Na Peter M Mabula. Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU |
Bwana YESU
atukuzwe ndugu yangu.
Karibu
tujifunze Neno la MUNGU la uzima.
Uongozi ni
nini?
Uongozi ni
uwezo wa kushawishi watu au kundi ili
kutimiza lengo lililokusudiwa.
Kanisa
linahitaji viongozi wazuri na wanaomcha MUNGU.
Kanisani
viongozi wote wanatakiwa kuwa vielelezo
katika mambo mema.
Katika kikundi chochote Kanisani mfano kwaya,
uinjilisti, idara ya vijana au wamama au watoto n.k kunahitajika viongozi
wazuri wa kiroho.
Jambo
lingine la kujua ni kwamba sio kila mtumishi mzuri Kanisani ni kiongozi mzuri.
Sio watumishi wote wameitwa kuongoza mambo ya kiofisi Kanisani.
Unaweza kuwa
mhubiri mzuri sana lakini ukikabidhiwa idara ya wamama au vijana itakushinda
kwa sababu kuhubiri na uongozi ni vitu viwili tofauti.
Katika kuchagua viongozi tunahitaji MUNGU atusaidie na sio kwenda kwa akili zetu.
Katika kuchagua viongozi tunahitaji MUNGU atusaidie na sio kwenda kwa akili zetu.
1 Samweli
16:7'' Lakini BWANA akamwambia Samweli,
Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi
nimemkataa. BWANA haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu
huitazama sura ya nje, bali BWANA huutazama moyo.
''
Watu wengi
pia hawakai katika nafasi zao zinazoambatana na wito wao ndio maana wanapowekwa
katika nafasi zingine hawafanyi vizuri kwa sababu haziambatani na wito wao.
Leo viongozi
wengi makanisani wanaweza kuwa ni wale walioonekana kwa viongozi wa juu ya sio
wale waliochaguliwa na MUNGU kukaa katika nafasi husika.
Mchungaji
akimkubali mtu fulani kanisani basi anampa uongozi, hiyo ni sawa lakini kama
hamna kusudi la MUNGU ujue kiongozi huyo anaweza kuharibu badala ya kujenga.
Ngoja nikupe
mfano mimi kama Peter natambua kabisa kuna nafasi za kiuongozi kanisani siziwezi
kwa sababu nikipewa zitanizuilia kuandaa masomo na kufanya huduma yangu kwa
ufanisi. Mimi kama mimi, ROHO wa MUNGU alishaniambia kwamba ameniita kufundisha
Neno la MUNGU, sijawahi kusikia sauti nyingine nje na hiyo ya kiutumishi, sasa
inawezekana kabisa kwa viongozi wangu wa Kanisa naweza kuonekana kama mtumishi
ambaye nitafaa sana hivyo unaweza ukapewa hata nafasi mbili au tatu za
kiuongozi kanisani lakini kwa sababu wewe una wito wako basi uongozi unaweza
kuvuruga wito wako.
Sasa katika
Kanisa la MUNGU ni muhimu sana kutafuta mtu ambaye ni kusudi la MUNGU na sio
kutafuta tu mtumishi mzuri, anaweza akawa mtumishi mzuri lakini asiwe kiongozi
mzuri Kanisani.
Inawezekana
pia kanisani ni pahali ambapo hakuna kuwajibishana ndio maana kiongozi anaweza
kuchaguliwa na Mchungaji au Balaza la wazee na akajifanyia vile ambayo yeye
anataka, kuwajibishana kunahitajika sana katika Kanisa la MUNGU.
Wakati
mwingine kama kikundi ndani ya Kanisa mnaweza mkajikuta mnazidiwa ujanja na
shetani wakati wa utekelezaji hivyo aina ya viongozi wazuri hujua nini cha
kufanya ili kuwa washindi siku zote.
Wakati
mwingine kama huna mzigo rohoni na kazi yako utakuwa mtu wa mazoelea tu kwa
sababu umewekwa katika nafasi ambayo huna mzigo nayo. Hivyo kunahitajika
viongozi wenye mzigo na kazi ya MUNGU husika waliyopewa.
