![]() |
Na Peter M Mabula. Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU |
Bwana YESU
KRISTO atukuzwe sana ndugu yangu.
Karibu
tujifunze Neno la MUNGU.
Somo hili
nilipewa kama ufunuo kwa ajili ya kuwafundisha viongozi wa Kanisa ambao
wamekuwa na vita na wachungaji wao kwa miaka mingi kwa sababu tu ya matoleo.
Kuwapata wote kwangu ni jambo gumu hivyo
hata kwa nafasi hii najua maelfu ya viongozi Kanisani watajifunza kitu. Najua somo la namna hii ni moja ya masomo magumu sana kuyafundisha lakini MUNGU anaagiza nifundishe ndio maana sina budi kufundisha.
Nimewahi
kuwasiliana kwa simu na watu wengi wakiwalalamikia wachungaji wao juu ya
sadaka, rohoni mwangu nilishuhudiwa juu ya mara nyingi wanaolalamika ndio
walikuwa wanahitaji kusaidiwa kiroho.
Mfano Kuna Mchungaji mmoja katika Kanisa lenye
washirika 25 na katika washirika hao wanaotoa fungu la kumi ni chini ya watano
na hilo fungu la kumi la wote halifiki hata Elfu 40 kwa Mwezi. Mchungaji wa
Kanisa hilo kwa sababu ya vita na viongozi walio chini yake kanisani mara
kadhaa ameshaacha uchungaji lakini kwa
sababu ya wito na maonyo ya MUNGU imembidi kurudi, viongozi kanisani hapo
wamechachamaa wakimlaumu kwamba anatumia pesa yote inayopatikana, ambayo kwa
mwezi jumla haifiki hata laki moja. Nilipopata habari hiyo rohoni mwangu nilijikuta natafakari sana, na kuwaza kwamba
inawezekana watumishi wa jinsi hiyo wako wengi.
Hata
nilipopewa ufunuo huu nilikuwa bado nina maswali mengi sana. Mimi binafsi sio
Mchungaji lakini ROHO MTAKATIFU alishanijulisha kwamba ameniita katika Huduma
ya ualimu wa Neno la MUNGU. Uchungaji ni moja ya kazi ambazo naziogopa sana
hata kama Bwana YESU akisema juu ya
kumtumikia katika uchungaji hakuna
mjadala lazima nifanye kazi hiyo.
Inawezekana
pia katika baadhi ya watumishi
walioinuliwa kihuduma liko pia tatizo hivyo Kanisa la KRISTO kwa sehemu linakuwa kama limevurugwa.
Lakini pia
kuna wafundishaji wengi hasa wasio wachungaji makanisani hao hufundisha kwa
juhudi sana juu ya kuwafanya kanisa lisiwategemeze wachungaji wao, Wafundishaji
hawa wamejaa wivu juu ya wachungaji wao.
Wakati mwingine mimi huwa natamani
kila mwana kanisa ajue juu ya matoleo kila wiki ili kupunguza lawama mbalimbali
ambazo labda zisingekuwepo.
Kwa sababu
utoaji wa matoleo ni siri ya mtoaji
hivyo wakitoa Kanisa zima mfano Kanisa la
watu 100, mtu anaweza akadhani kwa kukadiria kwamba hapo jumla ya matoleo hayo labda ni laki mbili lakini
kumbe ukihesabu utakuta elfu 30 au 40. Kwa jinsi hiyo mitafaruku isiyohitajika
inaweza kujitokeza pasipo na sababu.
Na mara zote
washirika Kanisani huwa hawana tatizo ila tatizo linakuwa kutoka katika baadhi ya viongozi kanisani.
Sasa nisikilize ndugu itakusaidia maana wapo
pia walioambulia laana badala ya baraka kutokana na uongozi wao Kanisani.
Sasa
nisikilize.
1 Kor 9:14 '' Na BWANA vivyo hivyo ameamuru kwamba wale waihubirio Injili wapate riziki kwa hiyo Injili.
''
Ni MUNGU
ameamuru wahubiri injili wapate riziki katika hiyo injili.
Riziki ni
nini?
Kuna maana
mbili za Neno riziki.
1.
