MAOMBI YA KUFUTA MIPANGO MIBAYA YA SIRI DHIDI YAKO

Na Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
  Bwana YESU KRISTO atukuzwe ndugu yangu!
Karibu tena karibu sana tujifunze Neno la MUNGU kisha tuombe maombi ya ushindi katika jina la YESU KRISTO.
Najua unataka kushinda katika vita ya kiroho uliyopo, twende pamoja na MUNGU Baba atakupa kushinda leo.
Shetani wakati mwingine hutumia watu ili kukuletea madhara wewe.
Sio watu wote watakupenda siku zote, mimi Peter  miaka kadhaa iliyopita kuna mtu alitengeneza urafiki na mimi na alikuwa karibu sana na mimi kumbe alikuwa na ajenda yake ya siri dhidi yangu. Siku moja kabla hajatekeleza mpango wake alijikuta anakamatwa na nguvu za MUNGU na  kunitamkia mwenyewe kabisa kwamba alitumwa na shetani ili kunidhuru kiroho. Ukaribu na mtu huyo ukaisha tangu siku hiyo.
Hata wewe ndugu yangu unayesoma ujumbe huu naomba utambue kwamba sio watu wote wanakutakia mema.
Kwenye Biblia kuna mifano hai mingi ya watu ambao walipanga hila kwa wengine, hata wewe anaweza akatokea mtu na akapanga hila dhidi yako na usipopata neema ya MUNGU unaweza kuangamia kabisa au kudhurikaleo haribu kila ajenda ya siri inayopangwa na watu wasiokutakia mema, hata kama kwa macho wanaonekana ni watu wazuri kwako na wana furaha.
Tujifunze kwa mifano hii hai ya zama za Biblia.

1. Ndugu wa Yusufu walipanga mpango wa siri wa kumuua, wakaishia kumuuza Misri awe mtumwa.
Mwanzo 37:18 ''Wakamwona toka mbali, na kabla hajawakaribia, wakafanya shauri juu yake ili wamwue.''
Hata wewe wanaweza wakapanga kukudhuru au kukuua hata wale ambao hukutarajia.
Niliwahi kukaa kijiji fulani zamani ambako katika kijiji hicho alikuwepo Baba mmoja ambaye alikuwa tajiri sana wa ng'ombe na alikuwa na watoto wawili vijana wakubwa. Vijana wale walitaka Baba yao anunue gari fuso lakini Baba yao alikataa, vijana wale walimuua Baba yao na kisha kuuza baadhi ya ng'omba na kukunua fuso kubwa na wakahama ule mji, hiyo ni hatari ambayo hata mtoto wako mwenyewe wa kumzaa anaweza kupanga hila mbaya kama hii, kwa Yusufu yeye ni ndugu zake wa damu ndio walipanga kumuua. Hata wewe watu wako wa karibu wanaweza kupanga mabaya dhidi yako, ndugu leo futa kila mpango wa siri kukuhusu wewe.

2. Amnoni alifanya mpango wa siri ili ambake Dada yake aitwaye Tamari.
Hiyo Iko 2 Samweli 13:3-17.
Kwa ufupi Mistari 10,11,12 na 14 ya Hiyo Samweli wa pili sura ya kumi na tatu inasema '' Amnoni akamwambia Tamari, Kilete chakula chumbani, nipate kula mkononi mwako. Basi Tamari akaitwaa mikate aliyoifanyiza, akamletea Amnoni nduguye mle chumbani. Naye alipokwisha kuileta karibu naye, ili ale, Amnoni akamkamata, akamwambia, Njoo ulale nami, ndugu yangu.
 Naye akamjibu, La, sivyo, ndugu yangu, usinitenze nguvu; kwani haifai kutendeka hivi katika Israeli; usitende upumbavu huu.
Walakini yeye hakukubali kusikiliza sauti yake; naye akiwa na nguvu kuliko yeye, akamtenza nguvu, akalala naye.''


3. Absalomu alifanya mpango wa siri kwa miaka miwili ili amuue Amnoni, kwa lengo la kulipiza kisasi, hakika akamuua.
Hiyo iko 2 Samweli 13:23-29.
 Mstari wa 28 na 29 Biblia inasema '' Kisha Absalomu akawaamuru watumishi wake, akasema, Angalieni basi, moyo wake Amnoni utakapofurahiwa kwa mvinyo; nami nitakapowaambia, Mpigeni Amnoni, ndipo mwueni, msiogope; si mimi niliyewaamuru? Iweni hodari, iweni na ujasiri. Basi watumishi wa Absalomu wakamfanyia Amnoni kama alivyoamuru Absalomu. Ndipo wakaondoka wana wote wa mfalme, wakapanda kila mtu nyumbu wake, wakakimbia.''