Baada ya
hayo sana tuangalie uwezo wa kiongozi mzuri jinsi unavyoonekana.
1. Huonekana
katika maono yake.
Kama ni kiongozi hakikisha una maono mazuri na maono hayo hakikisha yako
sawa na Neno la MUNGU.
Hakikisha una macho ya kuona maono mazuri ambayo utayafanyia kazi.
Yeremia 1:11-12 '' Tena neno la BWANA likanijia, kusema, Yeremia, waona nini? Nikasema, Naona ufito wa mlozi. Ndipo BWANA akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize.''
Hakikisha una macho ya kuona maono mazuri ambayo utayafanyia kazi.
Yeremia 1:11-12 '' Tena neno la BWANA likanijia, kusema, Yeremia, waona nini? Nikasema, Naona ufito wa mlozi. Ndipo BWANA akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize.''
Lazima uwe na maono na utembee katika maono hayo ili kuikuza kazi ya
MUNGU.
2. Kujidhibiti yeye binafsi na kudhibiti tabia
binafsi.
1 Petro 4:2'' Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya MUNGU, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani. ''.
Inawezekana wewe una tabia ya ukali sana, kwenye uongozi wako jidhibiti tabia hiyo maana inaweza kukuondoa katika kundi la viongozi wazuri kiroho katika Kanisa la MUNGU.
1 Petro 4:2'' Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya MUNGU, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani. ''.
Inawezekana wewe una tabia ya ukali sana, kwenye uongozi wako jidhibiti tabia hiyo maana inaweza kukuondoa katika kundi la viongozi wazuri kiroho katika Kanisa la MUNGU.
Ziko tabia binafsi nyingi, wako viongozi wa tabia za kususa kila
akikosewa na wenzake tu kidogo, wako viongozi ambao hawatoi nafasi ya wengine
katika kundi kuchangia maono, wako viongozi wapenda sifa n.k. Ndugu kama
umepewa kuwa kiongozi wa kiroho basi dhibiti tabia zako binafsi maana zinaweza
kulivuruga kundi na wewe usiwe kiongozi mzuri. Tito 1:8
3. Uwezo mzuri huonekana katika maamuzi yake
mazuri.
Warumi 14:13'' Basi tusizidi kuhukumiana, bali afadhali toeni hukumu hii, mtu asitie kitu cha kumkwaza ndugu au cha kumwangusha. ''
Warumi 14:13'' Basi tusizidi kuhukumiana, bali afadhali toeni hukumu hii, mtu asitie kitu cha kumkwaza ndugu au cha kumwangusha. ''
Kama kiongozi ni lazima kuna mahali atatakiwa kutoa maamuzi, sasa maamuzi sahihi yanaweza kumfanya kiongozi awe
mzuri au sio kiongozi mzuri. Maamuzi ya kuwaogopa wanadamu, yanamfanya kiongozi asiwe mzuri.
Maamuzi ya kupendelea baadhi ya watu au marafiki zake, yanamfanya
kiongozi asiwe kiongozi mzuri
Bwana YESU alisema ndio yetu na iwe ndio maana yake tusiwe watu
wasioeleweka, wasio na msimamo, wanaosema mambo ambayo hawatendi. Kiongozi
Kanisani lazima awe anaongozwa na ROHO MTAKATIFU ili kutoa maamuzi sahihi hata
kama maamuzi hayo yatawakwaza marafiki zake, lakini kama ni maamuzi sahihi
basi basi ni heri kuyafanya. Isiwe
kiongozi aamue mfano kwamba ‘’Siku ya jumamosi tutakutana hapa Kanisani kwenda
kushuhudia’’ Kisha baadae rafiki yake mmoja au mke wake au mume wake amwambie
kwamba ‘’Wiki hii tusishuhudie bali tukamtembelee Mchungaji’’ Sasa kama
kiongozi umeshawaambia watu kuhusu kushuhudia na wote wakaenda wakijua kuna
ushuhudiaji na wengine hata wakombea jambo hilo kisha inafika ijumaa unatangaza
tena kwamba ushuhudiaji haupo jumamosi bila sababu ya msingi, unakuwa huna
maamuzi sahihi. Hata kama umeshauriwa jambo jema basi hakikisha unafuata ratiba
njema ya kwanza mliyokubaliana. Angalizo ni hili, Kwa sababu kila Mchungaji
kanisani ndio msimamizi wa idara zote basi mipango yote kabla hujaipeleka kwa
kikundi chako au idara yako hakikisha unamshirikisha Mchungaji ili akibariki
Mchungaji basi asiwepo wa kuzuia maamuzi hayo mema ya kumtumikia MUNGU na kumpa
utukufu.
