaondoa kibali na neema juu yako.


Kazi ya kibali hata mawakala wa shetani wakiandame kibali chako ni hii;
1. Kibali kinafungua macho ya watu kukuona.


2. Kibali kinaamrisha watu kukukubali.


wanaweza kushangaa tu wanakukubali sana na hawajui kwanini wanakukubali kumbe ni kwa sababu tu una kibali na neema.


3. Kibali kinawafanya watu wakuheshimu.


4. Kibali kinawafanya watu kukupenda na kukukaribisha.


5. Kibali kinawafungua watu ili wakuthamini.


6. Kibali kinaamrisha watu wakufuate.


7. Kibali kinakutengeneza ili uonekane unafaa.


Jambo muhimu kujua ni kwamba laana iliyotokana na madhabahu za giza inaweza kufuta kibali chako usiposimama vizuri kwa Bwana YESU.
 Hivyo futa laana na haribu madhabahu za giza zilizokufunga.

Jina la YESU KRISTO lipo na Damu ya YESU KRISTO ipo ili kukushindia hivyo omba ndugu na utashinda.

Kumbuka katika kupata kazi nzuri unahitaji kibali cha MUNGU.
Ili kupata Mke mwema au mume mwema unahitaji kibali cha MUNGU.
Ili Biashara yako ifanikiwe unahitaji kibali cha MUNGU.
Ili huduma yako ifanikiwe unahitaji kibali cha MUNGU.
Ili ufaulu masomo unahitaji kibali cha MUNGU.
Ili ujenge unahitaji kibali cha MUNGU.
Ili ushinde unahitaji kibali cha MUNGU.
Usikubali wachawi na madhabahu zao za giza wakakupangia mabaya, futa uchawi wao na bomoa madhabahu zao zote kwa jina la YESU KRISTO.


ukikosa kibali umekosa kitu muhimu sana sana.
Ombea kibali chako na futa kila madhabahu za kipepo iliyokuwa imeshikiria kibali chako.


Zaburi 19:14 ''Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee BWANA, Mwamba wangu, na mwokozi wangu.''

 
Ndugu hakikisha unajiungamanisha na madhabahu ya MUNGU ili madhabahu za kipepo zote zifutike.


Mpokee YESU KRISTO kama Mwokozi wako, huko ndiko kujiungamanisha na madhabahu ya MUNGU.


Kwa sadaka sahihi pia unaweza kujiungamanisha na madhabahu ya MUNGU.

Ishi maisha matakatifu, hudhuria ibada na maombi na jitenge na kila kazi ya shetani ndipo utapata kibali kwa MUNGU.



Asante kama umelielewa Neno la MUNGU ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
Bwana YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na Bwana YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee Bwana YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwanna YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
+255714252292.

mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu

Comments