 4. Farao alipanga mpango wa siri wa kumuua Musa, Musa akakimbilia Midiani ndio ikawa pona yake.
Kutoka 2:15 ''Basi Farao alipopata habari, akataka kumwua Musa; lakini Musa akakimbia mbele ya Farao, akakaa katika nchi ya Midiani; akaketi karibu na kisima.''

Kwa mifano hiyo minne sasa najua umetambua jinsi ambavyo huwa wakati mwingine kunatokea mipango ya siri dhidi yako.
Hii ni mipango ya wanadamu tu lakini pia ipo mipango ya siri ya wachawi, waganga, wakuu wa giza na majini.
Mipango ya siri ya kipepo iko mingi sana lakini ukimtegemea MUNGU Baba huku unaishi maisha matakatifu katika KRISTO  na wewe ni muombaji hakika MUNGU atakuokoa  na kila hila ya giza.
Zaburi 68:20 ''Mungu kwetu sisi ni MUNGU wa kuokoa; Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA Bwana.''
 Hakuna aliye kama MUNGU hivyo jiamini ndugu na mpendeze MUNGU kwa kuishi maisha matakatifu hakika atakuokoa.
Mithali 18:10 '' Jina la BWANA ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.''

SABABU ZA WATU  KUPANGA MIPANGO MIBAYA YA SIRI DHIDI YAKO.

1. Wivu.
Matendo 5:17-20 '' Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), WAMEJAA WIVU, wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza; lakini malaika wa BWANA akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema, Enendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya Uzima huu. ''

2. Chuki zisizo na maana.
Mwanzo 37:8 ''Ndugu zake wakamwambia, Je! Kweli wewe utatumiliki sisi? Nawe utatutawala sisi? WAKAZIDI KUMCHUKIA KWA AJILI YA NDOTO YAKE, na kwa maneno yake.''

3. Kukosa moyo wa msamaha.
2 Samweli 13:32 ''Akajibu Yonadabu, mwana wa Shama, nduguye Daudi, akasema, Asidhani bwana wangu ya kwamba wamewaua vijana wote, wana wa mfalme; maana ndiye Amnoni peke yake aliyekufa; yakini haya yamekusudiwa kwa kinywa chake Absalomu tangu siku ile alipotenzwa nguvu umbu lake, Tamari.''
Absalomu alishindwa kumsamehe Amnoni ndio maana kwa miaka miwili alikuwa anapanga kumuua na kisha akamuua, huko ni kukosa moyo wa msamaha.
Hata wewe watu inawezekana kuna ulimkosea zamani lakini kwa sababu hajakusamehe basi anafanya mipango ya siri mibaya dhidi yako.
Luka 6:37 '' Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa.''

 4. Watu hao kudanganywa na mawakala wa shetani.
Zaburi 106:35-38 ''Bali walijichanganya na mataifa, Wakajifunza matendo yao. Wakazitumikia sanamu zao, Nazo zikawa mtego kwao. Naam, walitoa wana wao na binti zao Kuwa dhabihu kwa mashetani. Wakamwaga damu isiyo na hatia, Damu ya wana wao na binti zao, Waliowatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani; Nchi ikatiwa unajisi kwa damu.''
Walitoa watoto wao kuwa sadaka kwa mashetani. Ili watoto hao hata wauawe na kuwa sadaka kwa mashetani kuna mipango mingi ya siri hufanyika kuhusu hao watoto.

5. Ili kukuondoa kwenye Wokovu.
Wagalatia 1:6-8  '' Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya KRISTO, na kugeukia injili ya namna nyingine. Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya KRISTO.  Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe.''
Hakuna mpango mbaya wa siri kama watu kukaa kikao cha kipepo ili wahakikishe unaacha wokovu. Watu hawa wanaweza kuwa wahubiri wa uongo, washauri wa uongo n.k, Target yao wewe umwache YESU,  futa huo mpango wa siri na uwe makini sana huku ukilitii sana Neno la Injili ya kweli ya YESU KRISTO.
 
5.  Ni dalili za siku za mwisho.
Mathayo 24:4-13  ''..............   Hayo yote ndiyo mwanzo wa utungu. Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu. Ndipo wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana, na kuchukiana. Na manabii wengi wa uongo watatokea, na kudanganya wengi. Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa. Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.''
Dalili mojawapo ya siku za mwisho ni pamoja na watu wabaya kupanga mipangon mibaya dhidi yako huku hujawakosea lolote.