Kama kiongozi wa aina yeyote Kanisani inakupasa kuwa makini sana katika
maamuzi. unaweza ukawafanya unaowaongoza wakakujua kwamba huna maamuzi sahihi,
hivyo hata ukiwaambia jambo hawatazingatia maana wanajua utabadilika tu.
Usiseme kitu kama huna uhakika nacho ili maamuzi yako yawe sahihi siku
zote yasiyomuonea mtu wala kumpendelea
mtu yeyote.
4. Kiongozi
mzuri ni yule anayeweza kuwasikiliza wengine na kuwaona wa thamani.
Wafilipi 2:3-4 ''Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.''
Wafilipi 2:3-4 ''Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.''
Hii ni changamoto kwa baadhi ya viongozi Makanisani. Kuna viongozi neno
lao ndio la mwisho kwenye kikao. Askofu au Mchungaji au kiongozi wa idara
yeyote akisema jambo ni muhimu sana kusikiliza mawazo ya watu wengine. Kama ni
kwenye kikao hakikisha unasikiliza maoni ya watu wote na sio wewe kuamua mwanzo
tu wa kikao, hivyo hata kama kuna maoni mazuri kuliko yako na yanayoweza
kulisaidia kundi basi hutatoa nafasi ya watu
wengine kukupinga. Mtu akikuita pembeni
baada ya ibada mfano akikushauri jambo ili kuboresha usimpinge. Kuna viongozi
wengine akipingwa kidogo ananuna, hiyo sio sifa nzuri ya kiongozi.
Ni muhimu kutambua kwamba ukiwa kiongozi kanisani au kwenye kikundi chako
au idara yako haina maana ya kwamba wewe ndio una akili kuliko wote
unaowaongoza, ndugu inawezekana nusu nzima ya unaowaongoza wana akili kuliko
wewe, wana maono na mipango mizuri kuliko wewe hivyo wasikilize ushauri wao na
ushauri mzuri fanyia kazi kwa faida ya
kanisa la MUNGU.
Usiwe kiongozi ambaye huwapi nafasi watu kuwasikiliza, kumbuka basi kwamba
tu viungo katika mwili mmoja wa KRISTO.
5. Kiongozi
mzuri ana juhudi kwa MUNGU na katika kazi yake aliyopewa kuongoza.
1 Petro 3:13 ''Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema?''
1 Petro 3:13 ''Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema?''
Wapo viongozi wao huonekana tu
katika vikao vya kiuongozi lakini katika kazi nyingine na utumishi mwingine
kanisani huwezi kuwaona.
Kiongozi mzuri lazima ahusike na ibada siku zote, ahusike na maombi na
mikesha ya maombi.
Usiwe kiongozi ambaye huna juhudi kwa MUNGU. Kumbuka umepewa uongozi ni
katika kazi ya MUNGU, katika Kanisa la KRISTO hivyo maisha yako ni kumwabudu MUNGU Baba katika Roho na kweli
na kumtumikia Bwana YESU.
Kiongozi lazima uwe na juhudi
kubwa katika kazi ya MUNGU hata ambayo haikuhusu.
