MAOMBI YA KUFUTA DUA ZA KIPEPO ULIZOHUSISHWA.

Na Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
 Bwana YESU atukuzwe ndugu yangu.
Karibu tujifunze Neno la MUNGU na kisha tuombe maombi  ya ushindi.
Dua ni nini?
Dua ni maneno unayowasiliana na MUNGU.
Dua ya kishetani ni nini?
Dua ya kishetani ni maneno unayowasiliana na mashetani.
Dada mmoja ambaye ni rafiki yangu siku moja aliniambia kwa simu kwamba katika ukoo wao kuna mwaka ndugu wengi sana katika ukoo walikufa kwa sababu wana ukoo walikosea kufanya dua ya ukoo. Nilishangaa na nikamuuliza ilikuwaje na mambo hayo ni nini? Akasema kwamba katika ukoo wao kila mwaka huwa wanasoma dua za kishetani za kuombea ukoo. Sasa Mwaka huo walikosea taratibu za kimatambiko ndio maana walikufa watu wengi. Nilichomwambia ni kwamba shetani  ni baba wa uongo, anajifanya analinda na wakati huo huo anaua hao hao aliojifanya anawalinda. Kuna watu wanafanya dua kwa mashetani na wao wanaziita ni hoja nzito kwenye miungu yao. Wengine huita dua hizo kuwa ni ibada ya daraja la juu zaidi. Sasa nisikilize ndugu itakusaidia.
Shetani ni baba wa uongo, hivyo wanaomtumainia wako katika njia isiyo sahihi.
Yohana 8:44  ''Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.''
 Ngoja nikupe mfano mmoja, Kwa sababu shetani ni baba wa uongo basi wapo watu hufanya dua kwa wafu, dua kwa majini, dua kwa watu, dua kwa mizimu na dua kwa shetani mwenyewe. Dua hizo za kipepo zimeleta madhara makubwa kwenye maisha ya watu wengi wasio na KRISTO YESU.
Dua hizo za giza zinaamsha majini kufuatilia watu na kuwatesa sana katika maisha yao, MUNGU anakataza wanadamu kujihusisha na nguvu za giza ikiwemo dua ya kipepo, mfano dua ya wafu.
Kumb 18:10-13 '' Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu. Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa BWANA; kisha ni kwa sababu ya hayo BWANA, Mungu wako, anawafukuza mbele yako. Uwe mkamilifu kwa BWANA, Mungu wako.''
 Kuomba wafu, hiyo ni dua ya kipepo.
Biblia inasema kwamba Wafu hawajui lolote hata moja.
Mhubiri 9:5 '' kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa.''
 na wanaowaomba wafu wanajua kabisa kwamba wafu hawajui lolote na hawana msaada hata mmoja kwa mwanadamu anayeishi duniani, lakini kwa sababu shetani ni baba wa uongo kuna watu matokeo ya kishetani  hutengenezwa na majini kupitia ibada hizo, na mtu huyo huanza kufuatiliwa na majini katika maisha yake.
Leo kumejaa dua nyingi za kipepo na hizo zinatesa maisha ya wengi.
Kuna watu wana matambiko ya ukoo, familia au kabila na hayo hujumuisha dua ambazo ni mlango wa shetani kuwatesa watu hao.
Kuna watu huenda kwa waganga na huko dua za kipepo husomwa na kufunga maisha ya watu.
Ndugu leo futa dua zote za kishetani ulizohusishwa. 
Jitenge na maagano ya giza yaliyotokana na dua za kichawi.
Ndugu mmoja alisoma hadi chuo kikuu huku baadhi ya ndugu zake na majirani wakiwa na hasira kwa sababu baba yake mzazi alikuwa anawalingishia watu hao kwamba mtoto wake akimaliza chuo atapata kazi nzuri na kuinua familia hiyo. Baada ya kumaliza masomo yule kijana, katika hali isiyo ya kawaida vyeti vyake vya masomo viliibiwa na kupelekwa kusomewa dua kwa mganga ili asipate kazi, kisha vikarudishwa huku akiambiwa kwamba vimesomewa dua hivyo kuhusu kazi asahau. Ndugu ilichukua zaidi ya miaka 8 akitafuta kazi bila mafanikio.
Dua za kipepo ni mbaya sana sana na leo futa dua zote za giza zilizosomwa ukihusishwa wewe ili usifanikiwe katika jambo fulani maishani mwako.
Inawezekana hata wewe kikwazo katika maisha yako ni dua ya kipepo uliyosomewa.
Kuna watu walisomewa dua ili wasifunge ndoa au wasizae, Leo kwa damu ya YESU KRISTO futa kila dua ya kipepo.
Kuna watu walisomewa dua ili wawe vichaa, leo futa kila dua ya kichawi, kwa maombi yako katika jina la YESU KRISTO.
Zamani za mitume kuna watu waliokoka na kuleta zana zao za kichawi, vitabu vyao vya kichwai ili vichomwe moto.
Matendo 19:19-20 ''Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu. Hivyo ndivyo neno la BWANA lilivyozidi na kushinda kwa nguvu. ''
 Vitabu vya kiganga na kichawi ni ibada ya shetani na vitabu hivyo hutumika katika dua za giza.
Wasoma dua za kipepo huhusisha vitabu vya kiganga na kichawi.
Hakikisha katika maisha yako hushiriki ibada hizi za giza na kama wamekufunga kipepo kwa dua za giza, leo zifute dua hizo kwa damu ya YESU.
Kumbuka ulimwengu wa roho unaenda kwa matamsha hivyo inawezekana unateseka kwa sababu ulitamkiwa mabaya, mabaya hayo ndio dua za giza.