Riziki
ni neema anayoipata mtu kutokana na uwezo wa MUNGU.
2. Riziki
ni kitu kinachopatikana kutokana na kazi ya mtu na hivyo kitu hicho kumwezesha
kuishi.
Biblia imeagiza kwamba watumishi wanaochunga Kanisa la MUNGU
duniani(Matendo 20:28) basi riziki zao wazipate katika kazi yao hiyo ya
kuchunga kundi la MUNGU.
Hiyo Matendo 20:28 Inasema '' Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi
lote nalo, ambalo ROHO MTAKATIFU amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani
yake, mpate kulilisha kanisa lake MUNGU, alilolinunua kwa damu yake
mwenyewe.
''
Kumbe ni muhimu pia Mtumishi kuwa amewekwa na ROHO MTAKATIFU na sio kujiweka kwa lengo la kujipatia pesa.
Kumbe Mtumishi huyo naye anatakiwa kuwa safi na sio Mchafu yaani mdhambi.
Watumishi hawa ni wale ambao wanafanya kazi ya MUNGU
ya moja kwa moja siku zote na riziki hiyo wanaipata kutoka kwa watu
wanaowachunga au kuwahudumia kiroho.
Watumishi
hawa wanaweza kuwa wachungaji wa makanisa(Wanapata riziki kutokea Kanisani
alipo)
Mitume na manabii wanapata riziki katika injili wanayoipeleka
Wainjilisti na walimu Wanaipata riziki katika semina au madarasa
wanayofundisha
Biblia haimtaki Mtumishi kuidai riziki yake au kupanga mipango ya kuipata
riziki hiyo kutoka kwa kundi la MUNGU. Mambo ya MUNGU hayana kulazimishana bali
ni mtu mwenyewe rohoni anapata ufunuo au msukumo wa kutoa sadaka hivyo anatoa.
Mambo ya MUNGU hayahitaji ushawishi wa namna yeyote bali kazi ya Mtumishi wa
MUNGU ni kufundisha Neno sahihi la MUNGU hasa la kuwafanya watu waokoke,waache
dhambi, waishi maisha matakatifu na wamtegemee MUNGU na kumwabudu MUNGU katika
Roho na kweli.
Utoaji ni jambo la muhimu na lazima kwa wateule wa MUNGU. Biblia inasema
''….. Mmeniibia Zaka na Dhabihu. Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote-Malaki 3:8b''
Laana maana yake ni kutokufanikiwa, kutokustawi,kutofaulu, kukosa
furaha, kukosa amani, na kukosa mwelekeo sahihi. Ni wazi kabisa kuwa Wakristo
wengi sana hawana furaha, hawana amani na hawafanikiwi katika maisha yao ya
kila siku, kwa sababu hawamtolei MUNGU zaka na dhabihu.
Utoaji ni agizo la MUNGU na hivyo kuna faida kubwa katika utoaji wa mtu.
2 Kor 9:7-8 '' Kila mtu na atende kama
alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana
MUNGU humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu. Na MUNGU aweza kuwajaza kila
neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote,
mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;
''
Biblia inaendelea kusema '' Tena zaka yote ya nchi, kama ni mbegu ya nchi, au kama ni matunda ya nchi, ni ya BWANA; ni takatifu kwa BWANA.- Kumb 27:30 ''
Kuna watu wengi pia hawapendi Watumishi kupewa funga la kumi, lakini maandiko yanasema '' Tena utanena na Walawi, na
kuwaambia, Hapo mtakapoitwaa zaka mkononi mwa wana wa Israeli niliyowapa
ninyi kutoka kwao kuwa urithi wenu, ndipo mtakaposongeza sadaka ya
kuinuliwa kwa BWANA katika hiyo, iwe zaka katika hiyo zaka.-Hesabu 18:26''
Ni kweli ni agizo la MUNGU kwamba wahubiri wa injili wapate riziki kutoka
katika kazi yao ya injili, ni vyema pia tukajua kwamba riziki hizo sio zile
anasa.
Sio kusudi la MUNGU mchungaji au mhubiri alazimishe kupewa pesa au
watumie mbinu za kujipatia pesa, Hiyo ni dhambi na ni makosa.