Usiwe kiongozi wa wamama au vijana au shemasi au mzee wa kanisa na huwa
unatoa michango yako katika idara yako tu lakini kwenye Kanisa hutoi hata mia
maana hutaki Kanisa lifanikiwe ila wewe idara yako tu ndio ifanikiwe.
Usiwe kiongozi mwenye wivu wala husuda. Niliwahi kushuhudia Kanisa fulani
vijana wakifanya sherehe na katika sherehe hiyo walimtegemeza vizuri Mchungaji
wao na kufanya mambo mengi sana mazuri, lakini katika ibada hiyo na matukio
hayo waliokuwa na furaha ni vijana tu lakini wamama na wababa hawakuwa na
furaha kabisa, baadae baada ya ibada mama mmoja nikamsikia akisema ‘’Vijana
wamefanya vizuri katika sherehe yao kuliko sisi’’ Niliwaza sana na kujua kwamba
hapo kuna tatizo.
Mko Kanisa moja lakini imefika wakati hamtaki kikundi kingine kifanikiwe
kuwazidi, YESU hakumuita mtu yeyote katika hayo.
Kwanza Kanisani hatushindani. Ukiwa kiongozi wa namna hiyo
utashangaa kundi lako halifanikiwi kamwe
kwa sababu malengo yako ni kushindana na idara zingine ili muwazidi na kupata
heshima.
Ndugu, fanya kwa sehemu yako na fanya kazi ya MUNGU kwa juhudi lakini
epuka mashindano.
6. Kiongozi
mzuri hafanyii kazi jambo bila kulipima kwanza.
Mithali 18:17 '' Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki; Lakini jirani yake huja na kumchunguza.''
Mithali 18:17 '' Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki; Lakini jirani yake huja na kumchunguza.''
Tuko katika nyakati ambazo watu hugeukageuka hivyo ukiwa kiongozi unayetaka
kumpendeza MUNGU basi usiwe wa kufanyia kazi kila unachoambiwa, hata kama
hakistahili.
Ni kweli kabisa unatakiwa kila mara utoe nafasi ya kuwasikiliza wengine
lakini hakikisha unachuja pumba na
mchele safi.
Sio watu wamekosana na kisha mmoja anakuja kwako mzee wa Kanisa na
kukuambia kwa uongo na hila kwamba
‘’Mpendwa fulani jana alikuwa
disko’’ Wewe mzee wa Kanisa au Mchungaji kesho unasimama madhabahuni na
kutangaza mtu huyo kwamba jana yake alionekana disko hivyo aache mara moja
tabia hiyo, Jambo hilo kama ni la uongo basi hakika utakuwa umebomoa sana na
sio kujenga.
Kiongozi mzuri lazima asikilize watu lakini pale wanapomshawishi
anaowasikiliza ili aamue maamuzi fulani basi awe makini maana kuna ushawishi
mwingine ni tamaa za watu au ushawishi wa kipepo kabisa ili kuvuruga kundi.
Wako watu hadi wamehama makanisani kwa kusingiziwa na kunenewa uongo.
Hata ndoto na maono wanayokuambia watu kuhusu watu wengine usiamue tu dakika
hiyo hiyo hata kama hujui kama ni kweli au uongo.
Kiongozi lazima uwe kama kiongozi sahihi kwa kusikiliza watu na kisha fanyia
kazi hata ujilidhishe kwanza na toa maamuzi kulingana na Biblia na sio mtazamo
wako. Ndugu mmoja alikwenda kwenye mkutano wa injili wa mtumishi fulani, kwa
sababu madhehebu yale hawaelewani basi aliporudi kanisani kwake Mchungaji
alitangaza akisema ‘’Huyu kuanzia sasa muoneni kama mtu wa mataifa maana
amemwasi MUNGU na Kanisa’’
Kuna Madhehebu mengine muumini akihama dhehebu tu wanaanza kumwita mtu wa
mataifa, muasi na ameasi imani.