MADHARA YA DUA ZA GIZA.

1.Ni dhambi kwa MUNGU aliye hai.
Isaya 8:19  ''Na wakati watakapokuambia, Tafuta habari kwa watu wenye pepo na kwa wachawi; waliao kama ndege na kunong'ona; je! Haiwapasi watu kutafuta habari kwa MUNGU wao? Je! Waende kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?   ''

2. Ni ibada ya kishetani ambayo Mcha MUNGU hatakiwi kuhusika.
Walawi 19:31 '' Msiwaendee wenye pepo, wala wachawi; msiwatafute; ili kutiwa unajisi na wao; Mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.''

3. Hutengeneza maagano ya kishetani.
1 Kor 10:20 '' Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa MUNGU; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha BWANA na kikombe cha mashetani.''

4. Ni kujiunganisha na shetani ili awe na uhalali kwako.
1 Kor 10:14-15 '' Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu. Nasema kama na watu wenye akili; lifikirini ninyi ninenalo. ''

Inawezekana wewe umewahi kushiriki dua hizi za giza, tubu kwa ajili ya hilo na jitenge kwa jina la YESU KRISTO na hiyo dua ya giza.
Inawezekana wewe hujawahi kushiriki dua hizi za giza lakini wapo watu wasiokutakia mema ambao walifanya dua hizo ili zikupate, futa dua hizo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kumbuka hizi ni zama za mwisho na mafundisho ya mashetani ni mengi kama Neno la MUNGU linavyosema katika 1 Timotheo 4:1 kwamba ''Basi ROHO anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;   ''
 Watu wengi leo wamewaendea makuhani wa kishetani ambayo husoma dua hizo za giza. Makuhani wa giza wasoma dua ni waganga wa kienyeji, wachawi, wanajimu, wasihiri na wakuu wa giza wote.
Leo hata kanisa la MUNGU linashirikishwa katika ukumbi mmoja au uwanja mmoja na watu wenye Mungu mwingine ili kuomba maombi fulani, hapo kila imani na MUNGU wao, ndugub jitenge na dua za giza.
Maombi ya leo.
1. Futa kwa damu ya YESU KRISTO kila dua ulishiriki au uliyohusishwa.
2. Futa kwa damu ya YESU KRISTO kilichobebwa na dua za giza ulizohusishwa.
3. Futa maagano ya kishetani yaliyotokana na madhabahu za giza zilizosoma dua ya giza kukuhusu.
4. Haribu majini wote waliofanyia kazi dua za kishetani zilizofanyika kwa ajili yako au kwa ajili ya watu wanaokuhusu.
5. Batilisha kila mipango ya giza inayotokana na dua za giza.

Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane na nitakujulisha jinsi ya kukipata
na  Naamini kitakusaidia sana.
Hapa chini ni 
MAOMBI YA KUFUTA DUA ZA KIPEPO ULIZOHUSISHWA.
Maombi haya naomba yamsaidie mtu yule ambaye hajui kuomba ili katika kuomba kwa kutumia hayo basi atakumbuka mahitaji yake na kuyataja katika maombi yake. Haya hapa chini ni maombi ya kuanzia tu katika maombi yako ili uendelee zaidi kuomba
Kwa waombaji wazoefu naamini baada tu ya kulisoma somo na kulielewa basi anajua aombee nini maana alikuwa anaandika points za kuombea.


 MAOMBI YA KUFUTA DUA ZA KIPEPO ULIZOHUSISHWA.

 Wewe MUNGU Baba ni wa tahamni sana na ninakushukuru sana kwa kunilinda na kunipa uzima. Nikiwa na wewe YAHWEH MUNGU wangu ni bora kuliko vyote maishani mwangu.
Niko mbele zako MUNGU wangu ninaomba unisamehe kwa dua ya kipepo yeyote ambayo mimi binafsi nilishiriki katika dua hiyo, nisamehe MUNGU wangu na ninatubia dhambi hiyo. Damu ya YESU kristo Mwokozi itakase roho yangu na nafsi yangu na kila dua ya giza iyaachie maisha yangu sasa, katika jina la YESU KRISTO.
Ninatubu MUNGU wangu kwa ajili ya dua za kipepo walizoshiriki mababu zangu na wazazi wangu, mahali popote niliposhikilia na dua hizo za giza naomba kwa Neema yako Bwana YESU niachiliwe huru leo.
Kila dua yenye hukumu ndani yake, ninatubu kwa ajili ya dua hiyo na kwa neema yako Bwana YESU ninaomba hukumu hiyo ifutike na isiyaguse tena maisha yangu.
Nafuta kila dua ya giza iliyotamkwa na wachawi au na majini kunihusu, naifuta dua hiyo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila dua ya giza iliyotamkwa na wanadamu kunihusu mimi,  naifuta dua hiyo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila dua ya kichawi iliyofanywa na wasionitakia mema, naifuta dua hiyo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila dua ya giza iliyotajwa na wanaotaka nifukuzwe kazi au nifilisike biashara, naifuta dua hiyo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila dua ya kishetani aliyotamkiwa baba yangu au mama yangu ambayo na mimi nahusika kama sehemu ya uzao wao, naifuta dua hiyo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Dua za kunizuia kufunga ndoa, naifuta dua hiyo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Dua za kunizuia kuzaa,naifuta dua hiyo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Dua za kunizuia kuishi maisha ya amani na furaha katika ndoa, naifuta dua hiyo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Dua ya kunifanya nifuatiliwe na majini, naifuta dua hiyo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila dua ya kichawi iliyotamkwa na mchawi, mshirikina, mwanga, mgangaa wa kienyeji au mkuuu wa giza yeyote, naifuta dua hiyo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila adhabu iliyobebwa na dua za kichawi dhidi yangu, hiyo adhabu naifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila adhabu iliyo katika dua za giza kunizuia kupata kazi au kufanikiwa, hiyo adhabu naifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila hukumu ya kipepo iliyotokana na dua za giza, hiyo adhabu naifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila kilichobebwa katika dua za kishetani ninakiharibu hicho kwa jina la YESU KRISTO.