Sio kusudi la MUNGU Mtumishi kuwapangia washirika pesa za kumpa, hayo ni
makosa makubwa sana.
Riziki zinahusisha malazi na mavazi, hivyo ni heri kanisa au watu wa
MUNGU wakamsaidia mhubiri riziki za vyakula na mahitaji mengine yaliyo ya
lazima yatakayomwezesha aifanye kazi ya MUNGU vyema.
Mathayo 10:7-10 '' Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.
Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.
Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu;
wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, wala fimbo; maana mtenda kazi astahili posho lake.''
Lakini pia Mhubiri anatakiwa kuwa
na juhudi katika kazi yake mbele za MUNGU ili hata iwe sababu ya MUNGU
kumwinulia watu wa kumpa riziki. Haiwezekani wewe ni Mchungaji wa Kanisa na
hujawahi hujawahi kushuhudia watu hata 20 kwa mwaka wakati ni wewe kazi yako ni kumtumikia MUNGU
tu huku washirika wakifanya kazi zao za vipato ili katika hivyo na wewe
wakupatie kidogo kwa agizo la MUNGU.
Unaweza ukawa ni mtumishi ambaye hutumizi wajibu wako hivyo riziki
inaweza ikawa jaribu kwako kumbe ni wewe mzembe. Mimi naamini MUNGU ni rahisi
zaidi kukuinulia watu kukupatia riziki kama wewe mwenyewe unatimiza wajibu wako
kwa MUNGU.
Na zingatia sana kwamba hutakiwi kuhubiri Neno la MUNGU ili upate riziki,
bali hubiri ni watu wampokee YESU KRISTO kama Mwokozi wao, hapo ndipo utakuwa
mtumishi sahihi mbele za MUNGU.
Wewe umewekwa na MUNGU moja kwa moja katika kazi ya injili, kwanini
huitendei haki kazi hiyo ya MUNGU.
Kazi yako ni kuwasaidia watu kiroho, kuwaombea na kutimiza kila wajibu
wako kwa MUNGU.
Moja ya jambo la muhimu sana sana ni mtumishi wa MUNGU kujitambua.
Unaweza ukakabidhiwa funguo kiroho za maelfu ya watu ili uwapatie,
usipojitambua utawafanya watu wasifunguliwe na hata riziki kwako inaweza
kukosekana. Mfano mimi Binafsi ni mara kadhaa nimeombea watu kwa simu na MUNGU
alipowafungua waliniambia mambo ya ajabu sana.
Mfano kuna Dada mmoja alikuwa anaumwa sana bna akadai ameombewa na
watumishi wengi mno na ikafika kipindi akaacha kwenda kwenye maombezi, siku
moja aliona somo langu mtandaoni akanipigia simu akijisemea huyu ni Mtumishi wa
Mwisho kuniombea maana watumishi wameshashindwa, kwa Neema ya MUNGU
akafunguliwa jioni ile ile na kuanza kusema mbona ameenda kuombewa sana lakini
hakupona ila akapona kwa simu, nikamwambia amshukuru MUNGU. Watu wa aina hiyo
ni wengi na baada ya maombezi husema mbona nimeombewa kwa watumishi wakubwa na
nimeenda kwenye madhabahu kubwa sana lakini sikupona?
Nilichojifunza ni kwamba kila mtumishi wa KRISTO aliye sahihi anazo
funguo za kufunga kazi za giza na kufungulia baraka kwa baadhi ya watu wa
MUNGU(Mathayo 16:19 '' Nami nitakupa wewe funguo za ufalme
wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa
mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa
mbinguni.'') ndio maana unaweza ukaombea watu wakapona na wengine
wasipone na Mtumishi mwingine anaweza akaombea watu wakapona na wengine
wasipone, labda ni kanuni ya MUNGU tusiyoijua, hata kama mimi naamini mtu
akielekezwa kwenda kuombewa iwe ni Kanisa fulani, semina fulani, mkutano fulani
au kwa Mtumishi fulani hakika funguo za uponyaji wake zinakuwa huko huko hivyo
anaweza akafunguliwa. Hata kama ili mtu apone pia hasa magonjwa kunahitaji
Mambo manne nanayofanya kazi, ndivyo ROHO MTAKATIFU aliniambia, ila akanitajia
matatu kwanza na naamini siku moja jambo la nne nitalijua.