Ndugu zangu, kumwasi MUNGU ni
kuacha Wokovu wa YESU KRISTO ulio wa
thamani sana na sio kuhama dhehebu. Kama mtu atahamia dhehebu ambalo YESU KRISTO sio Mwokozi basi huyo amejipoteza
mwenyewe, lakini kama mtu husika ameokoka na amehama dhehebu kwa sababu
zake za msingi na kuhamia dhehebu lingine la Wokovu wa
KRISTO vilevile wanaoihubiri kweli ya
MUNGU huyo hajaasi. Sasa viongozi wengi hufanyia kazi mambo yasiyo sahihi na
hayo kuwakosesha wengine.
7. Kiongozi
mzuri wa kiroho hausiki na dhambi na anakemea dhambi.
Kitu cha kwanza kabisa ambacho MUNGU anahitaji kwa Kanisa lake yaani kwa
waliompokea YESU kama Mwokozi wao ni utakatifu.
1 Petro 1:15-16 '' bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;
kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.''
Utakatifu ndio jambo la muhimu zaidi baada ya kuokoka.
Kwa kiongozi ni lazima uwe kielelezo katika mema.
Uongozi wako unaweza kuuharibu
kama unafanya dhambi za siri.
Kuna hadi viongozi wa kiroho wana watoto nje ya ndoa, kiongozi kama huyo
anaweza akafika wakati akasema ‘’Msifuate matendo yangu bali fuateni maneno
yangu’’ Huyo hajitambui kwa sababu ya dhambi, kiongozi kama huyo hafai kuongoza
kundi la MUNGU. Ni heri sana mkachagua kiongozi asiyejua kusoma wala kuandika
lakini ni Mcha MUNGU kuliko kuchagua kiongozi msomi lakini mdhambi.
Kanisa linaweza likatukanwa na watu wa nje kwa sababu yako kiongozi
mtenda dhambi.
Kufanya dhambi kwako kunaweza kuwazuiliwa watu hata kuokoka.
Ukitaka uwe kiongozi mzuri kiroho hakikisha sana unaishi maisha
matakatifu ya Wokovu.
Nyongeza ni hizi;
Ø Huwezi kuwa kiongozi mzuri kama huna
maono mazuri.
Ø Huwezi kufanikiwa kiuongozi kama
hakuna ushirikiano baina yako na
unaowaongoza.
Ø Kiongozi bila ROHO MTAKATIFU na Bila
YESU KRISTO hawezi kuwa kiongozi anayempendeza MUNGU.
Ø Kiongozi anayefanya dhambi hawezi
kuwa kiongozi mzuri wa kiroho.
Ø Kiongozi mwenye tamaa na vitisho
hawezi kuwa kiongozi mzuri wa kiroho.
Ø Kiongozi ambaye Neno la MUNGU sio
kiongozi wake, huyo hawezi kamwe kuiwa kiongozi mzuri
Kwanini uongozi wa kiroho
katika baadhi ya maeneo Makanisani haufanikiwi?
1.
Hofu
ya MUNGU inapoondoka kwa kiongozi husika na kwa anaowaongoza.
Hofu ya MUNGU ni nyezo kuu ya kufanikiwa kwa
Kanisa, idara au kundi katika kazzi ya MUNGU.
2. Kufanyia kazi jambo
jipya , kabla yya jambo la kwanza kumalizika.
Mnaweza mkapanga kujenga
Kanisa kwa mwaka huu, kabla ya mwezi wa 4 mnapanga tena mwaka huu mtamnunulia
Mchungaji Gari, kabla ya mwezi wa 8 mnapanga tena kwamba mwaka huu mtasafiri
kihuduma n.k kwa jinsi hiyo mnaweza mkajikuta mwaka mzima umeisha na hamjafanya
hata moja katika mipango yenu kwa sababu ya kupandikiza mambo.
1 Kor 15:58 ''Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda
kazi ya BWANA sikuzote, kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure
katika BWANA.
''
Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane nitakujulisha jinsi ya kukipata.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwana YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
0714252292(Hadi whatsapp).
0786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.
Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane nitakujulisha jinsi ya kukipata.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwana YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
0714252292(Hadi whatsapp).
0786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.
Comments