 Kila agano la giza lililo katika dua ya kishetani kunihusu, hilo agano nalifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila agano la kipepo la kunifanya nidharauliwe na kuonewa,hilo agano nalifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila agano la kunizuia kusonga mbele katika biashara na maisha yangu, hilo agano nalifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila agano la kunifanya niwe mtumwa wa shetani, hilo agano nalifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila agano la kunifanya niwe wa kuonewa tu kipepo na wachawi kila siku, hilo agano nalifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila agano la giza lolote lililotokana na dua za giza,
hilo agano nalifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
 Sasa katika jina la YESU KRISTO nafanyika silaha ya MUNGU kwa ajili ya kuharibu majini wote wanaotumika kunifuatilia na kufuatilia maisha yangu na baraka zangu, Kama Neno linavyosema katika Yeremia 51:20-22 kwamba '' Wewe u rungu langu na silaha zangu za vita; kwa wewe nitawavunja-vunja mataifa; na kwa wewe nitaharibu falme; na kwa wewe nitamvunja-vunja farasi, na yeye ampandaye; na kwa wewe nitalivunja-vunja gari la vita, na yeye achukuliwaye ndani yake; na kwa wewe nitawavunja-vunja mwanamume na mwanamke; na kwa wewe nitawavunja-vunja mzee na mtoto; na kwa wewe nitawavunja-vunja kijana mwanamume na kijana mwanamke; ''
 Sasa kwa mamlaka ya jina la YESU KRISTO ninawaadhibu majini wote waliotumwa kipepo kupitia dua za giza ili wanitese na kutesa fursa zangu, nawapiga kwa moto wa jina la YESU KRISTO sasa.
Kila jini aliyejificha katika mwili wangu ili kuleta magonjwa,  Nampinga jini huyo  na kumfukuza, kwa jina la YESU KRISTO Mwokozi wangu aliye hai.
Kila jini aliyejificha katika ndoa yangu ili kuleta migogoro, Nampinga jini huyo  na kumfukuza, kwa jina la YESU KRISTO Mwokozi wangu aliye hai.
Kila jini aliyejificha katika bishara yangu, Nampinga jini huyo  na kumfukuza, kwa jina la YESU KRISTO Mwokozi wangu aliye hai.
Kila jini aliyeingia uchumba wangu, Nampinga jini huyo  na kumfukuza, kwa jina la YESU KRISTO Mwokozi wangu aliye hai.
Kila jini aliyeingilia afya yangu,Nampinga jini huyo  na kumfukuza, kwa jina la YESU KRISTO Mwokozi wangu aliye hai.
Nawapiga kwa fimbo ya chumba sasa, sawasawa na Zaburi 2:9 Inayonipa mammlaka kwa jina la YESU KRISTO ikisema '' Utawaponda kwa fimbo ya chuma, Na kuwavunja kama chombo cha mfinyanzi.''
 Sasa nabatilisha kila mipango ya siri mibaya ya kunidhuru au kuniharibia maisha yangu, naiharibu kwa jina la YESU KRISTO mipango hiyo.
Sasa mimi ni mshindi na sitashikwa tena na dua za giza katika maisha yangu.
Asante Bwana YESU maana umeniokoa leo na kunikomboa na sasa nimeshinda kwa jina la YESU KRISTO.
Utukufu na heshimu ni kwa MUNGU BABA wa MBINGUNI.
Katika jina la YESU KRISTO nimeomba na kupokea ushindi.

Amen Amen Ameeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeen.
Hakika umeshinda.
Ukiweza kufunga unaweza kufunga hata siku 1 au 3 au 3 au hata 5 au zile ambazo wewe utaona unaweza ukihusika kila siku na kipengele kimoja kuombea na kumbuka baada ya maombi ya kufunga au hata maombi ya bila kufunga fanya tendo la imani kwa MUNGU kwa kutoa sadaka nzuri ikiambatana na maombi kutoka kwako na kwa mtumishi hai wa Bwana YESU juu ya ukomo wa kuteswa na maadui katika ulimwengu wa roho
 Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa BWANA YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.
0714252292.
0786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.

Comments