7. Ili wakuonee kwa sababu ya huduma yako.
Yeremia 18:18 ''Hapo ndipo waliposema, Njoni na tufanye mashauri juu ya Yeremia; maana sheria haitampotea kuhani, wala shauri halitampotea mwenye hekima, wala neno halitampotea nabii. Njoni, na tumpige kwa ndimi zetu, wala tusiyaangalie maneno yake yo yote.''
 Yeremia alikuwa nabii wa MUNGU analiyelitumikia kusudu la MUNGU kwa uaminifu, lakini watu wabaya walipanga mipango mibaya dhidi yake, hata wewe kunaweza kukatokea watu wakapanga mipango mibaya dhidi yako kwa sababu tu ya mafanikio ya huduma yako au ya maisha yako.

 Leo kupitia maombi yako hakikisha unafuta kila mpango wa siri wa kipepo dhidi yako.
Mpango wa siri unaweza wakati mwingine ukahusisha siri kubwa sana sana, unamhitaji tu ROHO MTAKATIFU ili akujulishe ndipo ujue kuomba na kushinda.
Watu wanaweza wakafanya mipango ya siri kupitia chakula, kukuendea kwa waganga, kukufunga vifungo vya giza, kukukosanisha na watu wako muhimu, kupanga hila za kukudhuru au kukuharibia. Kufanya mipango ili ufukuzwe kazi, uachwe na mchumba au ndoa yako ife. Kufanya mipango ili uteswe na mapepo.
Ziko hila nyingi sana watu wanaweza kupanga mabaya kumhusu mtu mwingine waliyemkusudia.
Hata katika kumtumikia MUNGU kunahitaji uwe na roho ya kushinda hofu na vitisho  maana ukizubaa unaweza kuikimbia kazi ya MUNGU kwa kuwaogopa tu wanadamu wanaopanga mipango mibaya dhidi yako.
Mama mmoja siku moja kwenye simu alinipigia nimuombee huku analia sana, Alisema kwamba kuna binti wa kazi alimtoa mkoani . Alipomfikisha mjini  maisha yaliendelea vyema tu lakini majanga yalikuja kuanza baada ya Mama huyo kuwa mjamzito. Wakati akiwa mjamzito mume wake alianza kutembea na msichana wa kazi  na baada ya muda jambo hilo likawa live na yeye sasa ndio akaanza kufukuzwa kwenye nyumba, alifukuzwa akiwa mimba akikaribia kujifungua. Msichana wa kazi akageuka mwiba mbaya sana uliyochoma moyo. Ndugu leo futa mipango ya siri iliyokwishwa kupitishwa na mawakala wa shetani dhidi yako, hata mipango inayotarajiwa kupitishwa na wapambe wa shetani baadae ifuteb leo kwa damu ya YESU KRISTO.
Kuna kushindi katika jina la YESU KRISTO.
Zaburi 91:2-6 '' Nitasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu, MUNGU wangu nitakayemtumaini.  Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, Na katika tauni iharibuyo.  Kwa manyoya yake atakufunika, Chini ya mbawa zake utapata kimbilio; Uaminifu wake ni ngao na kigao.  Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana,  Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri,''

 JINSI YA KUJINASUA KATIKA MIPANGO MIBAYA YA SIRI DHIDI YAKO.

1. Kwa maombi kataa kila mpango mbaya wa siri dhidi ya afya yako, uchumi wako, uzao wako, ndoa yako  na maisha yako kwa ujumla.
Zaburi 91:10 '' Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.''

2. Mwambia MUNGU kwamba awashughulikie wote waliopanga mipango mibaya dhidi yako na akulipizie kisasi.
Warumi 12:19 ''Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya MUNGU; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena BWANA.''

3. Kwa maombi ita malaika wa MUNGU ili walitimize kusudi la MUNGU kwako.
Zaburi 34:7 '' Malaika wa BWANA hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa. ''

4. Wapige upofu kwa maombi wote wanaopanga mabaya kukuhusu wewe.
2 Wafalime 6:18 ''Na walipomtelemkia Elisha akamwomba Bwana, akasema, Uwapige, nakusihi, watu hawa kwa upofu. Akawapiga kwa upofu sawasawa na neno la Elisha.''

5. Ita Neema ya KRISTO YESU, Upendo wa MUNGU Baba na ushirika wa ROHO MTAKATIFU ili hayo matatu yote yawe pamoja na wewe.
2 Kor 13:14 '' Neema ya Bwana YESU KRISTO, na pendo la MUNGU, na ushirika wa ROHO MTAKATIFU ukae nanyi nyote.''