Aliniambia kwamba, katika maombi kuna hitajika
1.
Imani
ya muombaji
2.
Imani ya muombewaji
3.
Mapenzi
ya MUNGU
Jambo la 4 sikuambiwa ila
naamini siku moja nitajulishwa, lakini hata haya matatu tu MUNGU amewaponya
wengi. Hivyo mtu akienda kuombewa madhabahu fulani na asipone inawezekana
tatizo sio la waombaji bali wakati mwingine tatizo ni lake na wakati mwingine
ilihitajika kuyatafuta mapenzi ya MUNGU juu ya kupona kwa ndugu huyo. Mapenzi
ya MUNGU kivipi?
Mfano Mtu husika alionywa
sana juu ya kuacha uasherati, yeye akashupaza shingo na kuja kupata magonjwa
mabaya, sasa kuomba tu apone kunaweza kusimsaidie bali mapenzi ya MUNGU atubu
kwanza kwa sababu alipinga maonyo ya MUNGU.
Inawezekana mhusika
alitamkiwa maneno ya kumfunga kwa ugonjwa na wachawi, sasa anaweza akafika kwa
mtumishi akiomba aombewe ili apone, sasa mtumishi kuita uponyaji tu kunaweza
kukapunguza tu tatizo na sio kuliondoa, mapenzi ya MUNGU katika hilo labda ni
kuharibu madhabahu iliyomshikiria, kufuta agano la kipepo alilofungwa nalo n.k
ukifanya hivyo kisha kwa dakika chache ukitamka apone kwa jina la YESU KRISTO
hakika anapona. Mapenzi ya MUNGU anayo ROHO MTAKATIFU hivyo ni muhimu sana
kumsikiliza ROHO MTAKATIFU katika maombi. Siku moja Kanisani kwetu alikuja dada
mmoja kuombewa, kwa sababu waliokuwa wanaombewa walikuwa ni watu zaidi ya 5
basi Mchungaji akatugawa ili tuendelee kuwaombea. Mimi na wengine wawili tukuwa
tunamuombea huyo dada, alianguka lakini tatizo lilikuwa halijatoka, Mchungaji
alipofika alitamka jambo la ajabu sana na hapo hapo yule dada akafunguliwa na
kupona. Mchungaji alipofika alisema ‘’Eee roho ya mauti mwachie binti huyu na
usimfuate tena’’ Hapo hapo Binti yule aliinuka na kupona, nilijifunza kitu
muhimu sana kwamba Kumsikiliza ROHO MTAKATIFU
ni faida kuu kwa Mtumishi wa MUNGU. Huo ni ufunuo aliopewa Mchungaji
hivyo wengine tulikuwa tunapiga risasi
kwa adui lakini tulikuwa tunapiga pembeni.
Sasa nimesema hapo ili
aliye Mtumishi ahakikishe anatimiza wajibu wake vyema.
Leo agizo la MUNGU la
wahubiri kupata riziki katika hiyo kazi yao wengi wanaitumia vibaya sana baadhi
ya watumishi.
Leo ni rahisi kuona
Kanisa linamchangia pesa kwa nguvu sana Mchungaji wao za kumnunulia gari la
nne(4), yaani ana magari matatu na sasa kanisa liko kwenye changizo ya lazima
ili kumnunulia Mtumishi wao gari ya 4.
Inawezekana sio kosa la moja kwa moja lakini ni heri sana tuhusike zaidi
kuchangia upelekaji wa injili na sio mambo ya anasa, ni heri kuhusike zaidi
kujenga Kanisa na sio anasa. Mchungaji mmoja alikataa Kanisa kumjengea nyumba
ya kawaida, akidai anataka Kanisa limjengee ghorofa, kama kanisa hawataki
waache maana kama ni nyumba za kawaida anazo 3. Ndugu zangu, riziki wanazopewa
watumishi hazitakiwi kugeuka anasa.
Lakini pia kuna maeneo
watu wamewaacha wachungaji wao kabisa kiasi kwamba hata utumishi umekuwa mgumu
sana.