6. Tumia damu ya YESU kufuta mitego yao na na jifunike kwa damu ya YESU KRISTO ili wasikuone kamwe katika ulimwengu wa roho.
Ufunuo 12:11 '' Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.''

7. Ishi maisha matakatifu siku zote na uwe mtu wa maombi  daima.
1 Thesalonike 5:17 '' ombeni bila kukoma;''

8. Enenda kwa ROHO MTAKATIFU siku zote.
Zaburi 32:8 '' Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.''
ROHO MTAKATIFU ndiye atakuonyesha njia ili adui zako wasikupate, atakushauri nini cha kufanya na atakuwa akikutazama, mpokee yeye katika KRISTO na mtiii sana.

 Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane na nitakujulisha jinsi ya kukipata
na  Naamini kitakusaidia sana.
Hapa chini ni 
MAOMBI YA KUFUTA MIPANGO MIBAYA YA SIRI DHIDI YAKO
Maombi haya naomba yamsaidie mtu yule ambaye hajui kuomba ili katika kuomba kwa kutumia hayo basi atakumbuka mahitaji yake na kuyataja katika maombi yake. Haya hapa chini ni maombi ya kuanzia tu katika maombi yako ili uendelee zaidi kuomba
Kwa waombaji wazoefu naamini baada tu ya kulisoma somo na kulielewa basi anajua aombee nini maana alikuwa anaandika points za kuombea. Kumbuka pia fundisho ni muhimu kuliko maombi hivyo wewe ambaye huwa unahusika na maombi tu hakikisha unajifunza kwanza somo lote ndipo utapata nguvu za kuomba na kushinda.