Nilienda mkoa fulani na Mchungaji alikuwa anahubiri vizuri sana
lakini koti la suti limechanika na kila wiki anavaa hilo hilo. Kanisani kuna waumini zaidi ya 60, hiyo
binafsi naiona sio sawa.
Ni vyema sana kanisa
kujitambua ili kuwasaidia wachungaji wao.
Hata kama riziki ni jambo stahiki lakini basi riziki
imuhudumia mchungaji na mkewe na sio Kanisa hadi linakuwa na michango ya
kuchangia karo za watoto watatu wa Mchungaji wanaosoma shule za gharama kubwa.
Biblia inasema ni heri
watu watoe zaka na sadaka ili kiwepo chakula nyumbani mwa MUNGU na sio chakula
hicho kwenda kinyume na kusudi la MUNGU
Malaki 3:10 ''Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu,
mkanijaribu kwa njia hiyo, asema BWANA wa majeshi; mjue kama
sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata
isiwepo nafasi ya kutosha, au la.''
Ni vyema sana kanisa
kuwapatia riziki wachungaji wao lakini iwe kwa upendo na sio amri wala
kulazimishana.
Mimi ninachojua Neno
sahihi la MUNGU hata kama halihusu utoaji ndilo linaloweza kumpa mtu mzigo wa
kutoa riziki kwa mtumishi.
Kuna watumishi wengine ni
watumishi majina tu. Ndugu kazi ndizo zinatakiwa zikuonyeshe kwamba wewe ni
Mtumishi wa MUNGU, sio maneno tu.
Leo kuna manabii na mitume ambao baadhi kazi yao ni kutapeli
tu watu, hiyo ni hatari sana.
Ndugu, kama Bwana YESU
amekuita hakikisha unamtumikia yeye na sio kutumikia tumbo lako, na sio
kutafuta sifa zako na heshima yako na ufahari wako.
Hubiri wokovu na sio
mafanikio tu ambayo hata wewe hujawahi kuyapata, hivyo wewe wala sio mfano
bora.
Watu wa Kanisa timizeni
wajibu wenu kwa Kanisa na kwa watumishi
wa MUNGU.
Kule unakolishwa Neno la
MUNGU na kuombewa kila mara pakumbuke, watumishi wanaokesha kwa ajili yako ili
ufanikiwe, uwe mzima na ushinde vita wakumbuke sana.
Wako watumishi hujitoa
sana katika kazi ya MUNGU na wanaifanya kwa uaminifu sana lakini Kanisa wala
halina habari na kuwapatia riziki zao, watumishi wamejaa madeni hadi
wanajificha. Ndugu nakuomba husika sana na Mtumishi wa MUNGU anayekusaidia
kiroho kila leo.
Kuna watumishi wengine
wanatamani kuacha kukuhudumia kwa sababu ya maisha yao kuwa magumu sana lakini
hawana jinsi kwa sababu agizo la MUNGU kwao ni kwamba wakuhudumie ili usiende
jehanamu.
Nilisoma kitabu cha Moses
Kulola ambaye mimi Peter nilifunuliwa
kwa ndoto kuwa ndiye mmoja wa wahubiri aliyefanya kazi kubwa zaidi Tanzania,
ni Baba wa kiroho wa maelfu ya wachungaji wakubwa wanaofanya kazi ya MUNGU
vizuri sana leo, Mwalimu wa Mwakasege siku moja nilimsikia akisema kwamba ni
mara kwa mara alikuwa anamtembelea Moses Kulola ili kushauriana, alikuwa hazina
njema sana kwa Tanzania. Lakini katika mambo wa huduma yake kuna kipindi
alijiombea afe maana hakukuwa na chakula na familia yake wanamlilia wakitaka
hata uji, ndipo mtu mmoja asiyejulikana kutoka Kwimba alipomtumia kwa njia ya
posta pesa kidogo na akawa anamtumia kila mwezi, mtu yule aliwahi kumfanyia
huduma na MUNGU akamfungua.