 MAOMBI YA KUFUTA MIPANGO MIBAYA YA SIRI DHIDI YAKO

 BABA katika jina la YESU KRISTO, ninakushuru na kukuabudu MUNGU wangu Muumbaji.
Pokea sifa heshima na utukufu wewe MUNGU mwangu mweza yote.
Niko pahali hapa muda naomba unitakase na kunisamehe dhambi zangu, uovu na makosa yote, nipe moyo wa toba na nipe kuiacha dhambi na kuichukia. Nahitaji nishinde katika wewe YESU KRISTO Mwokozi wangu.
Niko hapa leo ili kufuta kila mipango ya siri ya kipepo kunihusu mimi. Ninajua kabisa Bwana YESU ulinipa mamlaka kubwa kama Neno lako linavyosema katika Mathato 16:19  kwamba ''Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.''
 Eee MUNGU Baba ninaomba leo mamlaka hii uliyonipa  itumike ili kila mipango mibaya ya kipepo dhidi yangu ifutike, kwa jina la YESU KRISTO hakika inafutika leo.
Kila mpango wa siri uliofanywa na wanadamu dhidi yangu zamani, leo naufuta mpango huo wa siri, naufuta kwa damu ya YESU KRISTO katika jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila mpango wa siri uliokwisha kufanyika ili kunizuia kufunga ndoa, kufaulu mtihani, kupata mtaji,  kumalizia ujenzi wa nyumba yangu, leo naufuta mpango huo wa siri, naufuta kwa damu ya YESU KRISTO katika jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila mpango wa siri wa kunilelea magonjwa ya kipepo, leo naufuta mpango huo wa siri, naufuta kwa damu ya YESU KRISTO katika jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila mpango wa siri wa kunikosanisha na ndugu zangu, marafiki zangu au bosi wangu kazini kwangu, leo naufuta mpango huo wa siri, naufuta kwa damu ya YESU KRISTO katika jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila mpango wa siri wa kunisingia ili nifungwe au nifukuwe, leo naufuta mpango huo wa siri, naufuta kwa damu ya YESU KRISTO katika jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila mpango wa siri mahali popote ulipofanyika kunihusu mimi,
leo naufuta mpango huo wa siri, naufuta kwa damu ya YESU KRISTO katika jina la YESU KRISTO aliye hai.
 Eee MUNGU Baba ninaomba wote walipangan mipango ya siri mibaya dhidi yangu waabike na kufedheheka na kuumia wao kama Neno lako linavyosema katika Zaburi 71:13-15  kwamba ''Waaibishwe, watoweshwe, adui za nafsi yangu. Wavikwe laumu na aibu wanaonitakia mabaya. Nami nitatumaini daima, Nitazidi kuongeza sifa zake zote. Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako Mchana kutwa; maana sijui hesabu yake.''
 Kila mpango mbaya wa siri dhidi yangu ninafuta kwa damu ya YESU KRISTO.
Mpango wa siri wa zamani, mpango wa siri uliopo sasa na mpango wa siri unaotarajiwa kupangwa na watu wabaya, Hiyo mipango ya siri yote naifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO Mwokozi wangu aliye hai.
Kila mipango ya siri wa majini na wachawi, Hiyo mipango ya siri yote naifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO Mwokozi wangu aliye hai.
Kila mipango ya siri ya waganga wa kienyeji na waliowapelekea taarifa zangu, Hiyo mipango ya siri yote naifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO Mwokozi wangu aliye hai.
Kila mipango ya siri ya wakuu wa giza na mawakala wote wa shetani, Hiyo mipango ya siri yote naifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO Mwokozi wangu aliye hai.
Eee MUNGU Baba ninaomba unilipizie kisasi BWANA dhidi ya kila aliyepanga mipango mibaya ya kutaka kuniua au kunidhuru.
Kwa jina la YESU KRISTO ninawapiga sasa kwa upofu katika jina la YESU kila mawakala wa shetani wanaofanya mipango mibaya dhidi yangu, dhidi ya uchumba wangu, dhidi ya ndoa yangu, biashara yangu, kazi yangu, kipato changu, uchumi wangu na kilka kitu changu, Hiyo mipango ya siri yote naifuta kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO Mwokozi wangu aliye hai.
 Eee ROHO MTAKATIFU ninakuomba kwa Neema yako BWANA uwe pamoja na mimi, unifunulie siri za maadui zangu na unionyeshe njia ya kuwashinda.
Nawaalika sasa Malaika wa MUNGU ili watimize kusudi la JEHOVAH MUNGU wangu katika maisha yangu. Kazi za Malaika wa MUNGU kwangu ni kuniokoa kama Neno linavyosema katika Zaburi 34:7, ninaomba MUNGU Baba kwamba Malaika zako waniokoe na kila hila ya giza. Kazi za Malaika wa MUNGU kwangu ni kunilinda kama Neno la MUNGU linavyosema katika Zaburi 91:11, ninaomba kwako MUNGU Baba kwamba Malaika zako wanilinde kama agizo lako kwao lilivyo kwenye Neno lako la milele. Kazi za Malaika za MUNGU kwangu ni kunihudumia kama Neno la MUNGU linavyosema katika Waebrania 1:14, Ninaomba MUNGU Baba kwamba malaika zako wanihudumie.
 Kila mpango wa siri leo umekoma, walioiwinda afya yangu kuanzia leo hawataiwinda tena, katika jina la YESU KRISTO.
Walioiwinda ndoa  yangu kuanzia leo hawataiwinda tena, katika jina la YESU KRISTO.
Walioiwinda uchumba wangu kuanzia leo hawatauwinda tena, katika jina la YESU KRISTO.
Walioiwinda biashara yangu na kazi  yangu kuanzia leo hawataiwinda tena, katika jina la YESU KRISTO.
  Walioiwinda maisha  yangu kuanzia leo hawatawinda tena, katika jina la YESU KRISTO.
 Walioiwinda Baraka zangu  kuanzia leo hawatawinda tena, katika jina la YESU KRISTO.
Kila mpango wa siri leo umekoma, walioiwinda afya yangu kuanzia leo hawataiwinda tena, katika jina la YESU KRISTO.
 Asante MUNGU Baba wa upendo maana umenishindia na leo kupitia maombi haya ya imani katika jina la YESU KRISTO.
Mabaya yote waliyoyakusudia maadui zangu kuanzia leo mabaya hayo yatawapata wao na sio mimi.
Katika jina la YESU KRISTO nimeomba na kupokea ushindi.
Amen Amen Ameeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeen.
Hakika umeshinda.
Ukiweza kufunga unaweza kufunga hata siku 1 au 3 au 3 au hata 5 au zile ambazo wewe utaona unaweza ukihusika kila siku na kipengele kimoja kuombea na kumbuka baada ya maombi ya kufunga au hata maombi ya bila kufunga fanya tendo la imani kwa MUNGU kwa kutoa sadaka nzuri itakayoambatana na maombi  juu ya ukomo wa kuteswa na maadui zako katika ulimwengu wa roho 

Nawaonya pia wanaotumia masomo yangu vibaya na kwa manufaa yao waache tabia hiyo.
 Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa BWANA YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.
0714252292.
0786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.

Comments