Hivyo kuna watumishi wa
MUNGU wanafanya kazi ya MUNGU katika mazingira magumu sana, sio kwamba MUNGU
hajali bali MUNGU amewakabidhi waumini
kuwategemeza wachungaji wao na ili MUNGU awabariki waumini hao, Katika Kanisa
wengi hawajui. Nigeria kuna mhubiri alitoka Marekani, watu wakajaa uwanja mzima
na Kabla ya matoleo akapata ufunuo kwamba awaambie baadhi ya watu kwamba sadaka
hiyo hiyo waliyopanga kutoa basi wakatoe kwa wachungaji wao Makanisani kwao,
sasa hapo baadhi ya watu walianza kuiona pesa hiyo ni kubwa sana kuwapa
wachungaji wao, lakini kwa mhubiri wa kutoka mbali waliona ni jambo la kawaida
sana. Kanisa kama hilo linahitaji sana kusaidiwa kiroho.
Mchungaji mmoja ambaye ni
rafiki yangu sana alipoona anakoswa hata
chakula na wakati mwingine wanalala njaa familia yake aliamua kuacha utumishi
na kwenda kuomba kazi serikalini na kupata. Akapata kazi lakini MUNGUB akampiga
mapigo akamwambia arudi katika utumishi, alirudi kwenye uchungaji akilia.
Sasa jiulize, MUNGU
alitaka Kanisa kumlisha Mchungaji wao na kumhudumia lakini kanisa lilikuwa
halijitambui japokuwa walikuwa zaidi ya 70.
Ndugu yangu unayesoma
ujumbe huu nakuomba tambua hili ya kwamba una wajibu sana wa kumhudumia Mchungaji wako kwa pesa yako.
Una wajibu wana wa
kumsaidia mtumishi wa MUNGU anayekesha kwa ajili yako ili ufanikiwe.
Wakati mwingine ukimuona
Mtumishi anafundisha soma usidhani somo hilo alilipata tu kienyeji. Kuna masomo
Mengine ili usemeshwe na ROHO MTAKATIFU unahitaji kuwa na muda mwingi wa
kuomba, kuna masomo uandaaji wake tu unaweza kufika masaa manane, kuna
watumishi kila siku wanalala nje ya nyumba zao wakiombea Kanisa la MUNGU, Ni
vyema sana kundi la MUNGU kuwategemeza watumishi hawa ambao wamepewa jukumu na
MUNGU na kuwa waangalizi wa kundi la MUNGU.
Luka 10:7-9 '' Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo,
mkila na kunywa vya kwao; maana, mtenda kazi amestahili kupewa ujira
wake. Msihame-hame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii.
Na mji wo wote mtakaouingia, wakiwakaribisha, vileni vyakula viwekwavyo mbele yenu;
waponyeni wagonjwa waliomo, waambieni, Ufalme wa MUNGU umewakaribia. ''
waponyeni wagonjwa waliomo, waambieni, Ufalme wa MUNGU umewakaribia. ''
Biblia pia inasema kwamba
Mwanafunzi amshirikishe Mwalimu wake katika mema yote wagalatia 6:6 ''Mwanafunzi na amshirikishe mkufunzi wake katika mema yote.
''
Mema yote
ni pamoja na kumtegemeza.
Hata Mtumishi akikuombea
sana na MUNGU akakubariki kwa maombi yake basi mshirikishe kwa mema hayo.
Kuna watumishi hata nguo
tu hawana lakini wameombea watu wengi kupata kazi nzuri na hakika walipata.
Ndugu nakuomba uwe mtu wa
kumshirikisha mema yote unayoyapata huyo Mtumishi wa KRISTO anayekuombea kila
leo.
Inawezekana wewe kila
wiki unaombewa, kila jumapili unaombewa au kila mara unamfuata Mtumishi
akuombee na unafanikiwa sana, basi mshirikishe katika hayo mema yote
uliyobarikiwa.
Mtumishi hana mamlaka ya
kulazimisha kupewa kitu chochote lakini kwa wateule wanaojitambua basi
kuwashirikisha baraka watumishi ni jambo jema sana.
Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane nitakujulisha jinsi ya kukipata.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwana YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
0714252292(Hadi whatsapp).
0786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane nitakujulisha jinsi ya kukipata.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwana YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
0714252292(Hadi whatsapp).
0786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.
Comments